Saturday, July 13, 2013

Lindsay mrembo mwenye matumizi mabaya fedha


                                                                   Lindsay  Lohan
                                                                      Lindsay Lohan
New York, Marekani
Mwigizaji, Lindsay Lohan ni miongoni mwa warembo waliokuwa katika chati ya juu kwa kuvuta hisia  za wengi kutokana na muonekana wake sambamba na vituko vyake, anavyofanya kila kukicha.
Mwanadada huyo anayependa kutumia fedha vibaya kama vile ameokoa, wakati ni fedha zake alizopata kwa kufanya kazi usiku na mchana. Jarida la Forbes la mwaka jana, limeandika kwamba Lindsay ameshika namba thalethini katika orodha ya waigizaji wanaotafuta fedha ili waweze kuishi maisha mazuri.
Lindsay mwenye umri wa miaka 27  raia wa Marekani ana utajiri wa dola 11 milioni.Utajiri huo umetokana na uigizaji, uimbaji wa muziki, uanamitindo na utangazaji wa manukato.
Kutokana na matumizi yake kuwa mabaya, mwaka 2011 alijikuta akifikia hatua ya kufilisika, mahesabu ya haraka aliyofikia ili aweze kupata fedha, ni kupiga picha za utupu na kupata dola milioni moja. Baada ya kupiga picha hizo alipata fedha na kurudi tena kwenye chati ya wenye fedha.
Kwa kutaka kuonyesha jeuri ya fedha alipangisha nyumba kwa dola 10,000 kwa mwezi. Anatumia dola 800 kila wiki kwa ajili  ya kutengeneza nywele zake, alinunua gari aina porsche kwa dola 80,000.
Amekamatwa mara nyingi kuhusiana na utumiaji wa madawa ya kulevya na kuendesha gari akiwa amelewa, mwaka 2007 aliwahi kufungwa jela kwa muda wa siku tisini baada ya kupatikana na hatia ya kufanya fujo.Kutokana mwendo wa tabia zake kuwa tofauti na jamii iliyostarabika, Lindsay anapata ushauri wa kuacha kutumia dawa za kulevya.

No comments:

Post a Comment