Wednesday, February 4, 2015

Sinema ya Bekitatu yatoa watu machozi


Unaweza kuona kama hadithi ya kufikirika, lakini tukio hili limetokea katika banda la video la maeneo ya Mwanagati, wilaya ya ilala, jimbo la Ukonga. Baadhi ya watu waliokuwa wakiangalia sinema hiyo walijikuta wakitokwa na machozi.
Kwa mujibu wa maelezo ya Kijana anayeonyesha video katika banda hilo, anayejulikana kwa jina Festo amesema alichukua DVD ya BEKITATU kwa kushawishiwa na muuzaji, hakutarajia kama itatokea kuwa nzuri kiasi cha kuvutia watu.
"Wengi wameingia katika banda langu kuangalia video ya Swagga ya JB, baada ya kumaliza kuonyesha sinema ya Swagga niliweka Bekitatu yenye waigizaji wanaochipukia, baada ya kuweka katika deki, baadhi  watu walinyanyuka na kutoka nje,  ila wengine waliendelea kuangalia." alisema.Baada ya kuanza sinema na kuonekana kijana akinyata  kwenda kubaka, vijana waliokuwa wanaangalia wakaanza kupiga makelele ya kushangilia, waliotoka nje wakaanza kurudi kuangalia. Kadri sinema ilivyozidi kuendelea watu walianza kuingiwa na huruma na kuanza kusifia kama waigizaji wamejitahidi.
"Binafsi sina kawaida ya kutokwa na machozi ninapoangalia sinema za kibongo. Ila Bekitatu ni sinema ya aina yake, unapoangalia huwezi kujua nini kitakachotokea mbele, kila hatua inakuvutia kutazama.
Kama kuna wanawake makatili, Rukia ni miongoni mwao, kwa upande wa Bekitatu amecheza vizuri sana, ameweza kupokea manyanyaso kwa kiwango cha juu kiasi cha kuwafanya watazamaji kumuonea huruma na hatimaye kutokwa na machozi. Vipande vilivyonipa machungu makubwa ni pale walipompiga kwa kumchangia, chakula chake kilipotiwa katika maji machafu, chungwa lake kukanyagwa na kulazimishwa kula. Nguo yake ilivyochomwa moto, alivyonyimwa mshahara wake, kukanyagwa na kiatu. Sehemu nyingine ni watoto wa Rukia walivyokuwa wanatapatapa kwa ajili ya sumu, Bekitatu alivyokamatwa, Rukia analilia watoto wake baada ya kugundua wamekufa. Nikitaja vipande vyote nitamailiza sinema, kipande kilichowachekesha watu ni kile cha kijiweni. Hasa yule kijana mchungaji alivyokuwa akichangia maongezi na wenzake." alisema Festo.

No comments:

Post a Comment