Lagos, Nigeria
Mwigizaji nyota wa Nigeria Chioma Tolips ametangaza hadharani kuwa hana tena ugomvi kama sio bifu na mwigizaji mwenzake anayejulikana kwa jina Oge Okoye. Bifu hilo lilikuwa la muda mrefu, hivi sasa ameamua kuachana na bifu na kujikita zaidi kwenye biashara zake.
Chioma alizungumza hivyo baada ya kuulizwa na mtandao mmoja wa taariza za sinema za kinaigeria, kuhusiana na bifu hilo kwani lilikuwa gumzo katika vyombo mbali mbali vya habari nchini Nigeria kwa kipindi kirefu.
Kwa mujibu wa maelezo yake Chioma amesema amewasamehe watu wote waliomfanyia mabaya, akiwemo Oge Okoye ambaye alisumbuana naye kwa muda mrefu.
" Ukweli ni kwamba siwezi kuongea chochote kuhusu Oge kwani, nimemsamehe kutoka moyoni. Tena si yeye tu hata waengine waliowahji kuniendea kinyume,"alisema Chioma mwanadada mwenye umbo kubwa la kuvutia.
Hata hivyo amedai kwamba kilichotokea ni kama darasa, yaani amejifunza kutokana na tatizo hilo, hivi anaendelea na shughuli zake.
No comments:
Post a Comment