Tuesday, January 6, 2015

Nurati aibuka ndani ya Sinema ya Bekitatu

                                                         
                                                                 
Nurati Ngeleshi


Nurati Ngeleshi
Mwigizaji anayechipukia katika ulimwengu wa sinema nchini,  Nurati Ngeleshi a.k.a Belinda ameitaka serikali kuwasaidia kurahisisha upatikani wa vitendea kazi ili kuleta uhalisi katika sinema zao, sambamba na kutoa ushindani katika soko la kimataifa.
Kwa mujibu wa maelezo yake,  Belinda  amesema sinema nyingi zinazotayarishwa hivi sasa, hazina ubora na uhalisia kwa sababu ya kukosekana vitendea kazi na sehemu husika za kuigizia.
Amesema inakuwa vigumu kupata mavazi ya kweli ya polisi, jeshi, magereza na trafiki. Kukosekana kwa mavazi hayo kunachangia sinema zetu kupoteza uhalisi.
“Hebu angalia sinema za waafrika wenzetu kama Nigeria, Ghana, Kenya, Uganda na nchi nyingine. Utaona walivyopiga hatua katika kujenga uhalisia wa sinema zao kwa kutumia vitendea kazi husika na maeneo husika ya kuigizia" alisema Belinda.
Serikali ingesaidia watayarishaji kupata kwa urahisi mavazi ya askari wa aina zote, kutumia vituo vya polisi, majengo ya mahakama, bendera, majengo ya hospital za serikali sambamba na maofisi yake.
Kwa upande wa silaha, serikali ingeruhusu  bastola, bunduki na hata mabomu ya bandia kuingia nchini kwa ajili ya kurahisisha utayarishaji wa sinema kwa lengo la kuleta uhalisia.
Hivi sasa wengi wanatayarisha sinema kwa kutumia vibastola vya kuchezea watoto. Mtu yoyote akitazama anagundua kama ni kibastola cha watoto, ubora unapungua na uhalisia unapotea.
Belinda amewataka baadhi ya wadau na viongozi wa serikali, wasipende kulalamika kama sinema za kitanzania hazina uhalisia, eti kwa sababu wanavaa nguo fupi na kucheza sana kuhusu mapenzi. Kabla ya kulalamika walitakiwa kuitazama jamii ya kitanzania, wanaweza kupata majibu ya kwanini watayarishaji wanatengeneza sinema za kuvaa vimini na mapenzi.
Kwa kawaida mtayarishaji, mwandishi wa kitabu au mtunzi wa nyimbo, wana kawaida ya kutunga au kutengeneza yale mambo yanayotokea katika jamii yetu. Sio rahisi kutunga vitu vya kufikirika.
Kwa hiyo vimini na mapenzi ndivyo vinavyoendelea hivi sasa katika jamii yetu. Ndio maana sinema zinahusu mapenzi, nyimbo zinahusu mapenzi na vitabu vinahusu mapenzi.
Belinda ameitaka serikali kuweka utaratibu wa kuwakodisha waigizaji vitendea kazi vitakavyosaidia kuleta uhalisia na ubora tofauti na hivi sasa. Hata hivyo serikali inatakiwa kujua kama sinema imetoa na kuendelea kutoa ajira kwa watu wengi nchini.
Akizungumzia  maisha yake ya sanaa, anasema alizaliwa wilaya ya Rombo, mkoani Kilimanjaro. Sanaa alianza kuifanya  toka alivyokuwa shule,  baada ya kumaliza hakuendelea na mambo ya sanaa zaidi ya kujitumbukiza katika biashara.  Alikuwa akitoka Rombo kwenye Kenya kufanya biashara.
"Si unajua toka Rombo kwenda Kenya ni karibu sana, kipindi kile vijana wengi walikuwa wanakwenda Kenya kufanya biashara, hivi sasa hali imebadilika vijana wengi wanatoka kenya kuja Tanzania kufanya biashara." alisema Belinda.
Anadai kwa vile sanaa ipo katika damu yake alivyokuja Dar es Salaam aliamua kujifunza kuandika script na kuhakiki, miongoni mwa sinema ambazo alihakiki ni pamoja na Uwanja wa dhambi,  I love you, Bunge la wachawi,  Picnic, Popobawa, Zindiko na sinema mpya ya Bekitatu.
"Kwa vile nilikuwa na kipaji cha kuigiza  nilijikuta nikikosa kila wakati ninapoangalia sinema,  nikaamua kujinga katika kikundi cha Alwatan Artstis Theatre kilichokuwa chini ya uongozi wa  mwalimu wangu wa script, Haji Dilunga.", alisema Belinda
Baada ya kujiunga na kikundi hicho alishiriki kucheza sinema inayoitwa Julio na Romeo iliyotungwa na kuandikwa script na Haji Dilunga, katika sinema hiyo alicheza kama dada anayesambaratisha penzi la mdogo wake kwa kumtafutia msichana mwingine.
 Mbali ya sinema hiyo, alipata nafasi ya kushiriki katika sinema nyingine iliyotungwa na kuandikwa script na Haji Dilunga, inayoitwa Sound of soul.
Katika hali ya kuleta ushindani na changamoto katika ufanisi, Dilunga aliamua kuanzisha kundi la jingine linaloitwa Sun Shine Artists Theatre kwa ajili ya kuleta ushindani miongoni mwetu. Kwa bahati nzuri nilijikuta nikiwa katika Sun shine badala ya Alwatan, waigizaji wengine niliocheza nao sinema hizo nilizotaja wamebaki katika kundi la Alwatan.
Maisha ya kifamilia nimeolewa, nina watoto wawili wa kiume. Nampende mume wangu na kuheshimu, mwigizaji anayenivutia ni kutoka Nigeria anaitwa Omotola Jalade Ekeinde .  Anavutiwa na namna anavyoigiza na mapozi yake.
Belinda amewataka wapenzi na mashaki wanunue sinema ya Bekitatu wajionee kile alichofanya, watakubaliana naye kwa sanaa ni kipaji nasio kulazimisha kama wengine.
Amesema katika sinema ya Bekitatu amecheza kama mwanamke anayeishi na mfanayakazi wa ndani anayeitwa Sikitu au Bekitatu, katika sinema hiyo anaonekana anavyomtesa mfanyakazi wake wa ndani.
"Ni sinema nzuri inayosikitisha, kufurahisha na kuelimisha, kuikosa ni dhambi kubwa kwa sababu utakuwa umekosa ujumbe muhimu sana katika maisha yako,"alisema Belinda.Wale wanaotaka nakala ya sinema yetu wasikose kupiga namba hizi 0753 833773 au 0655 833 772.

No comments:

Post a Comment