Thursday, October 10, 2013
Sound of Soul itakuwa mitaani hivi karibuni
Sinema ni sanaa ya maigizo kwa njia ya vitendo, inayoelimisha jamii kwa mfumo wa picha. Lengo la mtayarishaji kutengeneza sinema ni kutaka kufikisha ujumbe kwa jamii iliyotuzunguka.
Wataalamu wa sanaa ya sinema, wamebainisha kwamba sinema imegawanyika katika makundi tofauti, kuna sinema zinazohusu maisha ya mtu fulani au famila. Sinema nyingine zinahusu jamii husika, mfano sinema ya Sound of Soul, inaelezea madhara ya tamaa katika jamii yetu ya kitanzania.
Kwa mujibu wa maelezo ya msemaji wa kampuni ya Swahili World Picture, Haji Dilunga
ambaye ndiye mtunzi na mwandishi wa script hiyo, amesema kisa hicho kiliwahi
kutokea miaka ya nyuma kabla ya yeye (Dilunga) hajazaliwa, baada ya kusimulia
aliamua kutayarisha sinema ili iwe fundisho kwa wengine wenye tabia kama hiyo.
Dilunga ambaye ni mwandishi wa habari, amesema kisa hicho amekiboresha ili kiweze
kuwa na mvuto kwa watazamaji, pamoja na kuongeza matukio ya kusikitisha na
kuhuzunisha.
Amesema sinema hiyo inamzungumzia msichana Whitney, aliyekuwa na tamaa ya kutafuta
mali baada ya mali za urithi alizoachiwa na marehemu baba yake, kunyang'wa na Baba
yake mkubwa, alipokuwa na mdogo na hatimaye kufukuzwa kwenye nyumba yao pamoja na
mama yake.
Kitendo hicho kilimfanya Whitney kutafuta mali kwa udi na uvumba, ili aweze kuwa
na maisha mazuri. Kwa bahati nzuri alifanikiwa kuwa na maisha mazuri, baada ya
muda mfupi maisha mazuri yalimtumbukia nyongo.
Ni nani aliyesababisha maisha mazuri yamtumbukie nyonge, ni msichana mwingine
anayeitwa Lolita, Msichana huyu alitokea kumsumbua Whitney kupita kiasi. Nini
matokeo ya usumbufu wa Lolita kwa Whitney? Unajua kwanini alimsumbua? Jibu
utalipata baada ya kuangalia Sound of Soul.
Utamu wa sinema hiyo unakuja pale unapotaka kujua kama sio kufahamu, kilichompata
Baba yake mkubwa Whitney, baada ya kumnyang'anya mali Whitney. Alifanikiwa kutimia
mali hizo, au alizikimbia na kuchukuliwa na watu wengine? Ukibahatika kuangalia
Sound of Soul utafahamu kisa hicho cha kusisimua.
“Nadhani wale wanaofuatilia sinema ninazotengeneza, watakubaliana na mimi kwamba si bahatishi katika utunzi na uandishi wa script sambamba na kuidirect movie. Watakumbuka sinema zangu nilizoandika script na kudirect ni pamoja na Uwanja wa dhambi, I love you, Picnic, Bunge la Wachawi, Popobawa na Zindiko." Alisema Dilunga.
Sound of Soul inawataka vijana kutafuta mali au fedha kwa njia ya halali, pia wanatakiwa kufahamu kama umauti pia upo nyuma yetu. Kutafuta fedha au mali kwa njia zisizokubali na jamii yetu au muumba wetu, nikujitafutia matatizo katika maisha yako ya duniani na kesho ahera.
“Sisi ni tofauti na watengenezaji wengine wa sinema, sisi hatutengenezi sinema zenye visa vya mapenzi ya kufikirika. Tunatengeneza sinema zenye ujumbe wa visa vya kweli katika maisha ya binadamu." Alisema Dilunga.
Amesema Sinema kama uwanja wa dhambi ilivuma sana, mpaka leo bado watu wanaikumbuka. Kuna baadhi ya wapenzi wa sinema walitoka Mombasa kuja kuonana na waigizaji wa sinema ya uwanja wa dhambi.
