Showing posts with label Movie. Show all posts
Showing posts with label Movie. Show all posts

Tuesday, February 19, 2013

Movie Tanzania, Inawezekana kila mwigizaji kutayarisha sinema?

  Inawezekana kila mwigizaji kuwa mtayarishaji wa sinema. Jibu linaweza kuwa ndio au hapana, kwa sababu utayarishaji wa sinema unaweza kufanywa na mdau yoyote mwenye uwezo wa fedha, ila awe anajua sanaa ya sinema kwa undani zaidi. Vinginevyo anaweza kuingia mikononi mwa wababaishaji na kujikuta akipoteza muda na fedha.

Mwigizaji anaweza kutayarisha sinema ila ni lazima awe na upeo mkubwa wa kutayarisha sio kuigiza, unaweza kuwa mwigizaji mzuri lakini ukashindwa kuwa mtayarishaji au muongozaji mzuri yaani director mzuri.

Wapo madirector wazuri sana, lakini hawawezi kuigiza. Kwa sababu hawana taranta au tunaweza kuita kipaji, wapo waandishi wazuri wa hadithi na vitabu, lakini hawawezi kuandika script.

Wapo wachezaji wazuri wa soka lakini hawezi kuwa makocha wazuri, wapo makocha wazuri lakini hawakuwahi kucheza mpira kwa kiwango cha kuitwa mastaa. Kwa hiyo ni vizuri kujikagua kama una taranta kabla ya kufanya chochote unachotaka kufanya.

Wapo waigizaji wenye taranta ya kutayarisha sinema na kuziongoza vizuri, mfano mwigizaji Mel Colm Cille Gerard Gibson wa Marekani, wengi wanamfahamu kwa Mel Gibson ni mwigizaji, mtayarishaji, mwandishi wa script na muongozaji. Moja ya sinema aliyoongoza ni Apocalypto

Marekani na Ulaya wapo wengi wenye uwezo wa kufanya yote katika utengenezaji wa sinema, pia wapo ambao hawawezi. Wanatoa nafasi kwa wenzao wanaoweza.
Kwa Tanzania hali ni tofauti, wengi hawawezi kutayarisha sinema wala kuziongoza. Ila wanajilazimisha kufanya hivyo kwa sababu wanajiona mastaa, ukweli unabaki kama sinema wanazotayarisha zinakuwa hazina ubora unaotakiwa.

Ukijiona huna uwezo wa kuandika script, kutayarisha na kuongoza. Tafuta wadau wenye uwezo wa kufanya kazi hizo kwa ajili ya kupata sinema nzuri. Matokeo ya kila kitu kutaka kufanya mwenyewe ni kutayarisha kazi mbovu.

Aliyekupa fedha za kutayarisha sinema akigundua sinema yako haipendwi na watazamaji, atakumwaga na hatimaye kupotea katika soko la sinema kabisa.

Kama lengo la wadau ni kuendeleza sekta ya uigizaji, waigizaji wanaopata bahati ya kuingia mikataba na wasambazaji kwa ajili ya kutayarisha sinema, wasiwe wabinafsi. Kuendekeza ubinafsi ni kuua sekta sinema, inayoongoza hivi sasa kwa kutoa ajira kwa vijana na wazee.
 
 
 
 

Saturday, February 16, 2013

Movie Kitanzania bila mastaa haziuziki?


Baadhi ya wasambazaji wa sinema  nchini,  wameibuka na  kituko kitakachosambaratisha soko la sinema za kibongo, kama  hawatakubali kuachana  na mawazo yao mgando ya kudai sinema bila ya msanii maarufu huwezi kuuza.

Uchunguzi  wetu umeonyesha  kabla ya kuwa na wasanii maarufu, watanzania walikuwa  wakinunua sinema na kuangalia,  wapo waliokuwa wakinunua sinema za kihindi bila ya kuwafahamu waigizaji hao kama maarufu au sio maarufu.

Wapo waliokuwa wakinunua sinema za kichina, kijapan na kizungu. Baada ya kuingia sinema za kinaigeria watanzania walizinunua,  walipokuwa wananunua hawakujua kama wasanii hao ni maarufu, ila walinunua kwa ajili ya kupata burudani ya sinema.

