Monday, December 1, 2014

Mwigizaji Bollywood azabwa kofi kwa kuvaa nguo fupi


                                                                   
                                                                   Gauhar Khan
                                                                        Gauhar Khan
                                                                    Gauhar Khan
                                                                    Gauhar Khan
                                                                          Gauhar Khan
                                                                 Gauhar Khan

Mwigizaji maarufu wa Bollywood ambaye pia ni mwanamitindo, Gauhar Khan, alizabwa kofi wakati wa shughuli ya kurekodi makala ya kipindi kuhusu maisha yake.
Mwigizaji huyo alizabwa kofi na mmoja wa waliokuwa wanatazama kipindi hicho eti kwa kuwa alikuwa amevalia nguo fupi sana.
Polisi walimkamata mwanamume mwenye umri a miaka 24 kwa kumshambulia mwigizaji huyo wakati wa kurekodi kipindi kijulikanacho kama , ''India's Raw Star'' mjini Mumbai.
Mwanamume aliyemshambua muigizaji huyo alinukuliwa akimkaripia na kumwambia, kwamba kwa kuwa yeye ni mwanamke wa kiisilamu hapaswi kuvalia nguo fupi kama ile.
Mwanamume huyo alitarajiwa kufikishwa mahakamani Jumatatu.
Tukio hilo lilitokea Jumapili, wakati wa kurekodiwa kwa makala ya mwisho ya kipindi hicho.
Uchunguzi umeonyesha kuwa mtu mmoja kutoka kwa mashabiki, alianza kumkejeli Khan ambaye naye hakumsaza kwani alianza kujibizana naye. Katika majibizano yao, mwanamume huyo alimzaba kofi Khan.
Duru zinasema kuwa walinzi waliokuwa katika eneo hiloi walimshinda nguvu mwanamume huyo ambayo walimkabidhi kwa polisi.
Polisi walimshitaki mwanamume huyo kwa kitendo cha kumzaba kofi Khan ambaye ameigiza katika filamu nyingi tu ikiwemo, 'Rocket Singh: Salesman of the Year.'

Saturday, November 29, 2014

Sinema kumi za kitanzania zinazofanya vizuri sokoni

Mwaka huu kuanzia Januari mpaka Novemba zimeingia sokoni sinema nyingi sana,  kila sinema ilikuwa na utamu sambamba ubora wake, watayarishaji na waigizaji sambamba waongozaji walijitahidi kila mmoja kuhakikisha anafanya kazi nzuri itakayokubalika na jamii.
Kama tulivyosema mwanzo sokoni zimeingia sinema nyingi,  kati ya hizo  sinema kumi zimetokea kupendwa na watu wengi sana.  Tafiti za kupendwa  kwa sinema hizo zilizofanyika katika mkoa wa Dar es Salaam  na Arusha kwa wauzaji wa maduka ya jumla na  maduka ya rejareja,  sambamba na wauzaji wanaotembeza mitaani maarufu kwa jina la wamachinga.

 1.                                                       Jamila na pete ya ajabu
                                      Jamila imetokea kuvuwatia watoto wengi sana kwa mujibu wa
                                                   wadau wetu   waliotupatia taarifa hizo
                                                                   

                                                                                                                                                      
 2                                                                       Chausiku   

Chausiku imetokea kuwa gumzo kubwa katioka maeno ya uswahili
3                                                                Siri ya Giningi
                                                                             

                                                                                   
 4                                                             Zena na Betina
                                                                          
5                                                              Hakumu ya ndoa yangu
                                                                             
6                                                               Tom Boy  
                                                                       


 7                                                        Uliyemchokoza kaja
                                                                           



 

8                                                                    Nahama

                                                                           

 9                               Nendeze Mwali wa Kizaramo ( Sinema hii haina kava)

                                                                         

10                                                         Kwanini Mama 
                                                                        

                                                                     



