Sunday, March 1, 2015

Viatu vya kishetani, ukivaa unamsambaza kwa nguvu moja.


          

               
Ukivaa unaendelea kumtukuza na kumsambaza shetani kwa wengi,    sio kila kinachotengenezwa na wabunifu ni  lazima ukivae.  Vitu vingine vinatengenezwa kwa sababu maalumu, watengenezaji wanajua wanachofanya, hakuna anayebahatisha katika hilo. Miongoni mwa wabunifu na watengenezaji wa mitindo mbali mbali ni wafuasi wa dini ya shetani. Kuweni makini katika kuchagua aina gani ya kiatu unachotaka kuvaa. Hasa kina dada wanaongoza kwa kuwa na mitindo mingi ya viatu na nguo.  Kwa vile wabunifu wanajua kama waigizaji, wanamuziki na wanamitindo wa mavazi ni watu wanaotazamwa sana na jamii, wanawavisha viatu hivyo kwa lengo la kuvitafutia soko na umaarufu miongoni mwa jamii ili shetani aweze kuwa na nguvu. Hivi sasa viatu hivyo vimeanza kutumika sana katika sinema mbali mbali au katika baadhi ya video za wanamuziki maarufu. Wakati mwingine vimekuwa vikitumika katika majukwaa ya wanamitindo. lengo ni kusambaza nguvu za shetani. kuwa makini kama unapenda kuigi kila kitu.

Mwanamume ametumia pauni 150,000 kutaka kufanana na Kim Kardashian


                                                                           
                                                                     Jordan James

                                                                   Kim Kardashian                                                                     
                                                                   Jordan  na Kim                                                                    
                                                                         Jordan                                     


                                                               Jordan akiwa na mkoba

                                                                  Kim akiwa mkoba
Kutana na kijana Jordan James kutoka Uingereza mwenye umri wa miaka 23 ambaye ari yake maishani ni kufanana tu kama Kim Kardashian.Mvulana huyu amefanya mambo ya ajabu akijitahidi kufanana na Kim kwa kujiongeza urembo bandia, hasa kufanya midomo yake kuwa mikubwa akitaka ifanane na ya Kim.
Je unajua ametumia kiwango gani cha pesa katika harakati zake za kutaka kufanana kama Kim? Pauni 150,000 au dola laki mbili na arobaini.
Pesa hizo zote amezitumia kwa kufanyiwa upasuaji na kuongezwa urembo bandia. Cha kushangaza ni kwamba huyu ni mwanamume anayetaka kufanana kama mwanamke
Jordan James hutumia mamia ya dola kujiweka urembo bandia na kufanana na  kichekesho kwa wengi. Amekua akitazama mamia ya picha za Kim akipiga pozi kumuiga
Aliambia jarida la The Sun kwamba alianza kumuenzi Kim Kardashian mwenye umri wa miaka 33 baada ya kutazama makala ya kipindi kijulikanacho kama ''Keeping Up With The Kardashians.'' Kipindi kinachohusu Kim na Familia yake.
'ninapenda kila kitu kumhusu Kim,' aliambia The Sun. 'yeye ndiye mwanamke mrembo zaidi duniani. Ngozi yake ni nyororo, nywele zake zinapendeza yaani kila kitu kumhusu kinanipendeza. ''
Jordan amefanyiwa upasuaji kuongeza urembo bandia zaidi ya mara 50 katika juhudi zake za kutaka kufanana kama Kim, amerembeshwa midomo, ametolewa nywele kwa kutumia miale ya Laser , amewekwa Tatoo na hata kubadilisha kope zake na mengine mengi.
Lakini mabadiliko haya yote yamemgeuza sura sana Jordan na kumanya kuwa kichekesho kwa watu wengi.
''Mimi mwenyewe hucheka watu wanapojaribu kunitusi au kunikejeli, na kuniambia kwamba mimi ni kama tu plastiki, yaani kila kitu mwilini mwangu ni baandia. Lakini hio hainijalishi.'' alisema Jordan kwa mapozi yote ya kike aliyoiga toka Kim.

