Saturday, February 16, 2013

Unafahamu vitabu vya kitanzania vilivyotengenezwa sinema


Mtunzi kitabu cha Ngoswe, Edwin Semzaba akiwa na rafiki yake mwenye miwani
 
Unaweza kushangaa kusikia hivyo, ila vipo vitabu  vilivyotengenezwa  sinema,  miongoni mwa vitabu hivyo ni  MAMBO YA  NGOSWE  kilichotungwa  na Edwin Semzaba , kimechapishwa  mwaka  1996  na Dar es Salaam University Press.

Kitabu  hicho  kilitayarishwa  kuwa sinema  na kampuni ya utayarishaji sinema  Tanzania, hata hivyo haikuweza kutoka kwa wakati huo mpaka  mwaka 2005. Ilipochukuliwa na kampuni ya Heko Production  na kuikarabati  kwa kuiongezea ubora na hatimaye kuisambaza madukani.

Kabla ya kitabu hicho kutayarishwa  sinema,  kiliwahi kutumika katika mchezo wa redio. Uliorushwa hewani na redio Tanzania  hivi sasa ni TBC Redio.

Kitabu kingine kilichotengenezwa  sinema  na  NGOME  YA   NG’WANAMALUNDI  kilichotungwa na Emmanuel Mbogo, kilitayarishwa sinema na kampuni ya Heko Production mwaka 2005.  Director  akiwa  marehemu Hammie Rajabu, Executive Producer  akiwa marehemu Ben R Mtobwa, Production Manager akiwa Haji Dilunga.

Kitabu cha   LAZIMA UFE JORAM  kilitengenezwa sinema, kitabu hicho kilitungwa na Marehemu Ben R Mtobwa,  kilichapishwa na  kampuni ya  Heko Publishers mwaka 1985,  kilitayarishwa  sinema  na  Heko Production mwaka 2006.

Director wa sinema hiyo alikuwa Bob Masha,  Script writer alikuwa Haji Dilunga, Executive Producer Marehemu Ben R Mtobwa, Production Manager  alikuwa  Ngabwe.

SIMU YA KIFO ni kitabu kingine kilichotengenezwa sinema, kitabu hicho kilitungwa na Faraji Katarambula. Marehemu Hammie Rajabu  aliandika Script  na ndiye aliyekuwa Director wa movie hiyo.

Kitabu kingine ni MZEE WA BUSARA kilichotungwa na Sultan Tamba,  script  aliandika mwenye sambamba na kuidirect  mwenyewe  akisaidiwa na Marehemu Salum Karanda.

No comments:

Post a Comment