Showing posts with label Romeo. Show all posts
Showing posts with label Romeo. Show all posts

Saturday, February 16, 2013

Madirector wanachangia muvi kukosa uhalisia



Mwigizaji wa sinema ya Julio na Romeo, Nurati Ngeleshi alisikika akiwashutumu waongozaji wa movie a.k.a madirector kwa kushindwa kuwalazimisha waigizaji kuvaa uhusika wa nafasi wanazocheza.

Hakuna kitu kinachonikera kama waigizaji wa kike kuvaa vimini sehemu hisiyostahili."  Akasema director mwenye umakini na kazi hawezi kukubali kitu kama hicho.

Inawezekana alichoongea Nurati kitawaboa wengi, ukweli utabaki pale pale kama madirector wanachangia kupoteza uhalisia wa sinema zetu kwa kuogopa kuwaeleza waigizaji ukweli wa kuvaa taswira ya nafasi aliyopewa.

Katika utayarishaji wa sinema director ni mtu wa mwisho katika kufanya maamuzi. Hakuna mtu yoyote anayeweza kupinga maamuzi ya director, yeye ndiye mwenye mtazamo wa taswira wa sinema anayotaka kuitengeneza, na aina ya waigizaji na mavazi wanayotakiwa kuvaa.

Mwisho wa yote sinema ikitoka mbovu anaulizwa yeye sio muigizaji, kwa hiyo waongozaji kama sio madirector wanatakiwa kuwa makini sana.

Monday, February 11, 2013

Nurati ndani ya movie ya Julio na Romeo Tanzania


Kikundi cha Alwatan Artist Theater kimemtambulisha muigizaji mpya anayeitwa Nurati Ngereshi katika sinema yake ya Julio na Romeo inayotarajia kuingia sokoni hivi karibuni.

Kabla ya kuanza kuigiza, Nurati alikuwa akihakiki script za kundi hilo, lenye makao yake makuu Ilala Kimako. Sinema zote za kundi hilo utakutana na jina lake kwenye nafasi ya script editor.

Kwa vile stori ya Julio na Romeo lilikuwa ni wazo lake, alilomsimulia mwandishi wa script, baada ya kuandikwa alishauriwa kucheza

Katika sinema hiyo ameshiriki kama msichana anayempinga mdogo wake wa kiume anayeitwa Julio kumuoa msichana anayeitwa Romeo.

Wakati huo huo alikuwa akimshawishi rafiki yake Tunda aliyerejea nchini toka Marekani kuolewa na mdogo wake Julio. Ni sinema nzuri yenye mafunzo kwa jamii, inaweza kuangaliwa na watu wa rika zote.