Saturday, February 16, 2013

Vyombo vya habari vyawasahau Producer, Director na Script writer



Wadau wa sinema wanashindwa kuelewa kama waandishi wa script ni  kiungo muhimu sana katika utayarishaji wa sinema. Bila ya script huwezi kupata sinema, bila ya script huwezi kujua uwezo wa mwigizaji au director.

Mwandishi wa script anakuwa tayari ametayarisha sinema kimaandishi, waigizaji na director wanaitoa kwenye maandishi na kuiweka kivitendo.

Kila kinachofanywa na waaigizaji katika sinema husika  kimetoka katika akili ya mwandishi wa script. Cha ajabu  waandishi na watangazaji  wanawasahau  waandishi wa script na kutoa nafasi kubwa kwa waigizaji. Kitendo hicho kinachangia kuifanya jamii kutofahamu umuhimu wa waandishi wa script.

Angalau madirector wanapata nafasi ya kutangazwa katika vyombo vya habari, waandishi script bado hawajapata nafasi hiyo,  lakini hata madirector wanapata nafasi finyu sana ukilinganisha na waigizaji.

Madirector wanaopata nafasi katika vyombo vya habari ni wale wanaodirect na kuigiza, kwa wale wanaodirect  bila ya kuigiza bado wananafasi finyu katika vyombo vya habari.

Ikiwa kwenye  muziki, mtayarishaji (Producer )  anapata nafasi kubwa katika vyombo vya habari, inashindikana  vipi kwa  madirector, maproducer, mascript writer  wa sinema kupata nafasi kubwa kama wanavyopata waigizaji au watayarishaji wa muziki.

Imefika  wakati wa vyombo vya habari kubadili na kuandika  taarifa za madirector, maproducer na waandishi wa script.

Tatizo kama hili lipo kwenye muziki wa taarabu,  anayetunga wimbo, muziki na wapigaji vyombo hawapewi  nafasi kubwa  kwenye vyombo vya habari kuliko  waimbaji.  Badilikeni wadau wa vyombo vya habari.

No comments:

Post a Comment