Stella Baltazar
Msanii anayenyemelea kuwa
mkongwe katika fani ya sinema, Stella Baltazar ni zao la kikundi cha Alwatan
Artist Theater.
Stella aliletwa kampuni ya
Heko Production na Marehemu Salum Karanda kwa la kucheza sinema inayoitwa
Mikono mwa nunda, wakati huo alikuwa hajawahi kushiriki kikundi chochote cha
sanaa.
Kwa vile Stella alikuwa na
vitu vitano ambayo A, B, C, D, E. kwa ufanunuzi ni kwamba A for appearance, B
for body structure, C for civilization, D for discipline na E for education,
alipatia nafasi ya kucheza kama Nunda, msichana anayeua watu na kujidai ni
Nunda mla watu.
Kwa bahati mbaya sinema hiyo
haikuweza kutayarishwa. Mzee Karanda alimchukua tena na kumfikisha kikundi cha
Alwatan, Uongozi wa kikundi ulimpokea na kumfundisha mbinu mbali mbali za
kuigiza
Sinema yake ya kwanza ilikuwa
Uwanja wa Dhambi aliyocheza kwa jina la Shubiri. Sinema ya pili ilikuwa I love
you aliyocheza kwa jina la Sophia.
Baada ya hapo aliamua
kujiunga na kikundi cha Shirikisho kilichokuwa kinarusha tamthilia yake
televisheni ya ITV.
Katika tamthilia hiyo
alikuwa akitumia jina la Kitalansi, baadaye alijikuta akipata nafasi ya
kushiriki sinema zilizotayarishwa na kampuni ya Game first Quality Tanzania.
Huko alicheza sinema nyingi kama vile Red Valentine na nyingine nyingi.
No comments:
Post a Comment