Saturday, February 16, 2013

Madirector wanachangia muvi kukosa uhalisia



Mwigizaji wa sinema ya Julio na Romeo, Nurati Ngeleshi alisikika akiwashutumu waongozaji wa movie a.k.a madirector kwa kushindwa kuwalazimisha waigizaji kuvaa uhusika wa nafasi wanazocheza.

Hakuna kitu kinachonikera kama waigizaji wa kike kuvaa vimini sehemu hisiyostahili."  Akasema director mwenye umakini na kazi hawezi kukubali kitu kama hicho.

Inawezekana alichoongea Nurati kitawaboa wengi, ukweli utabaki pale pale kama madirector wanachangia kupoteza uhalisia wa sinema zetu kwa kuogopa kuwaeleza waigizaji ukweli wa kuvaa taswira ya nafasi aliyopewa.

Katika utayarishaji wa sinema director ni mtu wa mwisho katika kufanya maamuzi. Hakuna mtu yoyote anayeweza kupinga maamuzi ya director, yeye ndiye mwenye mtazamo wa taswira wa sinema anayotaka kuitengeneza, na aina ya waigizaji na mavazi wanayotakiwa kuvaa.

Mwisho wa yote sinema ikitoka mbovu anaulizwa yeye sio muigizaji, kwa hiyo waongozaji kama sio madirector wanatakiwa kuwa makini sana.

No comments:

Post a Comment