Showing posts with label Muvi. Show all posts
Showing posts with label Muvi. Show all posts

Thursday, July 18, 2013

Uru atamba amezaliwa kwa ajili muvi za mapenzi

                                                                           Uru Eke
Lagos, Nigeria
Mwigizaji wa sinema za Nigeria Uru Eke amesema anauwezo mkubwa wa kuigiza sinema za mapenzi, kwa sababu ana hisia kali za mapenzi. Hata hivyo amedai kwamba ameumbwa hivyo kuwa mkali wa kuigiza sinema za mapenzi.
"Nina uwezo mkubwa wa kuigiza aina hizo za filamu za mapenzi kwa sababu nimezaliwa nikiwa ni mtu mwenye hisia kali katika mapenzi," alisema mwigizaji huyo anayekuja juu kwa sasa na kutamba kwamba mwigizaji, Ramsey ni miongoni mwa waigizaji wa kiume wenye hisia kali katika mapenzi. Angependa kucheza naye kama angeambia kuchagua mwanaume wa kucheza naye sinema za mapenzi.
Licha ya kusema hivyo amesisitiza kwamba hisia zao za mapenzi zitakuwa katika kuigiza baada ya kuigiza hakuna kitakachoendelea.
" Najua kama Ramsey Noah ni mume wa mtu, kwa hivyo hakuna kitakachoendelea zaidi ya kuigiza na kila mtu kuendelea na shughuli zake," alisema Uru Eke aliyezaliwa London na kupata elimu ya msingi London. Elimu yake ya sekondary alipata Nigeria, baada ya kumaliza elimu ya sekondari alikwenda Uingereza kupata elimu ya chuo katika chuo cha City University.

Sunday, July 14, 2013

Snura Mushi kuibuka ndani muvi mpya

                                                                        Snura Mushi
Mwigizaji wa kike na mwimbaji wa muziki wenye midundo ya kipwani yaani mduara, Snura Mushi aliyetamba sana katika tamthilia ya Jumba la dhahabu na sinema mbali mbali, amefunguka na kudai kwamba muziki umempa dili la kwenda kurekodi filamu Afrika ya kusini.
Amesema watayarishaji wa sinama ya Tandeka iliyorekodiwa jijini Pretoria, walimshirikisha kutokana na kufanya vizuri kwa wimbo wake wa Majanga. katika sinema hiyo ametumia lugfha ya kiswahili, kizulu na kiingereza.

Saturday, February 16, 2013

Madirector wanachangia muvi kukosa uhalisia



Mwigizaji wa sinema ya Julio na Romeo, Nurati Ngeleshi alisikika akiwashutumu waongozaji wa movie a.k.a madirector kwa kushindwa kuwalazimisha waigizaji kuvaa uhusika wa nafasi wanazocheza.

Hakuna kitu kinachonikera kama waigizaji wa kike kuvaa vimini sehemu hisiyostahili."  Akasema director mwenye umakini na kazi hawezi kukubali kitu kama hicho.

Inawezekana alichoongea Nurati kitawaboa wengi, ukweli utabaki pale pale kama madirector wanachangia kupoteza uhalisia wa sinema zetu kwa kuogopa kuwaeleza waigizaji ukweli wa kuvaa taswira ya nafasi aliyopewa.

Katika utayarishaji wa sinema director ni mtu wa mwisho katika kufanya maamuzi. Hakuna mtu yoyote anayeweza kupinga maamuzi ya director, yeye ndiye mwenye mtazamo wa taswira wa sinema anayotaka kuitengeneza, na aina ya waigizaji na mavazi wanayotakiwa kuvaa.

Mwisho wa yote sinema ikitoka mbovu anaulizwa yeye sio muigizaji, kwa hiyo waongozaji kama sio madirector wanatakiwa kuwa makini sana.