Friday, November 28, 2014

Waigizaji vibonge wa Nigeria wanavyotesa na ubonge wao kuliko wembamba


Wakati  nigeria wasanii wa kike wenye maumbo makubwa na yakuvutia wanaongoza katika kurasa za mbele za magazeti ya udaku na majarida mbali mbali ya burudani sambamba na mitandao ya kijamii kutokana mavazi yao.  Mara nyinyi wasanii wanakuwa wanalipuka pamba za ukweli zinazoonyesha baadhi ya maungo yao yakiwa nusu. Kitendo hicho kimetokea kuwa gumzo kubwa katika miji  mbali mbali ya  nchi hiyo ,  miongoni mwa nguo wanazopenda kuvaa ni zile zinazoonyesha sehemu kubwa ya amatiti yao yakiwa wazi sambamba na mapaja yao. Wengine wanafikia mpaka kuonyesha vitovu vyao. Kwa mujibu wa  maelezo kwa nyakati tofauti wamesema si kitu cha ajabu kufanya hivyo kwani kila mmoja ana utaratibu wake wa kuvaa hasa kwenye matukio  mbali mbali cha muhimu ni kwamba hawatembei uchi wa mnyama. Kama kuna watu wanachukizwa au waandishi wanafuatilia maisha yetu, watajijua wenyewe kila ana stahili ya amaisha yake aliyochagua kuishi. Wafuatao ni miongoni mwa mastaa wanaotingisha kwa kuvaa mavazi yanawachanganya wanaume na hata wanawake wenzao, sambamba na kulalamikiwa na baadhi ya watu.
                                                                          
                                                                Ifeoma Okeke
Ni mwanamke anayejua  kuvaa kulingana na mwili wake unataka kuvalishwa nini, sio kujivalia ovyo ovyo kwa kuiga. Licha aya unene wa umbo lake bado anamvuto wa hali ya juu kutokana kupangili amvazi yake. Licha ya kuvaa nusu uchi bado anaonekana kutingisha kuvutia wanaume wengi kumtazama mara wanapobishana . Staa huyu alitamba na sinema ya Evil Genius, hata mara kwa mara amekuwa amesema hajisikii vibaya kwa jinsi anavyovaa na wala haoni ajabu au aibu. Mwanamama anakaribia kufikisha kilo mia mbili.


 
                                                                         

                                                         Chioma Toplis
                                                            
Ni mwanadada mwenye mvuto wa hali ya juu hasa namna anavyojua kumechisha mavazi yake viatu, licha kuwa bonge la mtu ni mpenzi wa viatu virefu.  Kwa mujibu wa maelezo amejikagua na kugundua  kama miezi ya karibuni uzito umekuwa ukipanda kwa kasi mpaka anashangaa. hata hivyo amesema licha kufanya maoezi bado uzito unaongezeka, ametamba na sinema ya Stolen Bible



                                                                     Eniola Badmus
Ana bonge la kitambi siku hizi na wala hajawahi kusikika akilalamika. Msanii huyo maarufu kwa jina la Gbogbo Big Girl, ni binti anayependa kujipodoa ingawa hakuna uhakika kama anajua madhara yake. Uchunguzi unaonyesha kwamba mwili wake mkubwa ndiyo umemfanya akawa maarufu zaidi kuliko kazi anazofanya.




                                                                            


                                                                    Adaora Ukoh
                                                                  
Marafiki zake wamesikika wakimuonya mara kadhaa, lakini ni kama vile anaona yuko sawa. Miezi michache iliyopita alizindua gauni kubwa alilolipa jina la Adaora akiwa anamaanisha kwamba ni nguo maalum kwa ajili ya wasichana mabonge kama yeye. Anaamini kila mwanamke ni mrembo na uzuri uko ndani na si ukubwa wa mwili japokuwa ameanza mazoezi ya gym.

                                                                                Foluka Daramola                                                                                     
Foluke Daramola anaijua kazi yake, acha apewe sifa. Lakini mashabiki wake wamekuwa wakiguna kila wanapomuona kutokana na unene wake mkubwa. "Unene au mwili wa mtu ni suala binafsi la maisha ya msichana hakuna wa kumuamulia, najua ninachopaswa kufanya," ndivyo anavyosema.

Kidawa ni sinema yenye mazingira ya uswahili kikweli kweli

                                                  Nuru Mohamed a.k.a Kidawa
                                                                Mohamed Nurdin
                                                      Haji Adam  na Mohamed Nurdin
                                                               Haji Adam
                                                              Zainabu Mshindo

