Inawezekana kila mwigizaji kuwa mtayarishaji wa sinema. Jibu linaweza kuwa ndio au hapana, kwa sababu utayarishaji wa sinema unaweza kufanywa na mdau yoyote mwenye uwezo wa fedha, ila awe anajua sanaa ya sinema kwa undani zaidi. Vinginevyo anaweza kuingia mikononi mwa wababaishaji na kujikuta akipoteza muda na fedha.
Mwigizaji anaweza kutayarisha sinema ila ni lazima awe na upeo mkubwa wa kutayarisha sio kuigiza, unaweza kuwa mwigizaji mzuri lakini ukashindwa kuwa mtayarishaji au muongozaji mzuri yaani director mzuri.
Wapo madirector wazuri sana, lakini hawawezi kuigiza. Kwa sababu hawana taranta au tunaweza kuita kipaji, wapo waandishi wazuri wa hadithi na vitabu, lakini hawawezi kuandika script.
Wapo wachezaji wazuri wa soka lakini hawezi kuwa makocha wazuri, wapo makocha wazuri lakini hawakuwahi kucheza mpira kwa kiwango cha kuitwa mastaa. Kwa hiyo ni vizuri kujikagua kama una taranta kabla ya kufanya chochote unachotaka kufanya.
Wapo waigizaji wenye taranta ya kutayarisha sinema na kuziongoza vizuri, mfano mwigizaji Mel Colm Cille Gerard Gibson wa Marekani, wengi wanamfahamu kwa Mel Gibson ni mwigizaji, mtayarishaji, mwandishi wa script na muongozaji. Moja ya sinema aliyoongoza ni Apocalypto
Marekani na Ulaya wapo wengi wenye uwezo wa kufanya yote katika utengenezaji wa sinema, pia wapo ambao hawawezi. Wanatoa nafasi kwa wenzao wanaoweza.
Kwa Tanzania hali ni tofauti, wengi hawawezi kutayarisha sinema wala kuziongoza. Ila wanajilazimisha kufanya hivyo kwa sababu wanajiona mastaa, ukweli unabaki kama sinema wanazotayarisha zinakuwa hazina ubora unaotakiwa.
Ukijiona huna uwezo wa kuandika script, kutayarisha na kuongoza. Tafuta wadau wenye uwezo wa kufanya kazi hizo kwa ajili ya kupata sinema nzuri. Matokeo ya kila kitu kutaka kufanya mwenyewe ni kutayarisha kazi mbovu.
Aliyekupa fedha za kutayarisha sinema akigundua sinema yako haipendwi na watazamaji, atakumwaga na hatimaye kupotea katika soko la sinema kabisa.
Kama lengo la wadau ni kuendeleza sekta ya uigizaji, waigizaji wanaopata bahati ya kuingia mikataba na wasambazaji kwa ajili ya kutayarisha sinema, wasiwe wabinafsi. Kuendekeza ubinafsi ni kuua sekta sinema, inayoongoza hivi sasa kwa kutoa ajira kwa vijana na wazee.
Showing posts with label Movie. Show all posts
Showing posts with label Movie. Show all posts
Tuesday, February 19, 2013
Saturday, February 16, 2013
Movie Kitanzania bila mastaa haziuziki?
Baadhi ya wasambazaji wa sinema nchini, wameibuka na kituko kitakachosambaratisha soko la sinema za kibongo, kama hawatakubali kuachana na mawazo yao mgando ya kudai sinema bila ya msanii maarufu huwezi kuuza.
Uchunguzi wetu umeonyesha kabla ya kuwa na wasanii maarufu, watanzania walikuwa wakinunua sinema na kuangalia, wapo waliokuwa wakinunua sinema za kihindi bila ya kuwafahamu waigizaji hao kama maarufu au sio maarufu.
Wapo waliokuwa wakinunua sinema za kichina, kijapan na kizungu. Baada ya kuingia sinema za kinaigeria watanzania walizinunua, walipokuwa wananunua hawakujua kama wasanii hao ni maarufu, ila walinunua kwa ajili ya kupata burudani ya sinema.
