Showing posts with label sokoni. Show all posts
Showing posts with label sokoni. Show all posts

Tuesday, January 6, 2015

FILAMU YA BEKITATU kuingia sokoni hivi karibuni

                                                                  Posters ya Bekitatu

Kikundi cha Sun Shine Artists Theatre chenye makao yake makuu  Ilala, jijini Dar es Salaam, kimetayarisha sinema inayoitwa Bekitatu inayotarajia kuingia sokoni hivi karibuni.  Kwa mujibu wa maelezo ya mtayarishaji  wa sinema hiyo Haji Dilunga amesema Beki tatu inaelezea na kutoa taswira ya jamii ya kitanzania inavyoishi na wafanyakazi wa ndani. Ni sinema inayofichukua siri nzito ya maisha ya wafanyakazi wa ndani na mabosi zao.Katika sinema hiyo Mwanadada Nurati Ngeleshi amecheza kwa jina la Rukia,  akiwa na watoto zake ambao ni  Nurdin  Salum aliyecheza kama Jaffary.  Clemensia Salum aliyecheza kama Leila, Hassan Lukuu aliyecheza kwa jina la Bakari akiwa kama mdogo wake Rukia. Mwingine ni Hawa Hassan aliyecheza kwa jina Sikitu au Bekitatu, katika sinema hiyo  amecheza kama mfanyakazi wa ndani wa familia ya Rukia.  Sinema inafumbua fumbo la kwanini wafanyakazi wa ndani wanatokea kutenda vitendo vya kikatili kwa mabosi wao."Sidhani kama  wewe mpenzi wetu utakuwa unafahamu, jibu lake ni kutafuta sinema hiyo utafahamu kwanini wafanyakazi wa ndani wanatenda vitendo vya kikatili kwa mabosi zao. Ni sinema inayosikitisha na kuhudhunisha, wakati huo huo kufurahisha na kutoa elimu kwa jamii." alisema Dilunga.Sinema hiyo imetungwa na kuandikwa script na Haji Dilunga, inasambazwa na kampuni ya BMO ya jijini Dar es Salaam ,  kuikosa sinema hiyo ni sawa na kukosa kitu muhimu sana katika maisha.Kama unakumbukumbu ya sinema ya Kwanini Mama? Jamila na Pete Ajabu, Mwandishi, Sound of Death   na nyingine nyingi zilizoandikwa na Haji Dilunga.  Beki tatu ni miongoni mwa hizo au zaidi ya hizo kwa utamu wa stori na mtiririko wa visa.Usiogope kununua kwa vile imechezwa na waigizaji wachanga, ununu ili upate uhondo na kutambua uwezo wa waigizaji wanaochipukia katika ulimwengu wa sinema.wale wanaotaka nakala ya sinema yetu wasikose kupiga namba hizi 0753 833773 au 0655 833 772.

Saturday, November 29, 2014

Sinema kumi za kitanzania zinazofanya vizuri sokoni

Mwaka huu kuanzia Januari mpaka Novemba zimeingia sokoni sinema nyingi sana,  kila sinema ilikuwa na utamu sambamba ubora wake, watayarishaji na waigizaji sambamba waongozaji walijitahidi kila mmoja kuhakikisha anafanya kazi nzuri itakayokubalika na jamii.
Kama tulivyosema mwanzo sokoni zimeingia sinema nyingi,  kati ya hizo  sinema kumi zimetokea kupendwa na watu wengi sana.  Tafiti za kupendwa  kwa sinema hizo zilizofanyika katika mkoa wa Dar es Salaam  na Arusha kwa wauzaji wa maduka ya jumla na  maduka ya rejareja,  sambamba na wauzaji wanaotembeza mitaani maarufu kwa jina la wamachinga.

 1.                                                       Jamila na pete ya ajabu
                                      Jamila imetokea kuvuwatia watoto wengi sana kwa mujibu wa
                                                   wadau wetu   waliotupatia taarifa hizo
                                                                   

                                                                                                                                                      
 2                                                                       Chausiku   

Chausiku imetokea kuwa gumzo kubwa katioka maeno ya uswahili
3                                                                Siri ya Giningi
                                                                             

                                                                                   
 4                                                             Zena na Betina
                                                                          
5                                                              Hakumu ya ndoa yangu
                                                                             
6                                                               Tom Boy  
                                                                       


 7                                                        Uliyemchokoza kaja
                                                                           



 

8                                                                    Nahama

                                                                           

 9                               Nendeze Mwali wa Kizaramo ( Sinema hii haina kava)

                                                                         

10                                                         Kwanini Mama