Katika makala yetu ya Sinema , leo naiangalia Sinema  inayoitwa Kidawa Uswahilini. Iliyotayarishwa na kampuni ya  Kapelele ya jijini Dar es Salaam na kusambazwa na kampuni ya BMO, pia  ya jijini Dar es Salaam. Ni filamu nzuri inayoelezea  vituko na visa vya wakazi wa maeneo ya uswahilini, hasa wale wanaoishi katika nyumba za kupanga.
Kidawa uswahilini inamzungumzia mwanamke anayeitwa Nuru Mohamed aliyecheza kwa jina la Kidawa na rafiki yake  Zainabu Mshindo aliyecheza kwa jina la Cecy ,  Mohamed Nurdin aliyecheza kwa jina Faiza, Haji Adam aliyecheza kama Mwasa pamoja na wapangaji wengine.
Hadithi (Story):
Wazo la hadithi  lilikuwa zuri sana, liliangalia mazingira ya maisha ya kweli wa wakazi wa maeneo ya uswahili na vituko vyao. Umbeya, chuki, shida, wivu wa kimaendeleo, ugomvi, matusi, kusutana, vyote hivyo vilionekana katika hadithi hii.  Kitu ambacho kwa watu wanaoishi maeneo ya watu wenye uwezo ni nadra kushuhudia mambo kama hayo. 
Nuru au Kidawa amecheza kama mwanamke mkorofi anayegombana na wenzake kila wakati,  nyumba inakosa amani na furaha kutokana na tabia yake ya ukorofi.  Zainabu au Cecy  katika sinema hiyo amecheza kama  rafiki wa Kidawa, anayevutiwa na ukorofi anaofanya Kidawa.
Mashoga hao wawili wametokea kuwa kero kwa wapangaji wenzao ambao ni Haji Adam au Mwasa na  Mohamed Nurdini au Faiza pamoja na wapangaji wengine wanaoishi katika nyumba hiyo yenye idadi kubwa ya wapangaji.
Sinema inaanza kwa Kidawa kupigana na mpangaji mwenzake anayeitwa Mwajuma,  majirani wanajitokeza kuwatenganisha,  kidawa anaonekana kutokubali na kuendelea kutoa matusi. wakati hilo likiwa bado halijapatiwa ufumbuzi, Mickynessy Joseph  aliyecheza kwa jina la Sinai  anamkuta Kidawa na rafiki yake Cecy wanamsema dada yake anayeitwa Sina. Wanarushiana maneno machache yanayoashiria kutaka kuleta ugomvi.
Kabla ya kumalizika hilo, wapangaji wote wanakaa kikao kujadili suala la umeme, kabla ya kufikia mwaka wa kikao hicho. Kidawa anakivuruga kikao kwa maneno yake ya kashfa na matusi na kisha kuondoka zake,  akidai kwamba hawezi kuendeshwa na watoto.
Kidawa aliongea hivyo baada ya watoto waliokuwa katika kikao hicho kudai kwamba Kidawa na Jenga wanamatumizi mabaya ya umeme.  Jenga ana mafriji mawili, Kidawa anapitisha marundo ya nguo ya rafiki zake kupiga pasi.
Kauli hiyo inamchukiza Kidawa na kuondoka zake katika kikao hicho, rafiki yake Cecy ananyanyuka anamfuata huku akiwa anatoa maneno ya matusi kumwambia miongoni mwa watoto waliokuwa wakichangia katika kikao hicho. Kiujumla  sinema hiyo inaelimisha na kuburudisha.
Usaili (Casting )
Mtu aliyefanya usaili (Casting Director)  alifanikiwa kuchagua waigizaji waliofanikiwa kuzitendea haki nafasi zao walizopangiwa kucheza.  Kila mmoja amecheza kwa kiwango cha hali ya juu, pongezi kwa casting director kwa kazi nzuri aliyofanya.
Mavazi (Costumes)
Aliyepangwa kuhakikisha waigizaji  wanavaa nguo zinazoendena na wakazi wa mitaa ya uswahilini,  kila mwigizaji alivaa kulingana na nafasi yake aliyocheza. Wapo wale waliovaa na  na kuonekana ni miongoni mwa wenye maisha nafuu zaidi ya wenzao kama vile Sinai na dada yake Sina anayeishi na mume wa mtu anayeitwa Faiza ambaye ni Nurdini. Wengine walionekana  ni wale wenye maisha ya kawaida hata Televishana hawana wanaangalia katika vyumba vya wenzao.
Mapambo (Makeup)
Mtu wa mapambo alifanikiwa kuwapamba vizuri na kuonekana ni miongoni mwa waliofanikiwa kuvaa taswira ya wakazi wa mitaa ya uswahilini kwa namna walivyopambwa na kupambika.
Mandhari(Location)
Mtu aliyepewa jukumu la kutafuta mandhari (Location) alifanikiwa kutafuta nyumba yenye uwezo wa kuchukua wapangaji wengi kwa wakati mmoja. Ki kweli kabisa anastahili pongezi kwa kufanikiwa kutafuta nyumba inayochukua wapangaji wengi kama nyumba hiyo iliyotumiwa kuchezea sinema ya Kidawa uswahiini.
Mwanga: (Light)
Mshika taa aliweza kushirikiana  vizuri na camera man wake  kuhakikisha wanatoa picha zenye ubora mzuri, licha baadhi ya scene zilionekana kuwa na mwanga hafifu pamoja na ubora mdogo. Alipoulizwa camera man   anayejulikana kwa jina la Rajabu Ngatale aliyeshuti sinema hiyo alisema baadhi ya scene zilitoka hivyo kutokana na camera ya mwanzo waliyotumia ilikuwa ina matatizo ya kiufundi.
Sauti (Sound man)
Sauti katika sinema hii haikuwa nzuri  sana,  hasa zile scene za  nje zilikuwa zina mvumo wa upepo. katika scene za ndani kutlikuwa na tofauti kubwa ya mabadiliko ya sauti hasa inapoingia shot ya CU  yaani ya karibu sauti inasikika vizuri. Inapokuja shot ya mbali yaani Long shot sauti inakuwa ndogo.  Tatizo lilitakiwa kuwekwa sawa na mhariri aliyehariri sinema hiyo.
Mhariri (Editor)
Mhariri alijitahidi kadri ya uwezo wake, lakini alishindwa  kuweka sawa tatizo la sauti. wakati mwingine mhariri anatakiwa  kuwa makini na sauti, sinema bila ya kuwa ana sauti inayosikika vizuri inapoteza utamu wake hata kama itakuwa stori  nzuri.
Muongozaji (Director)
Katika sinema muongozaji ni mtu muhimu sana katika kuhakikisha sinema inatayarishwa katika ubora unaotakikana kulingana na hadithi husika kwa kulinda wazo la mwandishi au mtunzi, ukiangalia filamu hii script imetendewa  haki licha ya mapungufu madogo madogo yalijitokeza kutokana  na sababu za kiufundi. Kwa wasiobahatika kuiona waitafute kushuhudia ufundi wa waigizaji wa sinema hiyo. Kwa naishi hapa tukutane katika sinema nyingine ya wiki..

