Sunday, July 14, 2013
Sinema yangu ya Safari itachukua Tuzo- Richie
Single Mtambalike
Nyota wa sinema za kitanzania, mkongwe Single Mtambalike maarufu kama Richie ametamba kuchukua tuzo kupitia sinema yake mpya ya Safari.
"Nimetayarisha sinema ya Safari kwa umakini, hivyo ni lazima iwe filamu ya kuingia katika tuzo mwaka huu kulingana na ubora wake, hata wasanii walioigiza wameigiza kwa kiwango cha juu," alitamba Richie.
Mkongwe huyo anadai kuwa yeye ni bora kwani ndiye msanii wa kwanza kabisa Tanzania kupewa tuzo na M-net mwaka 2006 huku akisifia utaratibu uliotumika kupatikana mshindi katika tuzo hizo.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment