Saturday, February 16, 2013

Camera man, mwigizaji wanapokuwa madirector



                                                                   Camera man
Imekuwa kawaida katika nchi yetu ya Tanzania kumsikia  camera man au mwigizaji akibishana na Director.  Ugonjwa huu usipokemewa unaweza kuambukiza kizazi kijacho katika sanaa ya sinema.

Kitaalamu  production yote ipo chini ya director,  yeye  ndiye mwenye maamuzi ya mwisho. Anapoamua  jambo lolote hakuna mwenye ubavu wa kubisha, mliokuwa hapo mnaweza kumpa ushauri,  ni maamuzi yake kukubali au kukataa.

Mfano mzuri  director ni kocha wa timu ya mpira,  huwezi kuingilia maamuzi ya kochi katika kutayarisha kikosi chake.

Kwa upande wa utayarishaji wa sinema  madirector wanaingilia katika kufanya maamuzi yao,  matokeo yake wanajikuta wanatayarisha sinema  yenye makosa. 

Makosa yenye yanasababishwa na kutokuwa makini. Mwigizaji anambishia director, camera man anambishia director anajifanya anajua sana,  matokeo ya mabishana hayo ni Director kupoteza umakini na kufanya kazi mbovu.

Camera man  na waigizaji  tuwaache  madirector wafanye kazi zao,  kuwaingilia kuna sababisha kuendelea kushuhudia sinema zenye mapungufu na makosa ya kijinga, ambayo hayahitaji  elimu ya chuo kikuu kuweza kuyabaini.

Kama wewe mwigizaji fanye kile ulichokufikisha pale, mambo ya kuelekeza hayakuhusu. Nawe camera man fanye kazi yako ya kupiga picha, kuelekeza waigizaji namna ya kucheza sio kazi yako. Hiyo ni kazi ya Director na msaidizi wake.

Kila mmoja akizingatia jukumu lake, makosa ya kipumbavu katika sinema zetu yatapungua.  Ushauri kwenu wenye tabia hizo, kusema  ACTION   na CUT sio sababu ya kujiona unaweza kudirect movie.

Kuidirect movie ni zaidi ya ACTION  na CUT,  tuwape nafasi  madirector kufanya kazi zao kwa uhuru zaidi. Unajua kama kusimama nyuma ya camera sio sababu ya kuitwa camera man, au kubeba  jezi na mpira sio kigezo cha kuitwa mchezaji. Au kubeba gitaa sio sababu ya kuitwa mwanamuziki. Au kushinda kutwa chumba cha habari huwezi kuitwa mwandishi au mtangazaji. Unaweza kuwa mfagiaji.

No comments:

Post a Comment