Monday, February 11, 2013

Actress Mwajuma anatamba kwenye redio Dar es Salaam, Tanzania.

 
                      Mwajuma aka Maimuna akiwa juu ya kaburi  katika sinema ya uwanja wa dhambi
Mwajuma  Abdul a.k.a Maimuna  ni  muigizaji ambaye huwezi kumaliza siku nzima bila ya kusikia sauti yake kwenye tangazo lolote redioni.  Kwa wale wanaofahamu sauti yake watakuwa mashahidi  wa hiki kilichoandikwa hapa.

Baadhi ya matangazo yake ni pamoja na lile la bidhaa bora za Azam, Ulevi noma, Nimeshinda  na Airtel, Airtel money linalosema nimetumia elfu ya kumi ya kununua dawa, nimefika dukani nimekuta dawa inauzwa elfu kumi hiyo hiyo na mengine mengi.

Mbali ya kushiriki matangazo ameshiriki kuigiza katika sinema mbali mbali kama vile Lazima ufe Joram, Uwanja wa Dhambi, I love you, Picnic, Bunge la wachawi, Popobawa, Zindiko na Bayana  zinapatikana madukani. Sinema ya Confess na Julio na Romeo inatarajia kutoka hivi karibuni.

No comments:

Post a Comment