Saturday, July 13, 2013

Navuta majani- Tonto Dikeh

                                                                   Tonto Dikeh
Lagos Nigeria
Nyota wa sinema za Nollywood, Tonto Dikeh ameendelea na tabia yake ya kufanya vituko, ila kituko cha safari hii kimetokea kuwashangaza wengi waliopita mtandao na kuona amebandika picha ya bangi iliyokuwa na maneno ya kusifia kilevi hicho.
" Mimi navuta ganja, mimi navuta majani napata stimu wakati wengine wanavuta majungu," aliandika ujumbe kwenye picha hiyo bila ya kuwa na wasi wasi licha ya kilevi hicho kupigwa maarufu na serikali za nchi mbali mbali duniani.
Licha kutundika picha inayonyesha bangi na kuandika ujumbe wa kusifia, ametundika picha yake inayomuonyesha akiwa tayari amepata stimu, yaani amevuta bangi. Sura yake inaonyesha jinsi alivyokolea na kilevi hicho.

No comments:

Post a Comment