Kama wasambazaji wa nchi nyingine wangekuwa na mawazao kama ya wasambazaji wetu. Tusingeshuhudia waigizaji wapya wakiibuka kila kukicha. Tungeendelea kushuhudia wale wale wa zamani ambao umri umeanza kuwatupa mkono.
Wasambazaji wanatakiwa kufahamu kama waigizaji wanaitwa mastaa hivi sasa, kuna watu wamewafikisha hapo, hawakuzaliwa wakiwa mastaa. Mnatakiwa na nyinyi kuzalisha wapya sio kutafuta mastaa walitengenezwa na wenzenu.
Bongo movie, Sinema bila Staa huwezi kuuza
Jamila chipukizi anayekuja juu
Baadhi ya wasambazaji wa sinema nchini,
wameibuka na kituko
kitakachosambaratisha soko la sinema za kibongo, kama hawatakubali kuachana na mawazo yao mgando ya kudai sinema bila ya
msanii maarufu huwezi kuuza.
Uchunguzi wetu
umeonyesha kabla ya kuwa na wasanii
maarufu, watanzania walikuwa wakinunua
sinema na kuangalia, wapo waliokuwa
wakinunua sinema za kihindi bila ya kuwafahamu waigizaji hao kama
maarufu au sio maarufu.
Wapo waliokuwa wakinunua sinema za kichina, kijapan na
kizungu. Baada ya kuingia sinema za kinaigeria watanzania walizinunua, walipokuwa wananunua hawakujua kama wasanii hao ni maarufu, ila walinunua kwa ajili ya
kupata burudani ya sinema.
Kama wasambazaji wa nchi nyingine wangekuwa na mawazao kama ya wasambazaji wetu. Tusingeshuhudia waigizaji wapya wakiibuka kila kukicha.
Tungeendelea kushuhudia wale wale wa zamani ambao umri umeanza kuwatupa
mkono.
Wasambazaji wanatakiwa kufahamu kama
waigizaji wanaitwa mastaa hivi sasa, kuna watu wamewafikisha hapo, hawakuzaliwa wakiwa mastaa. Mnatakiwa na
nyinyi kuzalisha wapya sio kutafuta mastaa walitengenezwa na wenzenu.
Friday, February 15, 2013
Anna Michael utakumbukwa daima kwenye Movie bongo, Tanzania
Jina
kama Sina alilotambanalo katika kikundi cha Kidedea au Tunu alilovuma nalo
katika sinema ya I love you,ni kilelezo tosha
kama uwezo wa Anna Michael katika sanaa ya kuigiza ulikuwa wa kiwango
cha juu.
Majina
hayo yalitaka kufuta jina lake halisi la Anna Michael, alilopewa na wazazi
wake. Wahenga walisema kila kilichokuwa kizuri hakidumu sana, ni kauli
inayowakilisha ukweli wa machungu yanayouma. Lakini yote ni mipango ya mwenyezi
mungu.
Licha
ya wazazi wake, mtoto wake, ndugu, marafiki, waigizaji wenzake, wapenzi na
mashabiki wake walimpenda, lakini mungu alimpenda zaidi na kumchukua.
Ni
miaka minne sasa tangu Anna Michael hatutoke kimwili na kiroho lakini kazi zake
zitaendelea kuwepo katika maisha yetu ya kila siku.
Kila
utakapotazama sinema ya Uwanja wa dhambi, I love you, Picnic na Confess.
Utaweza kujionea kipaji alichobahatika kuwa nacho marehemu.
Wasanii
wanaochipukia wangetafuta sinema alizocheza waweze kujifunza mambo muhimu.
Marehemu
alikuwa anavaa taswira anayotakiwa kucheza, ni vigumu kwa sasa kupata wasanii
wenye uwezo huo. Wengi wanapoteza uhalisi wanapoigiza.
Monday, February 11, 2013
Soko la Sinema za kinaigeria la shuka nchini, Tanzania


Kabla ya soko la sinema za kitanzania kupata umaarufu, sinema za kinaigeria zilikuwa na mvuto mkubwa sana nchini, hivi sasa zimepoteza umaarufu wake. Watanzania wengi wamezinduka na kuanza kupenda sinema zinazotayarishwa nchini na waigizaji wa kitanzania. Japokuwa sinema za kitanzania zinamapungufu mengi, bado watanzania wanazipenda.
