Kabla ya soko la sinema za kitanzania kupata umaarufu, sinema za kinaigeria zilikuwa na mvuto mkubwa sana nchini, hivi sasa zimepoteza umaarufu wake. Watanzania wengi wamezinduka na kuanza kupenda sinema zinazotayarishwa nchini na waigizaji wa kitanzania. Japokuwa sinema za kitanzania zinamapungufu mengi, bado watanzania wanazipenda.
Kinachotakiwa kufanywa na watayarishaji wa sinema ni kuwa makini wanapoanza kutayarisha. Ili kukwepa makosa ya kijinga ambayo hayahitaji elimu ya chuo kikuu kuweza kuyabaini.
Watayarishaji, waigizaji, waongozaji, waandishi wa script sambamba na wadau wa sinema wasipokuwa makini. Wanaweza kusababisha sinema za nje ya Tanzania kama vile wanaigeria, waghana na waafrika kusini kurudi katika chat ya juu.Kama ikitokea hivyo soko la sinema la kitanzania litapotea kama sio kusambarataika kabisa.
No comments:
Post a Comment