Saturday, July 13, 2013

Nikifa sitaki nikumbukwe kama mwigizaji- Eucharia




                                                             Eucharia Anunobi Ekwu
Lagos, Nigeria
Mwanamama nyota wa sinema za Nollywood Eucharia Anunobi Ekwu  ameachana na uchezaji wa sinema na kuamua kuokoka, kumtumikia mungu kwa muda wa maisha yake yaliyobaki hapa duniani.
Hivi karibuni  Euchari alitangaza kuachana na uigizaji na kuamua kumrudia mungu kwa kuokoka baada ya kutamba kwa sana katika sinema nyingi alizoshiriki kuigiza.
Katika mahojiano yake na kituo kimoja cha televisheni cha hapa Nigeria, Eucharia amesema  akifariki dunia akumbukwe kama aliwahi kuwa mwigizaji wa sinema.
"Ingawa nimecheza muvi nyingi kwa muda mrefu, lakini nasema wazi kwamba, nikifa nsikumbukwe kama msanii bali ni mtu wa mungu ambaye nimeamua kumtumikiakwa kipindi cha maisha yangu yote yaliyobaki duninai,"alisema mwanadada huyo mwenye mvuta wa kimapenzi na macho ya kuita.
Euchari atakumbukwa na wapenzi na mashabiki katika sinema ya Abuja Connection, sinema hiyo ameshirikiana kuigiza na wakali wengine kama Clarion Chukwura Abiola, Ngozi Ezeonu, Chidi Mokeme Enabeli Elabuwa na wengine wengi wenye majina makubwa Nigeria.
Sinema ilitungwa na Ojiofor Ezeanyaeche, script iliandikwa na Adim Williams sambamba na kuongozwa na Adim Williams mwenyewe.

No comments:

Post a Comment