Saturday, February 16, 2013

Bongo movie, Sound of Death inaoongoza kwa mastaa wengi Tanzania


                                                         Tumaini Bigirimana
                         Jacob Steven
                         Patcho Mwamba
                                                            Hemed Suleiman
                                                        Auntie Ezekiel
                      Yusufu Mlela
Sinema iliyotungwa na kuandikwa script na Haji Dilunga kisha kuongozwa na Mtitu G Game, inaongoza kwa kuwa na idadi kubwa ya waigizaji maarufu hapa nchini.

Swahili Cinema News ilishuhudia mabishano makali ya wapenzi na mashabiki ya sinema za kibongo katika kibanda cha video.

Mabishano hayo yalidai Sound of Death ni sinema pekee iliyokusanya waigizaji wengi wenye majina makubwa hapa bongo.

Miongoni mwa majina ya waigizaji walioshiriki katika movie hiyo ya aina yake ni pamoja na Auntie Ezekiel, Jacob Steven, Rose Ndauka, Hemedi Suleiman, Flora Mvungi, Yusuf Mlela, Tumaini Bigirimana, Patcho Mwamba, Mayasa Mrisho.

Wengine ni Hidaya Njaidi, Tito, Masinde, Grace Mapunda, Mariam Georger, Abdul Ahmed a.k.a Ben, Bakari Makuka, Maua na wengine

Mpaka mwanahabari anaondoka hapo hakuna mshindi wa mabishano hayo, ila utafiti wetu umefanikiwa kugundua kwamba Sound of Death inaweza kuwa miongoni mwa sinema iliyokusanya idadi kubwa ya waigizaji wenye majina makubwa kwa mwaka 2012.

No comments:

Post a Comment