Kama wasambazaji wa nchi nyingine wangekuwa na mawazao kama ya wasambazaji wetu. Tusingeshuhudia  waigizaji wapya wakiibuka kila kukicha. Tungeendelea kushuhudia wale wale wa zamani ambao umri umeanza kuwatupa mkono. 

Wasambazaji wanatakiwa kufahamu kama waigizaji wanaitwa mastaa hivi sasa, kuna watu wamewafikisha hapo,  hawakuzaliwa wakiwa mastaa. Mnatakiwa na nyinyi kuzalisha wapya sio kutafuta mastaa walitengenezwa na wenzenu.


Bongo movie, Sinema bila Staa huwezi kuuza




                                                         Jamila chipukizi anayekuja juu
Baadhi ya wasambazaji wa sinema  nchini,  wameibuka na  kituko kitakachosambaratisha soko la sinema za kibongo, kama  hawatakubali kuachana  na mawazo yao mgando ya kudai sinema bila ya msanii maarufu huwezi kuuza.

Uchunguzi  wetu umeonyesha  kabla ya kuwa na wasanii maarufu, watanzania walikuwa  wakinunua sinema na kuangalia,  wapo waliokuwa wakinunua sinema za kihindi bila ya kuwafahamu waigizaji hao kama maarufu au sio maarufu.

Wapo waliokuwa wakinunua sinema za kichina, kijapan na kizungu. Baada ya kuingia sinema za kinaigeria watanzania walizinunua,  walipokuwa wananunua hawakujua kama wasanii hao ni maarufu, ila walinunua kwa ajili ya kupata burudani ya sinema.

Kama wasambazaji wa nchi nyingine wangekuwa na mawazao kama ya wasambazaji wetu. Tusingeshuhudia  waigizaji wapya wakiibuka kila kukicha. Tungeendelea kushuhudia wale wale wa zamani ambao umri umeanza kuwatupa mkono. 

Wasambazaji wanatakiwa kufahamu kama waigizaji wanaitwa mastaa hivi sasa, kuna watu wamewafikisha hapo,  hawakuzaliwa wakiwa mastaa. Mnatakiwa na nyinyi kuzalisha wapya sio kutafuta mastaa walitengenezwa na wenzenu.


Friday, February 15, 2013

Anna Michael utakumbukwa daima kwenye Movie bongo, Tanzania




                                            Marehemu Anna Michael enzi ya uhai wake                                 
Jina kama Sina alilotambanalo katika kikundi cha Kidedea au Tunu alilovuma nalo katika sinema ya I love you,ni kilelezo tosha  kama uwezo wa Anna Michael katika sanaa ya kuigiza ulikuwa wa kiwango cha juu.

Majina hayo yalitaka kufuta jina lake halisi la Anna Michael, alilopewa na wazazi wake. Wahenga walisema kila kilichokuwa kizuri hakidumu sana, ni kauli inayowakilisha ukweli wa machungu yanayouma. Lakini yote ni mipango ya mwenyezi mungu.

Licha ya wazazi wake, mtoto wake, ndugu, marafiki, waigizaji wenzake, wapenzi na mashabiki wake walimpenda, lakini mungu alimpenda zaidi na kumchukua.

Ni miaka minne sasa tangu Anna Michael hatutoke kimwili na kiroho lakini kazi zake zitaendelea kuwepo katika maisha yetu ya kila siku.

Kila utakapotazama sinema ya Uwanja wa dhambi, I love you, Picnic na Confess. Utaweza kujionea kipaji alichobahatika kuwa nacho marehemu.

Wasanii wanaochipukia wangetafuta sinema alizocheza waweze kujifunza mambo muhimu.

Marehemu alikuwa anavaa taswira anayotakiwa kucheza, ni vigumu kwa sasa kupata wasanii wenye uwezo huo. Wengi wanapoteza uhalisi wanapoigiza.

Kuna wale wanaopoteza uhalisi wa sauti, muonekana na hata mavazi. Kazi kwenu wasanii chipukizi. 

