Sunday, July 14, 2013

Sipendi rafiki mnafiki- Yvonne Nelson

                                                                      Yvonne Nelson
 Lagos, Nigeria
Mwigizaji maarufu wa Nigeria, Yvonne Nelson amesema anachukizwa na marafiki wa wanafiki, amesema hapendi marafiki kama hao wanaochukua taarifa zake za siri na kuziandika kwenye blog.
Yvonne ambaye hivi karibuni alifanyiwa kitu mbaya na rafiki yake wa karibu, kitendo kilichomchukiza na kufikia kudai kwamba rafiki wa aina hiyo ni sawa na mchawi.
"Kama rafiki yangu ni lazima atafahamu mambo yangu ya siri, kufahamu siri zangu isiwe sababu ya kuandika katika blog. Binafsi nakerwa na marafiki wa aina hiyo, nitakuwa makini nao," alisema.

No comments:

Post a Comment