Friday, February 6, 2015

Mazishi ya Muna Obiekwe, na kile usichojua kuhusu maisha yake

                                                         
                                                             Marehemu Muna Obiekwe
KIFO cha mwigizaji maarufu  wa Nollwood, Muna Obiekwe kimezua gumzo kwa wapenzi na mashabiki wake, sambamba na wale  wasiokuwa mashabiki wake ila wanafuatilia tasnia ya filamu nchini Nigeria,  kuna mambo kadhaa ambayo yawezekana ulikuwa huyajui kuhusu staa huyo aliyefariki kutokana na matatizo ya figo.
Wapo watu waliosema Muna alikuwa muoga wa waandishi wa habari hakuwa tayari kujitokeza hadharani, kuomba kuchangishiwa fedha kwa  ajili ya matibabu yake.  Kwa sababu hakupenda watu kujua maisha yake binafsi.
Wengi wanasema kwamba hakutaka kuchangisha  kwa kuhofia kujishusha kutokana na umaarufu aliokuwa nao, ingekuwa aibu kwa kwake.  kwa watu watajiuliza  atashindwa vipi kujitibia mpaka atafute fedha za michango, wakati wanapatiwa malipo mazuri.
Inaelezwa kwamba Muna alikuwa akinywa pombe sana, licha ya kukatazwa na daktari kunywa pombe. Alikuwa akijihudumia mwenyewe bila msaada wa watu wengine, lakini baadaye siku za mwisho za uhai wake alipata msaada mkubwa kutoka kwa mwanamama Patience Ozokwor na Kanayo O. Kanayo.                                                              
                                                Gari iliyobeba jeneza la Muna Obiekwe
Licha ya kuwa  mtu wa kuona aibu sana kueleza matatizo ya maisha binafsi,  siku za mwisho za uhai wake aliwasiliana na muigizaji wa kike wa Nollywood, Ibinabo Fiberesima lakini hakuwa na msaada kwa sababu  alifariki siku chache baadaye.
Alijua tatizo hilo siku nyingi lakini inaelezwa kuwa alijua atalitatua kimya kimya, aliyapuuzia maumivu aliyokuwa akiyasikia. Muna alikuwa na mke na watoto wawili lakini wengi hawakujua alikuwa akifanya maisha yake siri kubwa.                                                                    
                                          Baadhi ya waigizaji wa Nigeria wakiwa katika mazishi
Habari ziko nyingi sana Nigeria baada ya msanii huyu kupoteza maisha. Wamoja wanasema kwamba alikufa kwajili ya kuendeleza pombe kwa kiasi kama inavyoojulikana alivyokuwa anaitumia. Wengine wakasema kwamba alikufa na ugonjwa wenyewe wa kifafa baada ya yeye kusema kwamba alikuwa ameishapona.
Kama inavyojulikana  Muna ameacha pengo kubwa sana Nigeria kutokana na ujuzi wa uigizaji wake. Aliwahi kuigiza katika sinema  inayoitwa  Men in Love,  sinema iliyopigiwa kelele sana Nigeria wakidai itachangia kuhamasisha ushoga.
 Inasemekana kwamba aliweza kunywa pombe kwa kiasi kikubwa , ila director akisema action anaingia kwenye scene utazani ajalewa. Hiyo ni moja ya sifa yake tofauti na wengine wakilewa hawawezi kucheza vizuri. R.I.P Muna Obiekwe.

Wednesday, February 4, 2015

Sinema ya Bekitatu yatoa watu machozi


Unaweza kuona kama hadithi ya kufikirika, lakini tukio hili limetokea katika banda la video la maeneo ya Mwanagati, wilaya ya ilala, jimbo la Ukonga. Baadhi ya watu waliokuwa wakiangalia sinema hiyo walijikuta wakitokwa na machozi.
Kwa mujibu wa maelezo ya Kijana anayeonyesha video katika banda hilo, anayejulikana kwa jina Festo amesema alichukua DVD ya BEKITATU kwa kushawishiwa na muuzaji, hakutarajia kama itatokea kuwa nzuri kiasi cha kuvutia watu.
"Wengi wameingia katika banda langu kuangalia video ya Swagga ya JB, baada ya kumaliza kuonyesha sinema ya Swagga niliweka Bekitatu yenye waigizaji wanaochipukia, baada ya kuweka katika deki, baadhi  watu walinyanyuka na kutoka nje,  ila wengine waliendelea kuangalia." alisema.Baada ya kuanza sinema na kuonekana kijana akinyata  kwenda kubaka, vijana waliokuwa wanaangalia wakaanza kupiga makelele ya kushangilia, waliotoka nje wakaanza kurudi kuangalia. Kadri sinema ilivyozidi kuendelea watu walianza kuingiwa na huruma na kuanza kusifia kama waigizaji wamejitahidi.
"Binafsi sina kawaida ya kutokwa na machozi ninapoangalia sinema za kibongo. Ila Bekitatu ni sinema ya aina yake, unapoangalia huwezi kujua nini kitakachotokea mbele, kila hatua inakuvutia kutazama.
Kama kuna wanawake makatili, Rukia ni miongoni mwao, kwa upande wa Bekitatu amecheza vizuri sana, ameweza kupokea manyanyaso kwa kiwango cha juu kiasi cha kuwafanya watazamaji kumuonea huruma na hatimaye kutokwa na machozi. Vipande vilivyonipa machungu makubwa ni pale walipompiga kwa kumchangia, chakula chake kilipotiwa katika maji machafu, chungwa lake kukanyagwa na kulazimishwa kula. Nguo yake ilivyochomwa moto, alivyonyimwa mshahara wake, kukanyagwa na kiatu. Sehemu nyingine ni watoto wa Rukia walivyokuwa wanatapatapa kwa ajili ya sumu, Bekitatu alivyokamatwa, Rukia analilia watoto wake baada ya kugundua wamekufa. Nikitaja vipande vyote nitamailiza sinema, kipande kilichowachekesha watu ni kile cha kijiweni. Hasa yule kijana mchungaji alivyokuwa akichangia maongezi na wenzake." alisema Festo.

