Hebu
jaribu kusikia kihoja cha mdau huyu wa muvi, anayeitwa Danny Alex
anayemiliki banda la video maeneo ya
Kipawa. Amesema miongoni mwa
waigizaji wanaomvutia ni Halima Madiwa.
Amedai
alianza kuvutiwa na umbo la Halima Baada ya kuona picha yake kwenye gazeti la
udaku.
Alex
amesema picha hiyo ilikuwa na maelezo yanayosema wanaume wanamsumbua kutokana
na makalio yake kuwa makubwa.
Kunzia
siku hiyo akaanza kufuatilia sinema alizocheza Halima kwa bahati nzuri
alibahatika kupata sinema ya Sound of Death. Katika movie hiyo hakuweza kumuona
vizuri kwa sababu alicheza kipande kidogo sana. Hata hivyo alicheza akiwa
amekaa.
Sinema
nyingine aliyocheza ilikuwa Secret file, pia alicheza kama msichana wa mapokezi
akiwa amekaa. Kwenye sinema ya Devil Kingdom amecheza kama sekretari,
alionekana akimpa barua Marehemu Kanumba.
Alifanikiwa kuona bodi yake
ila alichezeshwa kipande kidogo. Swali lake kwa watayarishaji, anataka kujua
vigezo gani vinavyotumika kumpatia nafasi kubwa ya kuigiza msanii. Kama ni umbo
na uzuri, mbona Halima analipa kuliko waigizaji wengine.
No comments:
Post a Comment