Monday, February 11, 2013

Nurati ndani ya movie ya Julio na Romeo Tanzania


Kikundi cha Alwatan Artist Theater kimemtambulisha muigizaji mpya anayeitwa Nurati Ngereshi katika sinema yake ya Julio na Romeo inayotarajia kuingia sokoni hivi karibuni.

Kabla ya kuanza kuigiza, Nurati alikuwa akihakiki script za kundi hilo, lenye makao yake makuu Ilala Kimako. Sinema zote za kundi hilo utakutana na jina lake kwenye nafasi ya script editor.

Kwa vile stori ya Julio na Romeo lilikuwa ni wazo lake, alilomsimulia mwandishi wa script, baada ya kuandikwa alishauriwa kucheza

Katika sinema hiyo ameshiriki kama msichana anayempinga mdogo wake wa kiume anayeitwa Julio kumuoa msichana anayeitwa Romeo.

Wakati huo huo alikuwa akimshawishi rafiki yake Tunda aliyerejea nchini toka Marekani kuolewa na mdogo wake Julio. Ni sinema nzuri yenye mafunzo kwa jamii, inaweza kuangaliwa na watu wa rika zote.

No comments:

Post a Comment