Tuesday, January 6, 2015

FILAMU YA BEKITATU kuingia sokoni hivi karibuni

                                                                  Posters ya Bekitatu

Kikundi cha Sun Shine Artists Theatre chenye makao yake makuu  Ilala, jijini Dar es Salaam, kimetayarisha sinema inayoitwa Bekitatu inayotarajia kuingia sokoni hivi karibuni.  Kwa mujibu wa maelezo ya mtayarishaji  wa sinema hiyo Haji Dilunga amesema Beki tatu inaelezea na kutoa taswira ya jamii ya kitanzania inavyoishi na wafanyakazi wa ndani. Ni sinema inayofichukua siri nzito ya maisha ya wafanyakazi wa ndani na mabosi zao.Katika sinema hiyo Mwanadada Nurati Ngeleshi amecheza kwa jina la Rukia,  akiwa na watoto zake ambao ni  Nurdin  Salum aliyecheza kama Jaffary.  Clemensia Salum aliyecheza kama Leila, Hassan Lukuu aliyecheza kwa jina la Bakari akiwa kama mdogo wake Rukia. Mwingine ni Hawa Hassan aliyecheza kwa jina Sikitu au Bekitatu, katika sinema hiyo  amecheza kama mfanyakazi wa ndani wa familia ya Rukia.  Sinema inafumbua fumbo la kwanini wafanyakazi wa ndani wanatokea kutenda vitendo vya kikatili kwa mabosi wao."Sidhani kama  wewe mpenzi wetu utakuwa unafahamu, jibu lake ni kutafuta sinema hiyo utafahamu kwanini wafanyakazi wa ndani wanatenda vitendo vya kikatili kwa mabosi zao. Ni sinema inayosikitisha na kuhudhunisha, wakati huo huo kufurahisha na kutoa elimu kwa jamii." alisema Dilunga.Sinema hiyo imetungwa na kuandikwa script na Haji Dilunga, inasambazwa na kampuni ya BMO ya jijini Dar es Salaam ,  kuikosa sinema hiyo ni sawa na kukosa kitu muhimu sana katika maisha.Kama unakumbukumbu ya sinema ya Kwanini Mama? Jamila na Pete Ajabu, Mwandishi, Sound of Death   na nyingine nyingi zilizoandikwa na Haji Dilunga.  Beki tatu ni miongoni mwa hizo au zaidi ya hizo kwa utamu wa stori na mtiririko wa visa.Usiogope kununua kwa vile imechezwa na waigizaji wachanga, ununu ili upate uhondo na kutambua uwezo wa waigizaji wanaochipukia katika ulimwengu wa sinema.wale wanaotaka nakala ya sinema yetu wasikose kupiga namba hizi 0753 833773 au 0655 833 772.

No comments:

Post a Comment