Kinachotakiwa kufanywa na watayarishaji wa sinema ni kuwa makini wanapoanza kutayarisha. Ili kukwepa makosa ya kijinga ambayo hayahitaji elimu ya chuo kikuu kuweza kuyabaini.
Watayarishaji, waigizaji, waongozaji, waandishi wa script sambamba na wadau wa sinema wasipokuwa makini. Wanaweza kusababisha sinema za nje ya Tanzania kama vile wanaigeria, waghana na waafrika kusini kurudi katika chat ya juu.Kama ikitokea hivyo soko la sinema la kitanzania litapotea kama sio kusambarataika kabisa.
Nurati ndani ya movie ya Julio na Romeo Tanzania
Kikundi cha Alwatan Artist
Theater kimemtambulisha muigizaji mpya anayeitwa Nurati Ngereshi katika sinema
yake ya Julio na Romeo inayotarajia kuingia sokoni hivi karibuni.
Kabla ya kuanza kuigiza,
Nurati alikuwa akihakiki script za kundi hilo, lenye makao yake makuu Ilala
Kimako. Sinema zote za kundi hilo utakutana na jina lake kwenye nafasi ya
script editor.
Kwa vile stori ya Julio na
Romeo lilikuwa ni wazo lake, alilomsimulia mwandishi wa script, baada ya
kuandikwa alishauriwa kucheza
Katika sinema hiyo
ameshiriki kama msichana anayempinga mdogo wake wa kiume anayeitwa Julio kumuoa
msichana anayeitwa Romeo.
Wakati huo huo alikuwa
akimshawishi rafiki yake Tunda aliyerejea nchini toka Marekani kuolewa na mdogo
wake Julio. Ni sinema nzuri yenye mafunzo kwa jamii, inaweza kuangaliwa na watu
wa rika zote.
Sinema Tanzania, Inakuwaje movie zake kuwa na majina ya kizungu
Wapenzi
na mashabiki waliobahatika kuongea na mtandao wa Swahili Cinema News, wamesema
sinema za kitanzania kuwa na majina ya kizungu, ni ushamba na ulimbukeni wa
hali ya juu.
“
Binafsi yangu sijawahi kuona sinema ya kihindi yenye jina la kizungu, au sinema
ya kichina, Kijapan na kiarabu zenye
majina ya kizungu. Kama zipo itakuwa na jina la kizungu na jina la lugha
yao" alisema Joshua Daniel.
Bi
Sauda Ramadhani amesema sinema zilizotoka mwanzo zilikuwa nzuri, zilizingatia
maadili ya kitanzania kuanzia stori, uvaaji, uchezaji na jina la sinema kuwa
katika lugha ya kiswahili.
Alizitaja
sinema hizo ni Nsyuka, Fungu la kukosa, Ngome ya Mwanamalundi, Lazima ufe
Joram, Mambo ya ngoswe na nyingine nyingi za wakati huo.
“
Baada ya kuingia watayarishaji wanaopenda kuona mapaja ya watoto wetu wa kike,
wakabadili mfumo wa utengenezaji sinema kwa kuandika majina ya
kizungu.Kuwavisha nguo za ajabu mabinti wetu na kuwalazimisha kupigana mabusu,
yaani huwezi kuangalia na watoto zako." Alisisitiza Bi Sauda.
Jaffar
amesema kabla ya kina Ray, Tino, Johari, Mainda, Teya, Tito, Swebe, Maya, Zawadi,
Nora, Nina na wengine, hawajaanza kuigiza sinema.
Walikuwa
wakizingatia maadili katika michezo yao ya kwenye televisheni. Baada ya kuanza
kujiunga na makampuni ya kutayarisha sinema, walibadilika kimaadili na kuanza
kuvaa taswira ya kishetani. Taswira iliyowachukiza watazamaji wao.
“
Binafsi nilichukizwa na muonekano wao mpya, kwanza walikuwa wanaiga maadili ya
kinaigeria kuanzia stori mpaka uchezaji." Alidai Jaffar.
Subscribe to:
Posts (Atom)
