Ini Edu
LAGOS, Nigeria
Nyota wa sinema za Nigeria anayeongoza kwa utajiri, Ini Edo amesema skendo pekee iliyowahi kumchukiza katika maisha yake ni ile iliyoandikwa na baadhi ya vyombo vya habari, ikimuhusisha na uvutaji wa dawa za kulevya.
Amesema vyombo vya habari vilimkosea kwa kuandika habari ya uzushi, habari ambayo ilinivunjia heshima yangu kwenye familia, marafiki, mashabiki na wapenzi wangu wa ndani ya Nigeria na nje.
" Skendo ile ilinipa wakati mgumu sana, ila nashukuru wapenzi na mashabiki zangu, waligundua ukweli kama sio mtumiaji wa madawa ya kulevya. Skendo ile iliandaliwa na wabaya wangu kwa lengo la kunishusha kiugizaji."
Alipoulizwa kama anavuta sigara, mwanadada mwenye mvuto wa kimapenzi, alisema amekuwa akifanya hivyo katika baadhi ya filamu alizocheza, lakini kwa kawaida si mvutaji wa sigara na hataraji kuvuta katika maisha yake.
Ini alidai mtazamo wake ni tofauti na wasichana wengine wanaodai kuzaa kunaharibu shepu ya mwanamke, amesema sio kweli. Kwa sababu mwanamke aliyeolewa, kuzaa ni jambo la lazima na kwamba anapenda kuwa na watoto
“Sihofuu kupoteza umbile langu kwa sababu ya kuzaa. Wakati utakapofika, nitaanza kuzaa. Napenda watoto. Siwezi kusubiri muda mrefu kupata watoto,”alisema mwanadada huyo mwenye umbo na sura yenye mvuto alipohojiwa hivi karibuni.
Hata hivyo, Ini amesema kama ni uzuri, alikuwa nao alipokuwa na umri mdogo. Alisema aliziona baadhi ya picha zake alipokuwa mdogo na kuvutiwa nazo kiasi cha kumfanya kutoa amani kama ni yeye.
Ini alisema hana njia yoyote anayoifanya ili aonekane mrembo zaidi ya kufanyakazi zake kwa bidii, kula vizuri, kuiweka ngozi yake katika hali nzuri na kuwa mwenye furaha muda wote.
Mwanadada huyo alisema anamshukuru Mungu kwamba maisha yake ya ndoa yanakwenda vizuri na kuongeza kuwa, kwa sasa ameamua kuacha kuigiza nafasi, ambazo zinaweza kuitia doa ndoa yake.
Alisema kamwe hajawahi kuigiza filamu za ngono na hawezi kufanya kitu kama hicho katika maisha yake yote. Alisema anapenda zaidi kuigiza filamu zinazoelezea maisha halisi ya jamii kwa vile ndizo zinazokuwa na mvuto zaidi kwa jamii.
Mwanadada huyo mwenye macho ya mwito alikataa kutaja kiasi cha pesa, ambacho amekuwa akilipwa katika uigizaji wa filamu. Hata hivyo, alikiri kwamba amekuwa akilipwa fedha nyingi.
Ini alikiri kuwa si rahisi kumudu kuwa mke wa mtu na mwigizaji. Alisema anajitahidi kadri ya uwezo wake kumudu mambo hayo mawili na kwa kiasi fulani amefanikiwa.
“Nimekuwa nikipanga mapema ni lini niwe mahali fulani na lini nisiwe mahali hapo. Siweki vitu vingi kwenye sahani moja kwa wakati mmoja kwa sababu nikifanya hivyo, nitashindwa kufanya vitu vingine wakati ninapaswa kuvifanya. Bado nafanya kila kitu ambacho mwanamke anapaswa kukifanya. Kila ninapotoka kazini, nafanyakazi ya kupika nyumbani,”alisema.
Ini, ambaye ni msomi wa shahada ya sanaa alisema iwapo asingekuwa mwigizaji, angependa kuwa mwanasheria au mwanahabari.
Hata hivyo, Ini alisema upo uwezekano pia angeweza kufanyakazi nyingine yoyote ilimradi tu awe anaipenda.
“Mimi ni mtu makini katika kila jambo. Kila kitu ninachokiseti kukifanya katika akili yangu, kama ninakipenda, lazima nikifanye,”alisema.
Hivi karibuni, Ini alizindua filamu yake mpya ya I Will Take My Chances, ambayo Ini ameielezea kuwa, ana hakika itafanya vizuri sokoni na kupendwa na mashabiki.
Ini alisema ilimchukua miezi miwili kutengeneza filamu hiyo, mwezi mmoja kwa ajili ya mazoezi na mwezi mwingine kwa ajili ya kupiga picha za filamu hiyo.
Mwanadada huyo alisema licha ya kuolewa, hafikirii kustaafu kucheza filamu kwa sasa na kwamba hakuna kinachoweza kumfanya afikie uamuzi huo.
Alisema kwake, uigizaji wa filamu hautokani na kutafuta pesa, bali mapenzi kwa kazi hiyo.
Mumewe Ini kwa sasa anaishi nchini Marekani. Lakini mwanadada huyo amesisitiza kuwa, hilo si tatizo kwao kwa sababu wamekuwa wakikutana mara kwa mara.
Katika kujiweka safi kimwili, Ini amesema siku zote amekuwa akipenda kusafisha uso wake na kuuweka safi. Alisema anapokuwa hana kazi ama tukio lolote, hatumii vipodozi kutengeneza uso wake.
Showing posts with label habari. Show all posts
Showing posts with label habari. Show all posts
Saturday, July 13, 2013
Saturday, February 16, 2013
Vyombo vya habari vyawasahau Producer, Director na Script writer
Wadau wa sinema wanashindwa kuelewa kama waandishi wa script
ni kiungo muhimu sana katika utayarishaji wa sinema. Bila ya
script huwezi kupata sinema, bila ya script huwezi kujua uwezo wa mwigizaji au
director.
Mwandishi wa script anakuwa tayari ametayarisha sinema
kimaandishi, waigizaji na director wanaitoa kwenye maandishi na kuiweka kivitendo.
Kila kinachofanywa na waaigizaji katika sinema husika kimetoka katika akili ya mwandishi wa script.
Cha ajabu waandishi na watangazaji wanawasahau
waandishi wa script na kutoa nafasi kubwa kwa waigizaji. Kitendo hicho
kinachangia kuifanya jamii kutofahamu umuhimu wa waandishi wa script.
Angalau madirector wanapata nafasi ya kutangazwa katika
vyombo vya habari, waandishi script bado hawajapata nafasi hiyo, lakini hata madirector wanapata nafasi finyu sana ukilinganisha na
waigizaji.
Madirector wanaopata nafasi katika vyombo vya habari ni wale
wanaodirect na kuigiza, kwa wale wanaodirect
bila ya kuigiza bado wananafasi finyu katika vyombo vya habari.
Ikiwa kwenye muziki,
mtayarishaji (Producer ) anapata nafasi
kubwa katika vyombo vya habari, inashindikana
vipi kwa madirector, maproducer,
mascript writer wa sinema kupata nafasi
kubwa kama wanavyopata waigizaji au watayarishaji wa muziki.
Imefika wakati wa
vyombo vya habari kubadili na kuandika
taarifa za madirector, maproducer na waandishi wa script.
Tatizo kama hili lipo kwenye muziki wa taarabu, anayetunga wimbo, muziki na wapigaji vyombo
hawapewi nafasi kubwa kwenye vyombo vya habari kuliko waimbaji.
Badilikeni wadau wa vyombo vya habari.
Subscribe to:
Posts (Atom)