Jacky Wolper mkali wa mapozi kuliko wenzake nchini Tanzani

                                                                
                                                   Wolper  pozi hili kama sio yeye
                                                              Wolper, hapa utakubali yeye
                                                       Wolper, na hapa mnasemaje alivyopozi
                                                           Hapa unasemaje jamani
                                                         Ametulia kama hataki kuongea
                                                 Anaonekana ana mawazo vile.

Tukubali au tubishe ukweli utabaki vile ulivyo kama mwanadada Jacky Wolper  ni mwigizaji wenyewe mapozi ya kipekee,  mapozi yake yanamuongeze mvuto wa hali ya juu katika picha zake anazopiga mara kwa mara. Baadhi ya watu wamesikika wakisema kwamba Wolper ni mkali wa mapozi katika upigaji wa picha tofauti  kuliko waigizaji wenzake. Na ndiyo maana aliweza kuchukua ushindi wa mwanamke mwenye mvuto. Hebu tazama picha hizi utagundua kama huyu binti ni mkali wa mapozi.

Wema bado ni kipenzi cha wabongo kila anachofanya wanashabikia

                                                                        
                                                      
Bila ya kupindisha ukweli mwigizaji Wema Sepetu ni miongoni mwa waigizaji wenye nyota kali sana kwa wapenzi na mashabiki,  ukitaka kudhibitisha hilo angalia magazeti ya udaku yakiwa na picha yake sambamba na stori yake. watu wengi kwenye daladala utawaona wanamagazeti hayo wanasoma. Udhibitisho mwingine angalia idadi ya wasomaji na watazamaji wa video zinazomuhusu yeye  katika blog mbali mbali ni kubwa kuliko waigizaji wengine.  Udhibitisho mwingine jaribu kuchungu wale watu waliokuwa karibu yake walivyojipatia umaarufu kubwa, baada ya kuachana nao wengi wao wanapoteza umaarufu.  Kama unataka kuwa maarufu jipendekeze kwa  Wema hata kwa kubeba mkoba wake au kumfuta jasho, siku tatu ya kuwa naye tayari utapamba katika kurasa za magazeti ya udaku. Wema bado ni kipenzi cha wabongo, habari ndiyo.

