Saturday, July 13, 2013

Auntie Ezekiel aibuka kwenye bongo fleva

                                                   Auntie Ezekiel katika moja ya pozi lake
                                                    Auntie Ezekiel katika  pozi jingine

Baada ya kujipatia umaarufu mkubwa katika uigizaji, mwanadada nguli katika uigizaji wa sinema za kibongo, Auntie Ezekiel ameamua kujikita katika muziki, baada ya kushirikishwa kwenye wimbo unaoitwa Movie Star wa January Joseph a.k.a January Eleven.
Kwa mujibu wa maelezo yake, Auntie Ezekiel amesema ana mambo mengi anayotaka kufanya katika muziki, ila kwa sasa hajawa tayari kuweka wazi mambo hayo. Ila anasubiri kuona namna mashabiki watakavyompokea.
"Nimeamua kuwaonyesha mashabiki na wapenzi wangu kwamba ninaweza kufanya muziki, kama nikubalika nitaamua kujiingiza moja kwa moja kwenye muziki. Ila naamini kama nitapokewa vizuri na kukubakli," alisema nyota huyo wa sinema ya Sound of death.
Kama Auntie Ezekiel ataingia moja kwa moja katika muziki, atakuwa anaungana na waigizaji wengine walioamua kujiingiza kwenye muziki kama vile Zuwena Mohamed maarufu kama Shilole, Salma Jabu maarufu kama Nisha, Flora Mvungi na Snura Mushi. 

No comments:

Post a Comment