Tuesday, February 3, 2015

Waigizaji kumi weusi wa kiume mwenye mvuto Hollywood

JE,UNAWAJUA WAIGIZAJI 10 WA KIUME WEUSI WA HOLLYWOOD WENYE MVUTO ?KAMA HUJUI ANGALIA HAPA
                                                                1. Morris Chesnut                                             
                                                             2. Taye Diggs
                                                                 3. Idrisa Elba                                                                      
                                                        4. Micharl Ealy                                                           
                                                                        
                                                          5. Shemar Moore
                                                                         
                                                                6. Will Smith

                                                                                                                                           
                                                        7 .Omar Epps                                                                    
                                                            8.Rick Fox                                                                    
                                                               9. Pooch Hall 
                                                                 10. Common

Maradhi ya kufanya manunuzi yawakumba wanawake


                                                                     
                                        Wanawake wakiwa dukani  na mifuko ya bidhaa zao
                                             Mwanamke akiwa dukani akijaribu viatu
                                             Mwanamke akiwa tayari amenunua bidhaa zake
                                       Mwanamke akiwa amechukua bidhaa zake anaondoka
                                          Mwanamke akiwa anajaribu viatu ili aweze kununua

Duniani kuna maradhi mengi sana yanayoibuka kila kikicha, hivi sasa dunia inasumbuliwa na maradhi ya kisaikolojia kuliko maradhi ya kimwili.  Hivi karibuni yamegundulika maradhi mapya  kwa wasichana na wanawake.  Maradhi hayo yanafahamika kama  shopping umegundulika aina mpya ya ugonjwa maarufu kwa wanawake wengi, Lakini hawajui yaani maradhi ya kupenda kufanya manunuzi ya nguo, viatu na mapambo. Chunguza kuanzia wasichana wa shule vyuo mpaka wamama wanao  maradhi hayo . Yaani mtu Ana nguo makabati chumba kizima viatu kibao Lakini bado anataka kuingia dukani anunue nguo mpya!  viatu vipya!  Watalaam wa maradhi ya akili wamesema shopping maradhi yanayoisumbua dunia kwa sasa, hasa kina dada na kinamama.. Tiba ya maradhi hayo ni ushauri zaidi kuliko vidonge au shindano.  Hata hivyo tafiti zinaonyesha hata baadhi ya wanaume wameanza kukumbwa na maradhi hayo, hasa wale wanaojifanya masharobaro.

Monday, February 2, 2015

Waigizaji wa kiume kumi wa Tanzania wenye mvuto kwa mashabiki

Waigizaji wa kiume kumi wa Tanzania wenye mvuto kwa  wapenzi na mashabiki wanaotazama sinema za kibongo,  listi hiyo tumeipata kutokana na kuongea na waonyeshaji wa video katika mabanda ya video.  Wakodishaji wa DVD katika maduka ya kukodisha ya jijini Dar es salaam hasa maeneo ya uswahilini kunakotizamwa sana sinema za kibongo, maduka hayo ni maarufu kama maktaba za uswahilini au uswazi.  Fuatilia listi ya mwigizaji namba moja mpaka kumi.  Muhimu kuzingatia ni listi ya blog yetu, sio mawazo ya watazamani wa nchi yote.                                                          
1. Salim Ahmed aka Gabo

                                                    
                                                                  2. King Majuto 
                                                                3. Haji Adam                                                                                                                                       
                                                                   4. Jacob Stephen aka JB
                                                                  5.Lucas Lazaro Mhuvile .ak.a Joti
                                                                          
                                                                 6. Rammy Galis
                                                               
                                                           7.  Hissani Muya  a.k.a Tino
                                                                      
                                                                 8. Abdul Mohamed a.k.a Ben Branco
                                                                                 

                                                                 9. Haji Mboto
                                                                              
                                                                  10.Musa Kitale





     

