Tuesday, February 19, 2013

Sinema kimataifa, Kambi kuigiza Ghana na Van Vicker


Hashim Kambi
                                      Van Vicker

Muigizaji wa filamu nchini Hashimu Kambi amefungua mwaka huu kwa neema ambapo hivi sasa muigizaji huyo anatarajia kusafiri kuelekea nchini Ghana na Nigeria kwa ajili ya kufanya kazi akiwa ni muigizaji mkuu msaidizi.

Kwa mujibu Televisheni ya EATV, Hashimu amesema kuwa amepata mwaliko huo baada ya kazi zake kumfikia msanii ambaye ni muongozaji wa filamu mahiri katika nchi ya Nigeria anayejulikana kwa jina la Van Vicker.

Aidha akiwa nchini Nigeria na Ghana Hashimu anatarajia kushiriki katika filamu inayoitwa Day after Death itakayofanyika kwa muda wa siku saba jijini Accra na siku saba kwenye jiji la Lagos, ambapo inamuweka katika nafasi nzuri ya ushiriki wake filamu za kimataifa baada ya marehemu Steven Kanumba aliyeweza kuipeperusha vyema bendera ya taifa kimataifa.

Sinema Tanzania, Mchungaji bado anamwandama Kanumba

                                              Steven Kanumba         
Kitendo cha baadhi ya wananchi kutumia jina la msanii aliyefariki kujipatia kipato au umaarufu ni kitu kibaya, kinachotakiwa kupigwa marufuku na kuwakamata wahusika na kufikisha mbele ya vyombo vya sheria.

Swahili Cinema News imeshuhudia mtu anayejiita Mchungaji George Kairuki akitumia jina la Marehemu Steven Kanumba kujipatia umaarufu katika kiwanja kilichokuwa Buguruni chama karibu na shule ya msingi, pamoja na kituo cha basi.

Mchungaji huyo aliibuka mara baada ya kifo cha Marehemu Kanumba na kueleza kama marehemu alikuwa muumini wa Freemasons, madai ambayo hakuna aliyekuwa na uhakika nayo.

Hata hivyo, kwa akili za kawaida madai hayo kwa sasa hayana umuhimu wowote, hakuna aliyetaka kufahamu kama alikuwa muumuni wa Freemasons. Kwa sababu haisaidi chochote hata watu wakifahamu.

Kikubwa anachofanya mchungaji huyo ni kujitafutia umaarufu kupitia mgongo wa marehemu Kanumba, taarifa ambazo kwa upande mwingine zilionyesha kumjenga kwa kumpatia umaarufu ili watu wajiunge na kanisa lake.
Kama lengo ni kutoa taarifa za Kanumba kujiunga na Freemasons, alikwishatoa baada ya kifo chake, vyombo vya habari viliandika na kutangaza.

Kwa hiyo hakuwa na sababu ya kuendelea kueleza taarifa hizo kwenye viwanja vya wazi. Ukifuatilia matukio ya mchungaji huyo, utagundua anachofanya ni kujitafutia umaarufu, mwaka jana alijisingizia kifo kilichofanana na kifo cha Marehemu Kanumba, magazeti ya udaku yaliandika taarifa zake na kuonyesha picha aliyokuwa kwenye jeneza.

Baada ya muda mfupi aliibuka kiwanja cha Buguruni akitoa maelezo ya namna Kanumba alivyokufa. Mchungaji huyu ni hatari anayestahili kuchukuliwa hatua kali za kisheria.

Wadua, Shirikisho, Familia na marafiki wa marehemu jitokeni kumtia adabu mtu huyo anayeendelea kujipatia umaarufu sambamba na kipato kupitia jina la Kanumba. Kwani hawezi kuzungumzia Freemasons bila ya kutaja jina la marehemu Kanumba.

Ikiwa nia yake ni safi, angeelezea imani ya Freemasons kwa kumtaja aliyekuwa kiongozi wa Afrika Mashariki, Sir Andy Chande , sio vizuri kumtaja mtu aliyekufa ambaye hawezi kujitetea.

Kwa mujibu wa maelezo yake anadai alikuwa anajua kama Kanumba ni muumini wa Freemasons kabla ya hajafa. Kama ni kweli, kwanini alikaa kimya mpaka alivyokufa na kuibuka kuanza kuzungumza mambo ambayo hayana faida kwa jamii. Badala yake ni kuhamasisha jamii ya vijana kutaka kujiunga na imani. Sisi wana Swahili Cinema News tunasikitishwa na tabia ya mchungaji huyo.

Movie Tanzania, Inawezekana kila mwigizaji kutayarisha sinema?

  Inawezekana kila mwigizaji kuwa mtayarishaji wa sinema. Jibu linaweza kuwa ndio au hapana, kwa sababu utayarishaji wa sinema unaweza kufanywa na mdau yoyote mwenye uwezo wa fedha, ila awe anajua sanaa ya sinema kwa undani zaidi. Vinginevyo anaweza kuingia mikononi mwa wababaishaji na kujikuta akipoteza muda na fedha.