Toni Braxton kuigiza kama msagaji

         




Mkali wa  muziki wa taratibu Toni Braxton ameonyesha nia aya kujitumbukiza katika fani ya uigizaji, baada  ya mwaka jana kutangaza kustaafu mambo ya muziki kama sio kupumzika.  Amesema nafsi yake inamtuma kufanya kitu ambacho alikuwa anakipenda sana toka zamani.Kwa mujibu wa maelezo yake anataka kuigiza sinema, tena anataka kuigiza kama msagaji. "Toka zamani nilikuwa na nndoto ya kuigiza kama mwanamke msagaji, nadhani sasa ndoto yangu inaweza kutimia kwa kufanya kitu roho inapenda." aliema Toni Braxton mwenye miaka 46, amabye amewahi kunyakuwa tuzo nne za grammy.











Mkali wa Home alone Macaulay Culkin hajafa







                                                                  
                                                       Macaulay Culkin alivyokuwa mdogo
                                 Macaulay Culkin alivyokuwa sasa baada ya kutumia madawa ya kulevya
                               Macaulay Culkin alivyoanza kujitumbukiza katika madawa ya kulevya
                                                     Macaulay Culkin katika pozi la kilevi
                                                      Macaulay Culkin alivyokuwa mdogo
                                                           
Yule makali wa sinema iliyojipatia umaarufu mkubwa ya home alone , Macaulay Culkin na pia ni mwanamuziki ameibuka na kufuta tetesi zilisambaa kwamba amefariki dunia. Hivi karibuni kuliibuka tetesi za kufariki mkwake licha ya kutokuwa na ufafanuzi wa kina kuhusiana na chanzo cha kifo chake. Taarifa za kifo chake zilienea katika mitandao ya kijamii,  baada taarifa hiyo. Dodo huyo aliibuka ana kusema "Tuko kwenye ziara ya kimuziki nyinyi wajinga, hakuna aliyekufa."  Ujumbe ulikuwa na picha inayomuonyesha akiwa rafiki zake ameshika kinywaji akiburudika.

Mkenya Lupita Nyong'o kuigiza katika Americanah

 







Muigizaji nyota kutoka Kenya Lupita Nyong'o amejumuishwa katika wasanii watakaoigiza katika filamu ya AMERICANAH  inayotokana na kitabu cha mwandishi Chimamanda Ngozi Adichie. Filamu hiyo haitofautini sana na  ile sinema  ya ''12 Years a Slave'' iliyompelekea mrembo  huyo kushinda tuzo la Oscars mwezi Februari itatayarishwa  na kampuni ya PLAN B P inayomilikiwa na Mtayarishaji na muigizaji  maarufu wa filamu, Brad Pitt . Filamu hiyo mpya ya AMERICANAH inaelezea mada ya mapenzi kati ya  wapenzi  wawili wa Nigeria ambao licha ya penzi kuchanuka kati yao wanatenganishwa na maswala ya uhamiaji. Muigizaji huyo aliwaambia mashabiki wake kuwa ni heshma kubwa kwake kupewa nafasi ya kuigiza katika filamu hiyo inayotokana na kitabu cha Adichie. Kitabu hicho cha Americanah, kiachoelezea maisha ya wapenzi wawili Ifemelu na Obinze. Kitabu hicho kilishinda tuzo la ''US National Book Critics Circle Award mwaka uliyopita. Aidha kimeteuliwa kuwa moja kati ya vitabu kumi bora na jopo la 'The New York Times Book Review. Nyongo aliiambia BBC kuwa baada ya kukisoma kitabu hicho , alitamanishwa na jinsi Ifemelu na mpenzi wake Obinze,walivyostahimili majaribu mengi katika uhusiano wao . Hali ambayo inawakumba waafrika wengi ambao kutokana na tamaa ya mafanikio wanakwenda ughaibuni kutafuta ajira na wengine kwa masomo ya juu. Mbali na Americanah , Adichie anajivunia tunu ya uandishi wa vitabu vingine kama vile Purple Hibiscus na Half of a Yellow Sun, ambayo pia imefasiriwa na kuigwa katika filamu na muigizaji nyota katika 12 Years a Slave , Chiwetel Ejiofor. Nyong'o aliwavutia wapenzi wa filamu kote duniani aliposhirikiana na Ejiofor na kutwaa taji la Oscar katika 12 years a slave.