Kinyembe
Komediani anayetamba kwa kubadilisha sura na sauti yake katika filamu za uchekeshaji anazocheza, Mohamed Abdallah a.k.a Kinyembe amesema licha ya kuisha na kuigiza Dar lakini anapenda kuishi mkoa kwake Mbeya.
Amesema kumekuwa na tabia ya waigizaji wengi wakifanikiwa kupata majina makubwa wanahama mikoani na kuja kuishi Dar.
Yoyote anayetaka kufanya kazi na Kinyembe hana budi kufunga safari mpaka Mbeya kwa ajili ya kufanya naye. Ni mwigizaji anayeonekana kwa sana katika michezo ya vituko show kupitia televisheni ya Channel Ten.
No comments:
Post a Comment