Sunday, July 14, 2013

Beckham kuigiza nafasi ya James Bond

                                                                   
                                                                      David  Beckham

London, England  
Mke wa aliyekuwa mwanasoka wa Klabu ya Manchester United, Victoria Beckham amependekeza jina la mumewe, David Beckham kuwa miongoni mwa majina yatakayochaguliwa kupata nafasi ya kuigiza kama James Bond katika mfululizo wa sinema za 007, zinazomtumia muhusika mkuu anayeitwa James Bond.
Mapendezo hayo yanafanyika baada ya mwigizaji, Daniel Craig anayecheza sasa kama James Bond kubwaga manyanga. Majina yaliyopendekezwa ni kucheza kama James Bond ni pamoja na Christian Bale, Henry Cavill, Tom Hardy na Idris Elba.
Victoria ana amini Beckham anaweza kuitendea haki nafasi hiyo kuliko wote waliotaja kuziba pengo la Daniel Craig anayeacha kucheza nafasi hiyo.
" Nina uhakika Beckham ni bidhaa inayouzika, kama watamtumia kucheza kama James Bond. Sinema hayo itapendwa na watu wengi sana hata wale ambao sio mashabiki wa kuangalia sinema, kwa sababu Beckham ni mtu wa watu," alisisitiza Victoria alipokuwa anaongea.
Kama watampa nafasi ya kucheza kama James Bond, Beckham atafanya vizuri, kwanza ni mwanaume mwenye mvuto. Sura yake nzuri na shepu ya umbo lake ni nzuri tofauti na wanaume. Kwa hiyo watu watapenda kumtazama.
Hata hivyo Beckham mwenyewe alipoulizwa, alisema hana uhakika kama ataweza kufanya vizuri, kwa sababu hajawahi kuigiza au kusimama mbele ya camera kuigiza.
"Sina uhakika kama nitakuwa mzuri katika kuigiza, kwa sababu sijawahi kufanya kitu kama hicho katika maisha yangu. Ila kama nitapewa nafasi naweza kufanya. Nina rafiki yangu Tom Cruise ambaye ni mwigizaji mkubwa, labda ninaweza kuwa kama yeye. Ila sijafikiria kitu kama hicho kwa sasa," alisema Beckham, wengi wanamkumbuka kwa uhodari wake uwanjani.

No comments:

Post a Comment