Sunday, February 1, 2015

MAZIKO YA MUNA OBIEKWE KUFANYIKA KESHO FEBRUARI 3, 201


                                                   Muna Obiekwe enzi za uhai wake

                         Moja ya sinema aliyoshiriki kucheza Muna Obiekwe

                                          Sinema nyingine aliyoshiriki kucheza Muna Obiekwe

                                             Kitu kingine alichosiriki  Muna Obiekwe


Kwa mujibu wa maelezo ya rais wa chama cha waigizaji Nigeria (AGN), Ibinabo Fiberesima ametangaza ratiba kamili ya mazishi ya mwigizaji wa Nollywood, Muna Obiekwe.  Mwigizaji huyo alifariki dunia Januari 18, 2015 baada ya kusumbuliwa na matatizo ya figo ambayo alikuwa ameyafanya siri kwa muda mrefu. Ibinabo Fiberesima amesema maziko ya Muna yanatarajia kufanyika  kesho,  Februari 3, mwaka huu katika eneo la Umudioka, Jimbo la Anambra nchini Nigeria.  wapenzi na mashabiki sambamba na waigizaji wnzake watakutana  Marsha eneo la makutano ya Surulere kisha kuelekea Uwanja wa Ojez. Mavazi yatakuwa ni tisheti nyeupe ambazo zitatolewa eneo hilo.

Mwigizaji wa Nigeria Muna Obiekwe amefariki


                                                                       
             Marehemu  Muna Obiekwe wakati wa uhai wake, wengi watamkumbuka kwa uigizaji wake
 Marehemu Muna Obiekwe akifikishwa hospital kwa ajili ya matibabu baada ya kuzidiwa na ugonjwa, hata hakuweza kupona, umauti ukamfika
Picha hii ya Marehemu Muna Obiekwe ilionekana katika kituo cha Televvisheni, kilichokuwa ionaelezea kifo chake.

HABARI kutoka Nigeria zimesema mwigizaji maarufu wa kiume wa sinema nchini humo, Muna Obiekwe, amefariki jana katika hospitali ya Festac, jijini Lagos, baada ya kusumbuliwa na ugonjwa wa figo. Vyanzo vilivyokuwa karibu na mwigizaji huyo, vinasema Muna alikuwa akipambana na matatizo ya figo ambayo alikuwa ameyafanya siri kwa muda mrefu kabla ya kumwambia rais wa chama cha waigizaji cha Nigeria (AGN), Ibinabo Fiberesima,  ambaye aliendelea kuwa karibu naye.Habari hizo zinasema kwamba tabia ya kutumia sana vileo ya mwigizaji huyo ambaye makazi yake yalikuwa katika mji wa Enugu,  inaweza isihusiane na matatizo yaliyosababisha kifo chake. Muna atakumbukwa katika baadhi ya filamu zake kama: He Lives in Me, Songs Of Sorrow, Enemies in Love, It’s Juliet or No One, Wasted Effort na zinginezo.Msanii mwenzake kutoka Nollywood, Nonso Diobi, amethibitisha kifo hicho baada ya kuwepo sintofahamu kutoka kwa baadhi ya watu waliokuwa wakiweka taarifa katika mtandao wa Twitter kuwa Muna hajafariki. Nonso amethibitisha kifo hicho baada ya kuwasiliana na rais wa chama cha waigizaji cha Nigeria (AGN), Ibinabo Fiberesima na kuwataka watu waliokuwa wakipotosha kuhusu kifo hicho kuacha mara moja.

Waigizaji wa kike kumi wa Tanzania wenye mvuto kwa mashabiki

Waigizaji wa kike kumi wa Tanzania wenye mvuto kwa  wapenzi na mashabiki wanaotazama sinema za kibongo,  listi hiyo tumeipata kutokana na kuongea na waonyeshaji wa video katika mabanda ya video.  Wakodishaji wa DVD katika maduka ya kukodisha ya jijini Dar es salaam hasa maeneo ya uswahilini kunakotizamwa sana sinema za kibongo, maduka hayo ni maarufu kama maktaba.  Fuatilia listi ya mwigizaji namba moja mpaka kumi.  Muhimu kuzingatia ni listi ya blog yetu, sio mawazo ya watazamani wa nchi yote.                                                          
Riama Ally

                                                                1. Riama Ally


                                                                  2. Shamsa Ford
                                                                                                                           
                                                                               Salma Jabu
                                                                3. Salma Jabu                                                                                                                                       
                                                                      Irene Paul
                                                                   4. Irene Paul

                                                                           
                                                                      Cathy Rupia
                                                                  5.Cathy Rupia
                                                                          
                                                                      Wellu Sengo

                                                               6. Wellu Sengo
                                                               
                                                               Elizabeth Chijumba
                                                                                  
                                                              7.Elizabeth Chijumba
                                                                      
                                                                   Hamisa Mabeto

                                                                      8. Hamisa Mabeto 
                                                                                 

                                                                 9. Jennifer Kyaka
                                                                              
                                                                         Flora Mvungi
                                                                  10. Flora Mvungi