Monday, February 11, 2013

Soko la Sinema za kinaigeria la shuka nchini, Tanzania

 
                 Mastaa wa sinema za kinaigeria katika picha ya pamoja Waigizaji wa Nigeria
 
                                                                        Mastaa wa Kinageria       
Kabla ya soko la sinema za kitanzania kupata umaarufu, sinema za kinaigeria zilikuwa na mvuto mkubwa sana nchini, hivi sasa zimepoteza umaarufu wake. Watanzania wengi wamezinduka na kuanza kupenda sinema zinazotayarishwa nchini na waigizaji wa kitanzania. Japokuwa sinema za kitanzania zinamapungufu mengi, bado watanzania wanazipenda.

Kinachotakiwa kufanywa na watayarishaji wa sinema ni  kuwa makini wanapoanza kutayarisha. Ili kukwepa makosa ya kijinga ambayo hayahitaji elimu ya chuo kikuu kuweza kuyabaini.

Watayarishaji, waigizaji, waongozaji, waandishi wa script sambamba na wadau wa sinema wasipokuwa makini. Wanaweza kusababisha sinema za nje ya Tanzania kama vile wanaigeria, waghana na waafrika kusini kurudi katika chat ya juu.Kama ikitokea hivyo soko la sinema la kitanzania litapotea kama sio kusambarataika kabisa.

Nurati ndani ya movie ya Julio na Romeo Tanzania


Kikundi cha Alwatan Artist Theater kimemtambulisha muigizaji mpya anayeitwa Nurati Ngereshi katika sinema yake ya Julio na Romeo inayotarajia kuingia sokoni hivi karibuni.

Kabla ya kuanza kuigiza, Nurati alikuwa akihakiki script za kundi hilo, lenye makao yake makuu Ilala Kimako. Sinema zote za kundi hilo utakutana na jina lake kwenye nafasi ya script editor.

Kwa vile stori ya Julio na Romeo lilikuwa ni wazo lake, alilomsimulia mwandishi wa script, baada ya kuandikwa alishauriwa kucheza

Katika sinema hiyo ameshiriki kama msichana anayempinga mdogo wake wa kiume anayeitwa Julio kumuoa msichana anayeitwa Romeo.

Wakati huo huo alikuwa akimshawishi rafiki yake Tunda aliyerejea nchini toka Marekani kuolewa na mdogo wake Julio. Ni sinema nzuri yenye mafunzo kwa jamii, inaweza kuangaliwa na watu wa rika zote.

Sinema Tanzania, Inakuwaje movie zake kuwa na majina ya kizungu


Wapenzi na mashabiki waliobahatika kuongea na mtandao wa Swahili Cinema News, wamesema sinema za kitanzania kuwa na majina ya kizungu, ni ushamba na ulimbukeni wa hali ya juu.

“ Binafsi yangu sijawahi kuona sinema ya kihindi yenye jina la kizungu, au sinema ya kichina, Kijapan na kiarabu  zenye majina ya kizungu. Kama zipo itakuwa na jina la kizungu na jina la lugha yao" alisema Joshua Daniel.

Bi Sauda Ramadhani amesema sinema zilizotoka mwanzo zilikuwa nzuri, zilizingatia maadili ya kitanzania kuanzia stori, uvaaji, uchezaji na jina la sinema kuwa katika lugha ya kiswahili.

Alizitaja sinema hizo ni Nsyuka, Fungu la kukosa, Ngome ya Mwanamalundi, Lazima ufe Joram, Mambo ya ngoswe na nyingine nyingi za wakati huo.

“ Baada ya kuingia watayarishaji wanaopenda kuona mapaja ya watoto wetu wa kike, wakabadili mfumo wa utengenezaji sinema kwa kuandika majina ya kizungu.Kuwavisha nguo za ajabu mabinti wetu na kuwalazimisha kupigana mabusu, yaani huwezi kuangalia na watoto zako." Alisisitiza Bi Sauda.

Jaffar amesema kabla ya kina Ray, Tino, Johari, Mainda, Teya, Tito, Swebe, Maya, Zawadi, Nora, Nina na wengine, hawajaanza kuigiza sinema.

Walikuwa wakizingatia maadili katika michezo yao ya kwenye televisheni. Baada ya kuanza kujiunga na makampuni ya kutayarisha sinema, walibadilika kimaadili na kuanza kuvaa taswira ya kishetani. Taswira iliyowachukiza watazamaji wao.

“ Binafsi nilichukizwa na muonekano wao mpya, kwanza walikuwa wanaiga maadili ya kinaigeria kuanzia stori mpaka uchezaji." Alidai Jaffar.