Tuesday, January 6, 2015

Sinema Bekitatu ni mwanzo mambo makubwa yanakuja- Leila



                                                                 Clemensia Salum
Clemensia Salum

MWIGIZAJI Chipukizi katika tasnia ya filamu bongo, Clemencia  Salum a.k.a Leila amejigamba kwa kusema kuwa pamoja na kuwa msanii chipukizi anaamini kuwa ataliteka soko la filamu na tasnia kwa ujumla kwa sababu amejipanga kufanya kazi  nzuri  iliweza kushindana na wakongwe waliotangulia katika gemu kabla yake.
Kwa mujibu wa maelezo yake, Leila  amesema  hakuna kitu anachopenda  katika maisha kama kuigiza.  Kitendo cha kuanza kuigiza ni kutimiza ndoto yake ya muda mrefu, kwa hiyo hana budi kufurahi kwa kufanikisha kutimiza yale alivyokuwa akiyafikilia kila siku katika maisha yake.
“Ninaamini kuwa haya ndio maisha yangu na ili niweze kudumu katika tasnia ya filamu ni lazima niwe makini, najua kila mtu kwa sasa anatamani kuigiza na kuwa nyota, kwa kuandikwa sana katika vyombo vya habari lakini kwangu si hivyo niandikwe kwa ajili ya kazi, nia yangu nikuwapoteza wakongwe wote waliopo katika sanaa,”anasema Leila.
Mwigizaji huyo mwenye umbo dogo lakini ni machachari katika kuigiza, amejikuta akifananishwa na  mwigizaji wa Nigeria mwenye umbo dogo kama yeye anayeitwa Genevieve Nnaji .
"Nafurahishwa kufafanisha na mwigizaji mkubwa kama Genevieve Nnaji, kwa sababu ni miongoni mwa waigizaji ninaowapenda sana na ninajifunza vitu vingi toka kwake. Kwa upande waigizaji wa Tanzania anavutiwa na Ndumbagwe Misayo a.k.a Thea." alisema Leila.
Mwigizaji  huyo aliyezaliwa Desemba 28 mwaka 1996,  wilaya  ya Urambo mkoani Tabora, alipata elimu ya msingi katika shule ya Azimio,  mwaka 2010  alijikutaka akimaliza elimu yake ya msingi. Kutokana na matatizo ya kifamilia alishindwa kuendelea na masomo ya sekondari.
Hata hivyo hakutaka kuongelea zaidi matatizo ya kifamilia, ila alisema baada ya kushindwa kuendelea na elimu ya sekondari aliamua kuja jijini Dar es Salaam kwa mama yake Mzazi aliyekuwa tayari ameachana na baba yake.
Leila ni miongoni mwa wasichana wapambanaji au unaweza kuita ni miongoni mwa wasichana watafutaji, alivyofika jijini Dar es Salaam eneo la Vingunguti  anapoishi mama yake, akutaka kuwa golikipa wa kila kitu kutafutiwa na mama yake. Aliamua kutafuta shughuli za kufanya ili kujipatia kipato kitachomsaidia kuendesha maisha yake,
"Nimefanyakazi katika viwanda mbali mbali kama vile kiwanda cha kuteneneza vyombo vya plastic,  kiwanda cha kuteneneza Pipi,  kiwanda cha kutengeza mafuta ya kupikia, kiwanda cha kutengeneza kandambili, nimeuza duka la kuuza hina eneo la kariakoo na kutembea bidhaa za promosheni," alisema Leila.
Katika mahojiano na  gazeti hili,  Leila  anasema kwa vile sanaa ipo katika damu yake aliamua kutafuta kikudni cha kujiunga ili kuweza kujifunza mbinu mbali mbali za kuigiza na kufanyikisha malengo yake.
Miongoni mwa makundi aliyowahi kupitia ni pamoja na kikundi cha Dedede kilichokuwa Vingunguti, alifanya kwa muda mfupi na kuamua kuacha baada ya kugundua kikundi hicho hakina dira ya maendeleo zaidi ya kupotezeana muda.
"Kuna baadhi ya vikundi vinaanzishwa havina hata dira ya maendeleo, kila siku mnafanya mazoezi lakini hakuna cha maana mnachotarajia kufanya zaidi ya kupotezeana muda.  Utakuta katika kikundi  hakuna mtu mwenye taalamu ya kutayarisha tamthilia au sinema,  wote mliokuwa hapo ni sawa na wanafunzi wanatarajia kupata mwalimu wa kuwaelekeza," alisem,a Leila.
Baada ya kuachana na kikundi hicho alijikuta anajiunga na kikundi cha Alwatan cha Ilala na kubahatika  kushiriki katika sinema ya Sound of Soul. Katika sinema hiyo amecheza kama mzimu.
"Licha ya kucheza scene moja katika sinema hiyo, linaweza kuitendea haki scenem hiyo mpaka nikajikuta katika sinema nyingine iliyotengenezwa na kikundi cha Sun shine ambayo kinaongozwa na yule yule alyekuwa anaongoza kikundi cha Alwatan, alinipatia nafasi ya kubwa ya kushiriki katika Bekitatu, kusema sikumwangusha nimefanya vizuri sana. Namshukuru mungu,"alisema Laila.
Matarajio yake ni kuja kuwa mwigizaji wa maarufu wa kitaifa na kimataifa,  japokuwa wengine wanaona kama vigumu ila kwake anaamini hakuna kinachoshindikana. Kuweza kushiriki katika sinema ya Bekitatu kwa kucheza kama mshiriki mkuu,  akisaidiana na wenzake kama Hawa Hassan, Nuruti Ngeleshi, Nurdin Salum na Hassan Lukuu pamoja na wengine waliocheza kama  sapota.
Akielezea nafasi aliyocheza katika Bekitatu, amesema amecheza kama mtoto wa Nurati Ngeleshi ambaye ni Rukia,  anatokea kumchukia  mfanyakazi wao wa ndani,  Hawa Hassan aliyecheza kama Bekitatu.
Leila anadai kwamba alimchukia Bekitatu wao baada ya kugundua anatongozwa na kijana anayeitwa Ramson, yeye alitokea kumpenda huyo kijana. Hakutaka kushuhudia Ramson akiwa mpenzi wa mfanyakazi wao badala yake.
Kuanzia hapo akaanza kumfanyia vituko na visa vya aina mbali mbali huku mama yake akionyesha kama kuvutiwa na vitendo anavyofanya binti yake.
"Kusema kweli Bekitatu ni sinema nzuri sana watu wasikose kuinunua na kuiangalia, ina mafundisho mazuri kwa jamii yetu. Hata mavazi tuliyovaa ni mavazi ya heshima, hakuna mtu aliyevaa nusu uchi." amesema Leila.
Hata hivyo Leila amesema sinema hiyo imeandikwa stori na script na mtaalamu wa kuandika script zinazovutia, si mwingine ni Haji Dilunga.  Script nyingi alizoandika na kutengenezwa sinema zimetokea  kuvutia watu wengine sana. wale wanaotaka nakala ya sinema yetu wasikose kupiga namba hizi 0753 833773 au 0655 833 772.

No comments:

Post a Comment