Sunday, July 14, 2013
Stephanie Okereke amepata tuzo
Stephanie Okereke
Lagas, Nigeria
Diva wa sinema za Nigeria, Stephanie Okereke amepata tuzo maalumu baada ya kuigiza filamu inayofahamika kama Dry. Sinema hiyo inazungumzia masuala yanayohusiana na ugonjwa wa FISTULA.
Kwa mujibu wa waliotoa tuzo hiyo, wamesema sinema hiyo ni miongoni mwa sinema bora zaidi hasa ukizingatia namna ilivyochezwa na kuelezea tatizo la ugonjwa wa FISTULA.
" Ni sinema nzuri inayoelezea namna ya kinamama wanavyokumbana na tatizo la kutokwa na haja ndogo kiholela."
Tatizo limekuwa likiwaweka njia panda wanawake wengi kwa sababu hana elimu ya kupata ufumbuzi wa tatizo na hawajui kinga ya tatizo hilo. Sinema hiyo imetoa mwanga kwa kueleza namna ya kukabiliana na FISTULA.Juhudi binafsi zilizoonyeshwa na mwigizaji huyo zimemsaidia kupata tuzo hiyo.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment