Tuesday, February 3, 2015
Maradhi ya kufanya manunuzi yawakumba wanawake
Wanawake wakiwa dukani na mifuko ya bidhaa zao
Mwanamke akiwa dukani akijaribu viatu
Mwanamke akiwa tayari amenunua bidhaa zake
Mwanamke akiwa amechukua bidhaa zake anaondoka
Mwanamke akiwa anajaribu viatu ili aweze kununua
Duniani kuna maradhi mengi sana yanayoibuka kila kikicha, hivi sasa dunia inasumbuliwa na maradhi ya kisaikolojia kuliko maradhi ya kimwili. Hivi karibuni yamegundulika maradhi mapya kwa wasichana na wanawake. Maradhi hayo yanafahamika kama shopping umegundulika aina mpya ya ugonjwa maarufu kwa wanawake wengi, Lakini hawajui yaani maradhi ya kupenda kufanya manunuzi ya nguo, viatu na mapambo. Chunguza kuanzia wasichana wa shule vyuo mpaka wamama wanao maradhi hayo . Yaani mtu Ana nguo makabati chumba kizima viatu kibao Lakini bado anataka kuingia dukani anunue nguo mpya! viatu vipya! Watalaam wa maradhi ya akili wamesema shopping maradhi yanayoisumbua dunia kwa sasa, hasa kina dada na kinamama.. Tiba ya maradhi hayo ni ushauri zaidi kuliko vidonge au shindano. Hata hivyo tafiti zinaonyesha hata baadhi ya wanaume wameanza kukumbwa na maradhi hayo, hasa wale wanaojifanya masharobaro.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment