Wapenzi
na mashabiki waliobahatika kuongea na mtandao wa Swahili Cinema News, wamesema
sinema za kitanzania kuwa na majina ya kizungu, ni ushamba na ulimbukeni wa
hali ya juu.
“
Binafsi yangu sijawahi kuona sinema ya kihindi yenye jina la kizungu, au sinema
ya kichina, Kijapan na kiarabu zenye
majina ya kizungu. Kama zipo itakuwa na jina la kizungu na jina la lugha
yao" alisema Joshua Daniel.
Bi
Sauda Ramadhani amesema sinema zilizotoka mwanzo zilikuwa nzuri, zilizingatia
maadili ya kitanzania kuanzia stori, uvaaji, uchezaji na jina la sinema kuwa
katika lugha ya kiswahili.
Alizitaja
sinema hizo ni Nsyuka, Fungu la kukosa, Ngome ya Mwanamalundi, Lazima ufe
Joram, Mambo ya ngoswe na nyingine nyingi za wakati huo.
“
Baada ya kuingia watayarishaji wanaopenda kuona mapaja ya watoto wetu wa kike,
wakabadili mfumo wa utengenezaji sinema kwa kuandika majina ya
kizungu.Kuwavisha nguo za ajabu mabinti wetu na kuwalazimisha kupigana mabusu,
yaani huwezi kuangalia na watoto zako." Alisisitiza Bi Sauda.
Jaffar
amesema kabla ya kina Ray, Tino, Johari, Mainda, Teya, Tito, Swebe, Maya, Zawadi,
Nora, Nina na wengine, hawajaanza kuigiza sinema.
Walikuwa
wakizingatia maadili katika michezo yao ya kwenye televisheni. Baada ya kuanza
kujiunga na makampuni ya kutayarisha sinema, walibadilika kimaadili na kuanza
kuvaa taswira ya kishetani. Taswira iliyowachukiza watazamaji wao.
“
Binafsi nilichukizwa na muonekano wao mpya, kwanza walikuwa wanaiga maadili ya
kinaigeria kuanzia stori mpaka uchezaji." Alidai Jaffar.
No comments:
Post a Comment