Uru Eke
Lagos, Nigeria
Mwigizaji wa sinema za Nigeria Uru Eke amesema anauwezo mkubwa wa kuigiza sinema za mapenzi, kwa sababu ana hisia kali za mapenzi. Hata hivyo amedai kwamba ameumbwa hivyo kuwa mkali wa kuigiza sinema za mapenzi.
"Nina uwezo mkubwa wa kuigiza aina hizo za filamu za mapenzi kwa sababu nimezaliwa nikiwa ni mtu mwenye hisia kali katika mapenzi," alisema mwigizaji huyo anayekuja juu kwa sasa na kutamba kwamba mwigizaji, Ramsey ni miongoni mwa waigizaji wa kiume wenye hisia kali katika mapenzi. Angependa kucheza naye kama angeambia kuchagua mwanaume wa kucheza naye sinema za mapenzi.
Licha ya kusema hivyo amesisitiza kwamba hisia zao za mapenzi zitakuwa katika kuigiza baada ya kuigiza hakuna kitakachoendelea.
" Najua kama Ramsey Noah ni mume wa mtu, kwa hivyo hakuna kitakachoendelea zaidi ya kuigiza na kila mtu kuendelea na shughuli zake," alisema Uru Eke aliyezaliwa London na kupata elimu ya msingi London. Elimu yake ya sekondary alipata Nigeria, baada ya kumaliza elimu ya sekondari alikwenda Uingereza kupata elimu ya chuo katika chuo cha City University.
Showing posts with label Muvi. Show all posts
Showing posts with label Muvi. Show all posts
Thursday, July 18, 2013
Sunday, July 14, 2013
Snura Mushi kuibuka ndani muvi mpya
Snura Mushi
Mwigizaji wa kike na mwimbaji wa muziki wenye midundo ya kipwani yaani mduara, Snura Mushi aliyetamba sana katika tamthilia ya Jumba la dhahabu na sinema mbali mbali, amefunguka na kudai kwamba muziki umempa dili la kwenda kurekodi filamu Afrika ya kusini.
Amesema watayarishaji wa sinama ya Tandeka iliyorekodiwa jijini Pretoria, walimshirikisha kutokana na kufanya vizuri kwa wimbo wake wa Majanga. katika sinema hiyo ametumia lugfha ya kiswahili, kizulu na kiingereza.
Mwigizaji wa kike na mwimbaji wa muziki wenye midundo ya kipwani yaani mduara, Snura Mushi aliyetamba sana katika tamthilia ya Jumba la dhahabu na sinema mbali mbali, amefunguka na kudai kwamba muziki umempa dili la kwenda kurekodi filamu Afrika ya kusini.
Amesema watayarishaji wa sinama ya Tandeka iliyorekodiwa jijini Pretoria, walimshirikisha kutokana na kufanya vizuri kwa wimbo wake wa Majanga. katika sinema hiyo ametumia lugfha ya kiswahili, kizulu na kiingereza.
Saturday, February 16, 2013
Madirector wanachangia muvi kukosa uhalisia
Mwigizaji
wa sinema ya Julio na Romeo, Nurati Ngeleshi alisikika akiwashutumu waongozaji
wa movie a.k.a madirector kwa kushindwa kuwalazimisha waigizaji kuvaa uhusika
wa nafasi wanazocheza.
“Hakuna kitu kinachonikera
kama waigizaji wa kike kuvaa vimini sehemu hisiyostahili." Akasema director mwenye umakini na kazi
hawezi kukubali kitu kama hicho.
Inawezekana
alichoongea Nurati kitawaboa wengi, ukweli utabaki pale pale kama madirector wanachangia
kupoteza uhalisia wa sinema zetu kwa kuogopa kuwaeleza waigizaji ukweli wa
kuvaa taswira ya nafasi aliyopewa.
Katika
utayarishaji wa sinema director ni mtu wa mwisho katika kufanya maamuzi. Hakuna
mtu yoyote anayeweza kupinga maamuzi ya director, yeye ndiye mwenye mtazamo wa
taswira wa sinema anayotaka kuitengeneza, na aina ya waigizaji na mavazi
wanayotakiwa kuvaa.
Mwisho wa yote sinema
ikitoka mbovu anaulizwa yeye sio muigizaji, kwa hiyo waongozaji kama sio
madirector wanatakiwa kuwa makini sana.
Subscribe to:
Posts (Atom)

