Saturday, July 13, 2013

Najivunia uwezo wangu wa kukata viuno- Shilole


                                                                       
                                                             Shilole katika pozi la nguvu
                                                                             Shilole

Mwanadada mrembo na mwigizaji maarufu katika tasni ya sinema za kibongo, Zuwena Mohamed a.k.a Shilole ambaye hivi sasa amejikita katika muziki, na kufanikia kutamba na kutishia waimbaji wa kike wenye uwezo, nyimbo zake zimetokea kupendwa na kufanya vizuri.
Wengi hawakutegemea kama angweza kufanya vizuri katika soko la muziki, kwani kuna baadhi ya waigizaji waliojaribu kuimba kama vile Zerishi, mwigizaji aliyetamba katika sinema ya Ngome ya Mwanamalundi.
Kwa Shilole hali imekuwa tofauti, ameweza kujipata umaarufu mkubwa na kupata maonyesho mengi.
"Ninapata maonyesho mengi kwa sababu ninapokuwa jukwaani, najituma kadri ya uwezo wangu kucheka, yaani kukata viuno. Najivunia uwezo wangu wa kukata viuno." alitamba Shilole msichana mwenye umbo la kuvutia na kuhamasisha kwa kila nguo anayovaa kwa inampendeza.
Nyimbo yake ya Paka la Baa iliyokuwa katika mtindo wa mduara, imejipata umaarufu kutokana na mashairi yake kugusa maisha ya halisi ya baadhi ya watu wenye tabia ya zisizokubali na jamii.
Kama kawaida yake anawashukuru wapenzi na mashabiki wake kwa kumkubali,pia amewataka waendelee kumpa sapoti kwa kuzikubali kazi nyingine anazotarajia kutoa hivi karibuni.
Shilole ameweza kufanikiwa kuwasisimua mashabiki wake, wanawake na wanaume kwa uwezo wake wa kuzungusha kiuno.
Zamani kabla ya Shilole  alikuwa akisifiwa Ray C kwa kuzungusha kiuno mpaka akapachikwa jina la kiuno si mfupa.




Auntie Ezekiel aibuka kwenye bongo fleva

                                                   Auntie Ezekiel katika moja ya pozi lake
                                                    Auntie Ezekiel katika  pozi jingine

Baada ya kujipatia umaarufu mkubwa katika uigizaji, mwanadada nguli katika uigizaji wa sinema za kibongo, Auntie Ezekiel ameamua kujikita katika muziki, baada ya kushirikishwa kwenye wimbo unaoitwa Movie Star wa January Joseph a.k.a January Eleven.
Kwa mujibu wa maelezo yake, Auntie Ezekiel amesema ana mambo mengi anayotaka kufanya katika muziki, ila kwa sasa hajawa tayari kuweka wazi mambo hayo. Ila anasubiri kuona namna mashabiki watakavyompokea.
"Nimeamua kuwaonyesha mashabiki na wapenzi wangu kwamba ninaweza kufanya muziki, kama nikubalika nitaamua kujiingiza moja kwa moja kwenye muziki. Ila naamini kama nitapokewa vizuri na kukubakli," alisema nyota huyo wa sinema ya Sound of death.
Kama Auntie Ezekiel ataingia moja kwa moja katika muziki, atakuwa anaungana na waigizaji wengine walioamua kujiingiza kwenye muziki kama vile Zuwena Mohamed maarufu kama Shilole, Salma Jabu maarufu kama Nisha, Flora Mvungi na Snura Mushi. 

