Saturday, July 13, 2013

Najivunia uwezo wangu wa kukata viuno- Shilole


                                                                       
                                                             Shilole katika pozi la nguvu
                                                                             Shilole

Mwanadada mrembo na mwigizaji maarufu katika tasni ya sinema za kibongo, Zuwena Mohamed a.k.a Shilole ambaye hivi sasa amejikita katika muziki, na kufanikia kutamba na kutishia waimbaji wa kike wenye uwezo, nyimbo zake zimetokea kupendwa na kufanya vizuri.
Wengi hawakutegemea kama angweza kufanya vizuri katika soko la muziki, kwani kuna baadhi ya waigizaji waliojaribu kuimba kama vile Zerishi, mwigizaji aliyetamba katika sinema ya Ngome ya Mwanamalundi.
Kwa Shilole hali imekuwa tofauti, ameweza kujipata umaarufu mkubwa na kupata maonyesho mengi.
"Ninapata maonyesho mengi kwa sababu ninapokuwa jukwaani, najituma kadri ya uwezo wangu kucheka, yaani kukata viuno. Najivunia uwezo wangu wa kukata viuno." alitamba Shilole msichana mwenye umbo la kuvutia na kuhamasisha kwa kila nguo anayovaa kwa inampendeza.
Nyimbo yake ya Paka la Baa iliyokuwa katika mtindo wa mduara, imejipata umaarufu kutokana na mashairi yake kugusa maisha ya halisi ya baadhi ya watu wenye tabia ya zisizokubali na jamii.
Kama kawaida yake anawashukuru wapenzi na mashabiki wake kwa kumkubali,pia amewataka waendelee kumpa sapoti kwa kuzikubali kazi nyingine anazotarajia kutoa hivi karibuni.
Shilole ameweza kufanikiwa kuwasisimua mashabiki wake, wanawake na wanaume kwa uwezo wake wa kuzungusha kiuno.
Zamani kabla ya Shilole  alikuwa akisifiwa Ray C kwa kuzungusha kiuno mpaka akapachikwa jina la kiuno si mfupa.




No comments:

Post a Comment