Showing posts with label bongo. Show all posts
Showing posts with label bongo. Show all posts
Friday, November 28, 2014
Wema bado ni kipenzi cha wabongo kila anachofanya wanashabikia
Bila ya kupindisha ukweli mwigizaji Wema Sepetu ni miongoni mwa waigizaji wenye nyota kali sana kwa wapenzi na mashabiki, ukitaka kudhibitisha hilo angalia magazeti ya udaku yakiwa na picha yake sambamba na stori yake. watu wengi kwenye daladala utawaona wanamagazeti hayo wanasoma. Udhibitisho mwingine angalia idadi ya wasomaji na watazamaji wa video zinazomuhusu yeye katika blog mbali mbali ni kubwa kuliko waigizaji wengine. Udhibitisho mwingine jaribu kuchungu wale watu waliokuwa karibu yake walivyojipatia umaarufu kubwa, baada ya kuachana nao wengi wao wanapoteza umaarufu. Kama unataka kuwa maarufu jipendekeze kwa Wema hata kwa kubeba mkoba wake au kumfuta jasho, siku tatu ya kuwa naye tayari utapamba katika kurasa za magazeti ya udaku. Wema bado ni kipenzi cha wabongo, habari ndiyo.
Saturday, July 13, 2013
Auntie Ezekiel aibuka kwenye bongo fleva
Auntie Ezekiel katika moja ya pozi lake
Auntie Ezekiel katika pozi jingine
Baada ya kujipatia umaarufu mkubwa katika uigizaji, mwanadada nguli katika uigizaji wa sinema za kibongo, Auntie Ezekiel ameamua kujikita katika muziki, baada ya kushirikishwa kwenye wimbo unaoitwa Movie Star wa January Joseph a.k.a January Eleven.
Kwa mujibu wa maelezo yake, Auntie Ezekiel amesema ana mambo mengi anayotaka kufanya katika muziki, ila kwa sasa hajawa tayari kuweka wazi mambo hayo. Ila anasubiri kuona namna mashabiki watakavyompokea.
"Nimeamua kuwaonyesha mashabiki na wapenzi wangu kwamba ninaweza kufanya muziki, kama nikubalika nitaamua kujiingiza moja kwa moja kwenye muziki. Ila naamini kama nitapokewa vizuri na kukubakli," alisema nyota huyo wa sinema ya Sound of death.
Kama Auntie Ezekiel ataingia moja kwa moja katika muziki, atakuwa anaungana na waigizaji wengine walioamua kujiingiza kwenye muziki kama vile Zuwena Mohamed maarufu kama Shilole, Salma Jabu maarufu kama Nisha, Flora Mvungi na Snura Mushi.
Auntie Ezekiel katika pozi jingine
Baada ya kujipatia umaarufu mkubwa katika uigizaji, mwanadada nguli katika uigizaji wa sinema za kibongo, Auntie Ezekiel ameamua kujikita katika muziki, baada ya kushirikishwa kwenye wimbo unaoitwa Movie Star wa January Joseph a.k.a January Eleven.
Kwa mujibu wa maelezo yake, Auntie Ezekiel amesema ana mambo mengi anayotaka kufanya katika muziki, ila kwa sasa hajawa tayari kuweka wazi mambo hayo. Ila anasubiri kuona namna mashabiki watakavyompokea.
"Nimeamua kuwaonyesha mashabiki na wapenzi wangu kwamba ninaweza kufanya muziki, kama nikubalika nitaamua kujiingiza moja kwa moja kwenye muziki. Ila naamini kama nitapokewa vizuri na kukubakli," alisema nyota huyo wa sinema ya Sound of death.
Kama Auntie Ezekiel ataingia moja kwa moja katika muziki, atakuwa anaungana na waigizaji wengine walioamua kujiingiza kwenye muziki kama vile Zuwena Mohamed maarufu kama Shilole, Salma Jabu maarufu kama Nisha, Flora Mvungi na Snura Mushi.
Saturday, February 16, 2013
Bongo movie, Sinema bila Staa huwezi kuuza
Jamila chipukizi anayekuja juu
Baadhi ya wasambazaji wa sinema nchini,
wameibuka na kituko
kitakachosambaratisha soko la sinema za kibongo, kama hawatakubali kuachana na mawazo yao mgando ya kudai sinema bila ya
msanii maarufu huwezi kuuza.
Uchunguzi wetu
umeonyesha kabla ya kuwa na wasanii
maarufu, watanzania walikuwa wakinunua
sinema na kuangalia, wapo waliokuwa
wakinunua sinema za kihindi bila ya kuwafahamu waigizaji hao kama
maarufu au sio maarufu.
Wapo waliokuwa wakinunua sinema za kichina, kijapan na
kizungu. Baada ya kuingia sinema za kinaigeria watanzania walizinunua, walipokuwa wananunua hawakujua kama wasanii hao ni maarufu, ila walinunua kwa ajili ya
kupata burudani ya sinema.
Kama wasambazaji wa nchi nyingine wangekuwa na mawazao kama ya wasambazaji wetu. Tusingeshuhudia waigizaji wapya wakiibuka kila kukicha.
Tungeendelea kushuhudia wale wale wa zamani ambao umri umeanza kuwatupa
mkono.
Wasambazaji wanatakiwa kufahamu kama
waigizaji wanaitwa mastaa hivi sasa, kuna watu wamewafikisha hapo, hawakuzaliwa wakiwa mastaa. Mnatakiwa na
nyinyi kuzalisha wapya sio kutafuta mastaa walitengenezwa na wenzenu.
Friday, February 15, 2013
Anna Michael utakumbukwa daima kwenye Movie bongo, Tanzania
Jina
kama Sina alilotambanalo katika kikundi cha Kidedea au Tunu alilovuma nalo
katika sinema ya I love you,ni kilelezo tosha
kama uwezo wa Anna Michael katika sanaa ya kuigiza ulikuwa wa kiwango
cha juu.
Majina
hayo yalitaka kufuta jina lake halisi la Anna Michael, alilopewa na wazazi
wake. Wahenga walisema kila kilichokuwa kizuri hakidumu sana, ni kauli
inayowakilisha ukweli wa machungu yanayouma. Lakini yote ni mipango ya mwenyezi
mungu.
Licha
ya wazazi wake, mtoto wake, ndugu, marafiki, waigizaji wenzake, wapenzi na
mashabiki wake walimpenda, lakini mungu alimpenda zaidi na kumchukua.
Ni
miaka minne sasa tangu Anna Michael hatutoke kimwili na kiroho lakini kazi zake
zitaendelea kuwepo katika maisha yetu ya kila siku.
Kila
utakapotazama sinema ya Uwanja wa dhambi, I love you, Picnic na Confess.
Utaweza kujionea kipaji alichobahatika kuwa nacho marehemu.
Wasanii
wanaochipukia wangetafuta sinema alizocheza waweze kujifunza mambo muhimu.
Marehemu
alikuwa anavaa taswira anayotakiwa kucheza, ni vigumu kwa sasa kupata wasanii
wenye uwezo huo. Wengi wanapoteza uhalisi wanapoigiza.
Subscribe to:
Posts (Atom)