Vyombo vya habari vilinikosea- Ini Edo

                                                                            Ini Edu
LAGOS, Nigeria
Nyota wa sinema za Nigeria anayeongoza kwa utajiri, Ini Edo amesema skendo pekee iliyowahi kumchukiza katika maisha yake ni ile iliyoandikwa na baadhi ya vyombo vya habari, ikimuhusisha na uvutaji wa dawa za kulevya.
Amesema vyombo vya habari vilimkosea kwa kuandika habari ya uzushi, habari ambayo ilinivunjia heshima yangu kwenye familia, marafiki, mashabiki na wapenzi wangu wa ndani ya Nigeria na nje.
" Skendo ile ilinipa wakati mgumu sana, ila nashukuru wapenzi na mashabiki zangu, waligundua ukweli kama sio mtumiaji wa madawa ya kulevya. Skendo ile iliandaliwa na wabaya wangu kwa lengo la kunishusha kiugizaji."
Alipoulizwa kama anavuta sigara, mwanadada mwenye mvuto wa kimapenzi, alisema amekuwa akifanya hivyo katika baadhi ya filamu alizocheza, lakini kwa kawaida si mvutaji wa sigara na hataraji kuvuta katika maisha yake.
Ini alidai mtazamo wake ni tofauti na wasichana wengine wanaodai kuzaa kunaharibu shepu ya mwanamke, amesema sio kweli. Kwa sababu mwanamke aliyeolewa, kuzaa ni jambo la lazima na kwamba anapenda kuwa na watoto
“Sihofuu kupoteza umbile langu kwa sababu ya kuzaa. Wakati utakapofika, nitaanza kuzaa. Napenda watoto. Siwezi kusubiri muda mrefu kupata watoto,”alisema mwanadada huyo mwenye umbo na sura yenye mvuto alipohojiwa hivi karibuni.
Hata hivyo, Ini amesema kama ni uzuri, alikuwa nao alipokuwa na umri mdogo. Alisema aliziona baadhi ya picha zake alipokuwa mdogo na kuvutiwa nazo kiasi cha kumfanya kutoa amani kama ni yeye.
Ini alisema hana njia yoyote anayoifanya ili aonekane mrembo zaidi ya kufanyakazi zake kwa bidii, kula vizuri, kuiweka ngozi yake katika hali nzuri na kuwa mwenye furaha muda wote.
Mwanadada huyo alisema anamshukuru Mungu kwamba maisha yake ya ndoa yanakwenda vizuri na kuongeza kuwa, kwa sasa ameamua kuacha kuigiza nafasi, ambazo zinaweza kuitia doa ndoa yake.
Alisema kamwe hajawahi kuigiza filamu za ngono na hawezi kufanya kitu kama hicho katika maisha yake yote. Alisema anapenda zaidi kuigiza filamu zinazoelezea maisha halisi ya jamii kwa vile ndizo zinazokuwa na mvuto zaidi kwa jamii.
Mwanadada huyo mwenye macho ya mwito alikataa kutaja kiasi cha pesa, ambacho amekuwa akilipwa katika uigizaji wa filamu. Hata hivyo, alikiri kwamba amekuwa akilipwa fedha nyingi.
Ini alikiri kuwa si rahisi kumudu kuwa mke wa mtu na mwigizaji. Alisema anajitahidi kadri ya uwezo wake kumudu mambo hayo mawili na kwa kiasi fulani amefanikiwa.
“Nimekuwa nikipanga mapema ni lini niwe mahali fulani na lini nisiwe mahali hapo. Siweki vitu vingi kwenye sahani moja kwa wakati mmoja kwa sababu nikifanya hivyo, nitashindwa kufanya vitu vingine wakati ninapaswa kuvifanya. Bado nafanya kila kitu ambacho mwanamke anapaswa kukifanya. Kila ninapotoka kazini, nafanyakazi ya kupika nyumbani,”alisema.
Ini, ambaye ni msomi wa shahada ya sanaa alisema iwapo asingekuwa mwigizaji, angependa kuwa mwanasheria au mwanahabari.
Hata hivyo, Ini alisema upo uwezekano pia angeweza kufanyakazi nyingine yoyote ilimradi tu awe anaipenda.
“Mimi ni mtu makini katika kila jambo. Kila kitu ninachokiseti kukifanya katika akili yangu, kama ninakipenda, lazima nikifanye,”alisema.
Hivi karibuni, Ini alizindua filamu yake mpya ya I Will Take My Chances, ambayo Ini ameielezea kuwa, ana hakika itafanya vizuri sokoni na kupendwa na mashabiki.
Ini alisema ilimchukua miezi miwili kutengeneza filamu hiyo, mwezi mmoja kwa ajili ya mazoezi na mwezi mwingine kwa ajili ya kupiga picha za filamu hiyo.
Mwanadada huyo alisema licha ya kuolewa, hafikirii kustaafu kucheza filamu kwa sasa na kwamba hakuna kinachoweza kumfanya afikie uamuzi huo.
Alisema kwake, uigizaji wa filamu hautokani na kutafuta pesa, bali mapenzi kwa kazi hiyo.
Mumewe Ini kwa sasa anaishi nchini Marekani. Lakini mwanadada huyo amesisitiza kuwa, hilo si tatizo kwao kwa sababu wamekuwa wakikutana mara kwa mara.
Katika kujiweka safi kimwili, Ini amesema siku zote amekuwa akipenda kusafisha uso wake na kuuweka safi. Alisema anapokuwa hana kazi ama tukio lolote, hatumii vipodozi kutengeneza uso wake.

