Friday, November 28, 2014

Waigizaji vibonge wa Nigeria wanavyotesa na ubonge wao kuliko wembamba


Wakati  nigeria wasanii wa kike wenye maumbo makubwa na yakuvutia wanaongoza katika kurasa za mbele za magazeti ya udaku na majarida mbali mbali ya burudani sambamba na mitandao ya kijamii kutokana mavazi yao.  Mara nyinyi wasanii wanakuwa wanalipuka pamba za ukweli zinazoonyesha baadhi ya maungo yao yakiwa nusu. Kitendo hicho kimetokea kuwa gumzo kubwa katika miji  mbali mbali ya  nchi hiyo ,  miongoni mwa nguo wanazopenda kuvaa ni zile zinazoonyesha sehemu kubwa ya amatiti yao yakiwa wazi sambamba na mapaja yao. Wengine wanafikia mpaka kuonyesha vitovu vyao. Kwa mujibu wa  maelezo kwa nyakati tofauti wamesema si kitu cha ajabu kufanya hivyo kwani kila mmoja ana utaratibu wake wa kuvaa hasa kwenye matukio  mbali mbali cha muhimu ni kwamba hawatembei uchi wa mnyama. Kama kuna watu wanachukizwa au waandishi wanafuatilia maisha yetu, watajijua wenyewe kila ana stahili ya amaisha yake aliyochagua kuishi. Wafuatao ni miongoni mwa mastaa wanaotingisha kwa kuvaa mavazi yanawachanganya wanaume na hata wanawake wenzao, sambamba na kulalamikiwa na baadhi ya watu.
                                                                          
                                                                Ifeoma Okeke
Ni mwanamke anayejua  kuvaa kulingana na mwili wake unataka kuvalishwa nini, sio kujivalia ovyo ovyo kwa kuiga. Licha aya unene wa umbo lake bado anamvuto wa hali ya juu kutokana kupangili amvazi yake. Licha ya kuvaa nusu uchi bado anaonekana kutingisha kuvutia wanaume wengi kumtazama mara wanapobishana . Staa huyu alitamba na sinema ya Evil Genius, hata mara kwa mara amekuwa amesema hajisikii vibaya kwa jinsi anavyovaa na wala haoni ajabu au aibu. Mwanamama anakaribia kufikisha kilo mia mbili.


 
                                                                         

                                                         Chioma Toplis
                                                            
Ni mwanadada mwenye mvuto wa hali ya juu hasa namna anavyojua kumechisha mavazi yake viatu, licha kuwa bonge la mtu ni mpenzi wa viatu virefu.  Kwa mujibu wa maelezo amejikagua na kugundua  kama miezi ya karibuni uzito umekuwa ukipanda kwa kasi mpaka anashangaa. hata hivyo amesema licha kufanya maoezi bado uzito unaongezeka, ametamba na sinema ya Stolen Bible



                                                                     Eniola Badmus
Ana bonge la kitambi siku hizi na wala hajawahi kusikika akilalamika. Msanii huyo maarufu kwa jina la Gbogbo Big Girl, ni binti anayependa kujipodoa ingawa hakuna uhakika kama anajua madhara yake. Uchunguzi unaonyesha kwamba mwili wake mkubwa ndiyo umemfanya akawa maarufu zaidi kuliko kazi anazofanya.




                                                                            


                                                                    Adaora Ukoh
                                                                  
Marafiki zake wamesikika wakimuonya mara kadhaa, lakini ni kama vile anaona yuko sawa. Miezi michache iliyopita alizindua gauni kubwa alilolipa jina la Adaora akiwa anamaanisha kwamba ni nguo maalum kwa ajili ya wasichana mabonge kama yeye. Anaamini kila mwanamke ni mrembo na uzuri uko ndani na si ukubwa wa mwili japokuwa ameanza mazoezi ya gym.

                                                                                Foluka Daramola                                                                                     
Foluke Daramola anaijua kazi yake, acha apewe sifa. Lakini mashabiki wake wamekuwa wakiguna kila wanapomuona kutokana na unene wake mkubwa. "Unene au mwili wa mtu ni suala binafsi la maisha ya msichana hakuna wa kumuamulia, najua ninachopaswa kufanya," ndivyo anavyosema.

No comments:

Post a Comment