Thursday, July 18, 2013

Mama Kanumba kama mwanae kwenye filamu ya Without Daddy.

 
Ben Blanco,  Jamila na mwenzake katika Without Daddy
                                             Frola Mtegeo Mama yake Marehemu Kanumba
Mama wa aliyekuwa mwigizaji maarufu marehemu Steven Kanumba  maarufu kama Big Daddy,  Frola Mtegoa ameigiza filamu katika muendelezo wa kipaji cha mwanaye baada ya kuigiza katika filamu ya Without Daddy akishirikiana na watoto waliokuwa wakiigiza na marehemu Kanumba kama Patrick na Jamila, katika filamu hiyo mama Kanumba kaigiza katika kiwango cha juu.
Kwa mujibu ya maelezo ya  mkurugenzi wa kampuni ya Big Daddy Production, Irene Kaungwa amesema filamu ya Without Daddy ni kazi mwendelezo wa kazi ya marehemu Kanumba iliyotoka siku za nyuma ya Big Daddy na ni kazi ambayo imetengezwa kwa ubora wa kimataifa ikiwa sambamba na kumtambulisha mama Kanumba katika tasnia ya filamu Tanzania.
“Kampuni ya Big Daddy Production imekusudia kuleta mapinduzi makubwa katika tasnia ya filamu Tanzania, na katika kumuenzi marehemu tumemchukua mama yake na  kumshiriki katika filamu hii, nadhani umeona uwezo wa mama Kanumba. Naweza kusema ameonyesha uwezo mkubwa katika uigizaji na hii ni filamu yake ya kwanza,”anasema mkurugenzi.
Irene Kaungwa amesema stori ya sinema hiyo ametunga yeye, script imeandikwa na Haji Dilunga. Waigizaji waliocheza sinema hiyo ni pamoja Abdalah Mkumbilah ‘Muhogo mchungu’, Fatuma Makongoro ‘Bi. Mwenda’ Cathy Rupia, Mayasa Mrisho, ‘Maya’, Othuman Njaidi ‘Patrick’ Wastara Juma ‘Stara’ Abdul Ahmed ‘Ben Blanco’,  Patcho Mwamba na wasanii mahiri wengineo.


                         

No comments:

Post a Comment