Nikifa sitaki nikumbukwe kama mwigizaji- Eucharia




                                                             Eucharia Anunobi Ekwu
Lagos, Nigeria
Mwanamama nyota wa sinema za Nollywood Eucharia Anunobi Ekwu  ameachana na uchezaji wa sinema na kuamua kuokoka, kumtumikia mungu kwa muda wa maisha yake yaliyobaki hapa duniani.
Hivi karibuni  Euchari alitangaza kuachana na uigizaji na kuamua kumrudia mungu kwa kuokoka baada ya kutamba kwa sana katika sinema nyingi alizoshiriki kuigiza.
Katika mahojiano yake na kituo kimoja cha televisheni cha hapa Nigeria, Eucharia amesema  akifariki dunia akumbukwe kama aliwahi kuwa mwigizaji wa sinema.
"Ingawa nimecheza muvi nyingi kwa muda mrefu, lakini nasema wazi kwamba, nikifa nsikumbukwe kama msanii bali ni mtu wa mungu ambaye nimeamua kumtumikiakwa kipindi cha maisha yangu yote yaliyobaki duninai,"alisema mwanadada huyo mwenye mvuta wa kimapenzi na macho ya kuita.
Euchari atakumbukwa na wapenzi na mashabiki katika sinema ya Abuja Connection, sinema hiyo ameshirikiana kuigiza na wakali wengine kama Clarion Chukwura Abiola, Ngozi Ezeonu, Chidi Mokeme Enabeli Elabuwa na wengine wengi wenye majina makubwa Nigeria.
Sinema ilitungwa na Ojiofor Ezeanyaeche, script iliandikwa na Adim Williams sambamba na kuongozwa na Adim Williams mwenyewe.

Lindsay mrembo mwenye matumizi mabaya fedha


                                                                   Lindsay  Lohan
                                                                      Lindsay Lohan
New York, Marekani
Mwigizaji, Lindsay Lohan ni miongoni mwa warembo waliokuwa katika chati ya juu kwa kuvuta hisia  za wengi kutokana na muonekana wake sambamba na vituko vyake, anavyofanya kila kukicha.
Mwanadada huyo anayependa kutumia fedha vibaya kama vile ameokoa, wakati ni fedha zake alizopata kwa kufanya kazi usiku na mchana. Jarida la Forbes la mwaka jana, limeandika kwamba Lindsay ameshika namba thalethini katika orodha ya waigizaji wanaotafuta fedha ili waweze kuishi maisha mazuri.
Lindsay mwenye umri wa miaka 27  raia wa Marekani ana utajiri wa dola 11 milioni.Utajiri huo umetokana na uigizaji, uimbaji wa muziki, uanamitindo na utangazaji wa manukato.
Kutokana na matumizi yake kuwa mabaya, mwaka 2011 alijikuta akifikia hatua ya kufilisika, mahesabu ya haraka aliyofikia ili aweze kupata fedha, ni kupiga picha za utupu na kupata dola milioni moja. Baada ya kupiga picha hizo alipata fedha na kurudi tena kwenye chati ya wenye fedha.
Kwa kutaka kuonyesha jeuri ya fedha alipangisha nyumba kwa dola 10,000 kwa mwezi. Anatumia dola 800 kila wiki kwa ajili  ya kutengeneza nywele zake, alinunua gari aina porsche kwa dola 80,000.
Amekamatwa mara nyingi kuhusiana na utumiaji wa madawa ya kulevya na kuendesha gari akiwa amelewa, mwaka 2007 aliwahi kufungwa jela kwa muda wa siku tisini baada ya kupatikana na hatia ya kufanya fujo.Kutokana mwendo wa tabia zake kuwa tofauti na jamii iliyostarabika, Lindsay anapata ushauri wa kuacha kutumia dawa za kulevya.

Navuta majani- Tonto Dikeh

                                                                   Tonto Dikeh
Lagos Nigeria
Nyota wa sinema za Nollywood, Tonto Dikeh ameendelea na tabia yake ya kufanya vituko, ila kituko cha safari hii kimetokea kuwashangaza wengi waliopita mtandao na kuona amebandika picha ya bangi iliyokuwa na maneno ya kusifia kilevi hicho.
" Mimi navuta ganja, mimi navuta majani napata stimu wakati wengine wanavuta majungu," aliandika ujumbe kwenye picha hiyo bila ya kuwa na wasi wasi licha ya kilevi hicho kupigwa maarufu na serikali za nchi mbali mbali duniani.
Licha kutundika picha inayonyesha bangi na kuandika ujumbe wa kusifia, ametundika picha yake inayomuonyesha akiwa tayari amepata stimu, yaani amevuta bangi. Sura yake inaonyesha jinsi alivyokolea na kilevi hicho.

Flora Mvungi amefunga na H. Baba

Baada ya kuvuka mito, milima na mabonde hatimaye wasanii wawili wa fani tofauti, Hamisi Ramadhani a.k.a H Baba ambaye ni mwanamuziki wa miondoko ya tekeu na mwigizaji nyota wa sinema za kibongo maarufu kama Bongo Movie Flora Mvungi  weekend hii waliamua wakate vilimi vya watu wanaongea mjini na kufanikiwa kutimiza ahadi yao ya kufunga ndoa.
Wote  waliokuwa wakisema kama wawili hao hawataweza kufunga ndoa wamebaki kimya wakishindwa kuamini macho na masikio yao.
                                                            Flora akisaini hati ya ndoa
                                                                Flora akiwa katika send off yake