Mwigizaji anaweza kutayarisha sinema ila ni lazima awe na upeo mkubwa wa kutayarisha sio kuigiza, unaweza kuwa mwigizaji mzuri lakini ukashindwa kuwa mtayarishaji au muongozaji mzuri yaani director mzuri.

Wapo madirector wazuri sana, lakini hawawezi kuigiza. Kwa sababu hawana taranta au tunaweza kuita kipaji, wapo waandishi wazuri wa hadithi na vitabu, lakini hawawezi kuandika script.

Wapo wachezaji wazuri wa soka lakini hawezi kuwa makocha wazuri, wapo makocha wazuri lakini hawakuwahi kucheza mpira kwa kiwango cha kuitwa mastaa. Kwa hiyo ni vizuri kujikagua kama una taranta kabla ya kufanya chochote unachotaka kufanya.

Wapo waigizaji wenye taranta ya kutayarisha sinema na kuziongoza vizuri, mfano mwigizaji Mel Colm Cille Gerard Gibson wa Marekani, wengi wanamfahamu kwa Mel Gibson ni mwigizaji, mtayarishaji, mwandishi wa script na muongozaji. Moja ya sinema aliyoongoza ni Apocalypto

Marekani na Ulaya wapo wengi wenye uwezo wa kufanya yote katika utengenezaji wa sinema, pia wapo ambao hawawezi. Wanatoa nafasi kwa wenzao wanaoweza.
Kwa Tanzania hali ni tofauti, wengi hawawezi kutayarisha sinema wala kuziongoza. Ila wanajilazimisha kufanya hivyo kwa sababu wanajiona mastaa, ukweli unabaki kama sinema wanazotayarisha zinakuwa hazina ubora unaotakiwa.

Ukijiona huna uwezo wa kuandika script, kutayarisha na kuongoza. Tafuta wadau wenye uwezo wa kufanya kazi hizo kwa ajili ya kupata sinema nzuri. Matokeo ya kila kitu kutaka kufanya mwenyewe ni kutayarisha kazi mbovu.

Aliyekupa fedha za kutayarisha sinema akigundua sinema yako haipendwi na watazamaji, atakumwaga na hatimaye kupotea katika soko la sinema kabisa.

Kama lengo la wadau ni kuendeleza sekta ya uigizaji, waigizaji wanaopata bahati ya kuingia mikataba na wasambazaji kwa ajili ya kutayarisha sinema, wasiwe wabinafsi. Kuendekeza ubinafsi ni kuua sekta sinema, inayoongoza hivi sasa kwa kutoa ajira kwa vijana na wazee.
 
 
 
 

Saturday, February 16, 2013

Movie Kitanzania bila mastaa haziuziki?


Baadhi ya wasambazaji wa sinema  nchini,  wameibuka na  kituko kitakachosambaratisha soko la sinema za kibongo, kama  hawatakubali kuachana  na mawazo yao mgando ya kudai sinema bila ya msanii maarufu huwezi kuuza.

Uchunguzi  wetu umeonyesha  kabla ya kuwa na wasanii maarufu, watanzania walikuwa  wakinunua sinema na kuangalia,  wapo waliokuwa wakinunua sinema za kihindi bila ya kuwafahamu waigizaji hao kama maarufu au sio maarufu.

Wapo waliokuwa wakinunua sinema za kichina, kijapan na kizungu. Baada ya kuingia sinema za kinaigeria watanzania walizinunua,  walipokuwa wananunua hawakujua kama wasanii hao ni maarufu, ila walinunua kwa ajili ya kupata burudani ya sinema.

Kama wasambazaji wa nchi nyingine wangekuwa na mawazao kama ya wasambazaji wetu. Tusingeshuhudia  waigizaji wapya wakiibuka kila kukicha. Tungeendelea kushuhudia wale wale wa zamani ambao umri umeanza kuwatupa mkono. 

Wasambazaji wanatakiwa kufahamu kama waigizaji wanaitwa mastaa hivi sasa, kuna watu wamewafikisha hapo,  hawakuzaliwa wakiwa mastaa. Mnatakiwa na nyinyi kuzalisha wapya sio kutafuta mastaa walitengenezwa na wenzenu.


Bongo movie, Sinema bila Staa huwezi kuuza




                                                         Jamila chipukizi anayekuja juu
Baadhi ya wasambazaji wa sinema  nchini,  wameibuka na  kituko kitakachosambaratisha soko la sinema za kibongo, kama  hawatakubali kuachana  na mawazo yao mgando ya kudai sinema bila ya msanii maarufu huwezi kuuza.

Uchunguzi  wetu umeonyesha  kabla ya kuwa na wasanii maarufu, watanzania walikuwa  wakinunua sinema na kuangalia,  wapo waliokuwa wakinunua sinema za kihindi bila ya kuwafahamu waigizaji hao kama maarufu au sio maarufu.

Wapo waliokuwa wakinunua sinema za kichina, kijapan na kizungu. Baada ya kuingia sinema za kinaigeria watanzania walizinunua,  walipokuwa wananunua hawakujua kama wasanii hao ni maarufu, ila walinunua kwa ajili ya kupata burudani ya sinema.

Kama wasambazaji wa nchi nyingine wangekuwa na mawazao kama ya wasambazaji wetu. Tusingeshuhudia  waigizaji wapya wakiibuka kila kukicha. Tungeendelea kushuhudia wale wale wa zamani ambao umri umeanza kuwatupa mkono. 

Wasambazaji wanatakiwa kufahamu kama waigizaji wanaitwa mastaa hivi sasa, kuna watu wamewafikisha hapo,  hawakuzaliwa wakiwa mastaa. Mnatakiwa na nyinyi kuzalisha wapya sio kutafuta mastaa walitengenezwa na wenzenu.


Vyombo vya habari vyawasahau Producer, Director na Script writer



Wadau wa sinema wanashindwa kuelewa kama waandishi wa script ni  kiungo muhimu sana katika utayarishaji wa sinema. Bila ya script huwezi kupata sinema, bila ya script huwezi kujua uwezo wa mwigizaji au director.

Mwandishi wa script anakuwa tayari ametayarisha sinema kimaandishi, waigizaji na director wanaitoa kwenye maandishi na kuiweka kivitendo.

Kila kinachofanywa na waaigizaji katika sinema husika  kimetoka katika akili ya mwandishi wa script. Cha ajabu  waandishi na watangazaji  wanawasahau  waandishi wa script na kutoa nafasi kubwa kwa waigizaji. Kitendo hicho kinachangia kuifanya jamii kutofahamu umuhimu wa waandishi wa script.

Angalau madirector wanapata nafasi ya kutangazwa katika vyombo vya habari, waandishi script bado hawajapata nafasi hiyo,  lakini hata madirector wanapata nafasi finyu sana ukilinganisha na waigizaji.

Madirector wanaopata nafasi katika vyombo vya habari ni wale wanaodirect na kuigiza, kwa wale wanaodirect  bila ya kuigiza bado wananafasi finyu katika vyombo vya habari.

Ikiwa kwenye  muziki, mtayarishaji (Producer )  anapata nafasi kubwa katika vyombo vya habari, inashindikana  vipi kwa  madirector, maproducer, mascript writer  wa sinema kupata nafasi kubwa kama wanavyopata waigizaji au watayarishaji wa muziki.

Imefika  wakati wa vyombo vya habari kubadili na kuandika  taarifa za madirector, maproducer na waandishi wa script.

Tatizo kama hili lipo kwenye muziki wa taarabu,  anayetunga wimbo, muziki na wapigaji vyombo hawapewi  nafasi kubwa  kwenye vyombo vya habari kuliko  waimbaji.  Badilikeni wadau wa vyombo vya habari.

Camera man, mwigizaji wanapokuwa madirector



                                                                   Camera man
Imekuwa kawaida katika nchi yetu ya Tanzania kumsikia  camera man au mwigizaji akibishana na Director.  Ugonjwa huu usipokemewa unaweza kuambukiza kizazi kijacho katika sanaa ya sinema.

Kitaalamu  production yote ipo chini ya director,  yeye  ndiye mwenye maamuzi ya mwisho. Anapoamua  jambo lolote hakuna mwenye ubavu wa kubisha, mliokuwa hapo mnaweza kumpa ushauri,  ni maamuzi yake kukubali au kukataa.

Mfano mzuri  director ni kocha wa timu ya mpira,  huwezi kuingilia maamuzi ya kochi katika kutayarisha kikosi chake.

Kwa upande wa utayarishaji wa sinema  madirector wanaingilia katika kufanya maamuzi yao,  matokeo yake wanajikuta wanatayarisha sinema  yenye makosa. 

Makosa yenye yanasababishwa na kutokuwa makini. Mwigizaji anambishia director, camera man anambishia director anajifanya anajua sana,  matokeo ya mabishana hayo ni Director kupoteza umakini na kufanya kazi mbovu.

Camera man  na waigizaji  tuwaache  madirector wafanye kazi zao,  kuwaingilia kuna sababisha kuendelea kushuhudia sinema zenye mapungufu na makosa ya kijinga, ambayo hayahitaji  elimu ya chuo kikuu kuweza kuyabaini.

Kama wewe mwigizaji fanye kile ulichokufikisha pale, mambo ya kuelekeza hayakuhusu. Nawe camera man fanye kazi yako ya kupiga picha, kuelekeza waigizaji namna ya kucheza sio kazi yako. Hiyo ni kazi ya Director na msaidizi wake.

Kila mmoja akizingatia jukumu lake, makosa ya kipumbavu katika sinema zetu yatapungua.  Ushauri kwenu wenye tabia hizo, kusema  ACTION   na CUT sio sababu ya kujiona unaweza kudirect movie.

Kuidirect movie ni zaidi ya ACTION  na CUT,  tuwape nafasi  madirector kufanya kazi zao kwa uhuru zaidi. Unajua kama kusimama nyuma ya camera sio sababu ya kuitwa camera man, au kubeba  jezi na mpira sio kigezo cha kuitwa mchezaji. Au kubeba gitaa sio sababu ya kuitwa mwanamuziki. Au kushinda kutwa chumba cha habari huwezi kuitwa mwandishi au mtangazaji. Unaweza kuwa mfagiaji.