Showing posts with label Alwatan. Show all posts
Showing posts with label Alwatan. Show all posts

Saturday, February 16, 2013

Alwatan yawakumbuka waliotangulia mbele ya haki




Kikundi cha Alwatan Artist Theater chenye makao yake makuu Ilala Kimako, kimefanikiwa kutayarisha sinema nane, miongoni mwa sinema hizo ni pamoja na Uwanja wa dhambi, Popobawa, I love you, Picnic, Bunge la wachawi, Zindiko, Confess na Julio na Romeo inayotarajiwa kuingia mtaani hivi karibuni.

Kwa mujibu wa msemaji wa kikundi hicho, Belinda amesema kikundi kimeondokewa na wasanii wake tegemezi kama Anna Michael, Nyanda Nduta, Zainabu Mbavumbili aliyejitenga na kujiunga na kikundi kinachitwa Kitisa kabla ya kufikwa na umauti.

Mwingine aliyefariki ni mwandishi wa script, muigizaji na Director, Salum Karanda. Licha ya kufanya makubwa katika sanaa ya sinema, lakini vifo vya wasanii hao havikupata nafasi kubwa  katika vyombo vya habari.

Kwa mfano Salum Karanda aliyetayarisha sinema nyingi sana, pia alikuwa akiandika habari katika magazeti ya kila wiki kama mwandishi wa kujitegemea.

Miongoni mwa sinema alizoshiriki kama muongozaji msaidizi ni Mzee wa Busara, Siri, Shetani wa mahaba, Roho mbili, Jinamizi, Kisu, Bosi, Best friend, Uwanja wa dhambi, I love you na Picnic na nyingine. Alizoshiriki kama muongozaji mkuu ni Fadhila, Mama Mwenye Nyumba, Gauni la Marehemu, Hofu na nyingine nyingi

Monday, February 11, 2013

Stella ni zao la Alwatan Artist Theater Tanzania



Stella Baltazar


Msanii anayenyemelea kuwa mkongwe katika fani ya sinema, Stella Baltazar ni zao la kikundi cha Alwatan Artist Theater.

Stella aliletwa kampuni ya Heko Production na Marehemu Salum Karanda kwa la kucheza sinema inayoitwa Mikono mwa nunda, wakati huo alikuwa hajawahi kushiriki kikundi chochote cha sanaa.

Kwa vile Stella alikuwa na vitu vitano ambayo A, B, C, D, E. kwa ufanunuzi ni kwamba A for appearance, B for body structure, C for civilization, D for discipline na E for education, alipatia nafasi ya kucheza kama Nunda, msichana anayeua watu na kujidai ni Nunda mla watu.

Kwa bahati mbaya sinema hiyo haikuweza kutayarishwa. Mzee Karanda alimchukua tena na kumfikisha kikundi cha Alwatan, Uongozi wa kikundi ulimpokea na kumfundisha mbinu mbali mbali za kuigiza

Sinema yake ya kwanza ilikuwa Uwanja wa Dhambi aliyocheza kwa jina la Shubiri. Sinema ya pili ilikuwa I love you aliyocheza kwa jina la Sophia.

Baada ya hapo aliamua kujiunga na kikundi cha Shirikisho kilichokuwa kinarusha tamthilia yake televisheni ya ITV.
Katika tamthilia hiyo alikuwa akitumia jina la Kitalansi, baadaye alijikuta akipata nafasi ya kushiriki sinema zilizotayarishwa na kampuni ya Game first Quality Tanzania. Huko alicheza sinema nyingi kama vile Red Valentine na nyingine nyingi.