“Hebu fikiri watu wamefunga safari toka Mombasa kuja Dar kuonana na waigizaji waliocheza uwanja wa dhambi, sio jambo la kawaida kutokea katika sanaa. Mara nyingi tumezoea kusikia na kuona watu wakitoka mikoani sio nje ya nchi." Alisema Dilunga.
Amesema Sound of Soul ni sinema nzuri inayofaa kuangalia na familia yako, kwa sababu imezingatia maadili ya kitanzania. Hakuna mwigizaji yoyote aliyevaa nguo za ajabu kama nusu uchi, unaweza kuangalia na watoto wako bila ya kujisikia vibaya.
Sinema hiyo imechezwa na Mwajuma Abdul Haji, aliyecheza kama Whitney. Fatuma Mwinchumu amecheza Mama Whitney, Jimmy Raphael amecheza kama Baba mkubwa. Nurati Ngereshi amecheza kama Lolita.
Wengine waliocheza majina ya kiuchezaji yakiwa kwenye mabano ni Zalka Athumani (Rose),Emilio John (Mganga Puchiro),Sikudhani Mkambo( Mke wa Puchiro), Clemencea Salum (Tina), Khadija Fundi(Bi Upupu), Peter Pascal (Mganga Chanuo),Apolinary Mathew(Bonzo) Abdullah Hassani (Bwino), Paul Leonard(Meneja), Amina Omary (Polisi), Paskazia Peter(Polisi), Halima(Magret),Yusuph (Polisi) na Said (Polisi)
Sound of Soul inatarajia kuingia sokoni mara baada ya kumalizika kueditiwa, kuna scene kama tatu zinafanyiwa marekebisho kwa ajili ya kuwapatia wapenzi uhondo wa aina yake.
Kwa wale vijana wanaotaka kuendeleza vipaji vyao, wanaweza kufika ukumbi wa CCM tawi la Amani siku ya jumanne, alhamisi na jumamosi saa kumi jioni. Au wanaweza kupiga simu namba 0789 904 226 au 0657 675 531.
Thursday, July 18, 2013
Mama Kanumba kama mwanae kwenye filamu ya Without Daddy.
Ben Blanco, Jamila na mwenzake katika Without Daddy
Frola Mtegeo Mama yake Marehemu KanumbaMama wa aliyekuwa mwigizaji maarufu marehemu Steven Kanumba maarufu kama Big Daddy, Frola Mtegoa ameigiza filamu katika muendelezo wa kipaji cha mwanaye baada ya kuigiza katika filamu ya Without Daddy akishirikiana na watoto waliokuwa wakiigiza na marehemu Kanumba kama Patrick na Jamila, katika filamu hiyo mama Kanumba kaigiza katika kiwango cha juu.
Kwa mujibu ya maelezo ya mkurugenzi wa kampuni ya Big Daddy Production, Irene Kaungwa amesema filamu ya Without Daddy ni kazi mwendelezo wa kazi ya marehemu Kanumba iliyotoka siku za nyuma ya Big Daddy na ni kazi ambayo imetengezwa kwa ubora wa kimataifa ikiwa sambamba na kumtambulisha mama Kanumba katika tasnia ya filamu Tanzania.
“Kampuni ya Big Daddy Production imekusudia kuleta mapinduzi makubwa katika tasnia ya filamu Tanzania, na katika kumuenzi marehemu tumemchukua mama yake na kumshiriki katika filamu hii, nadhani umeona uwezo wa mama Kanumba. Naweza kusema ameonyesha uwezo mkubwa katika uigizaji na hii ni filamu yake ya kwanza,”anasema mkurugenzi.
Irene Kaungwa amesema stori ya sinema hiyo ametunga yeye, script imeandikwa na Haji Dilunga. Waigizaji waliocheza sinema hiyo ni pamoja Abdalah Mkumbilah ‘Muhogo mchungu’, Fatuma Makongoro ‘Bi. Mwenda’ Cathy Rupia, Mayasa Mrisho, ‘Maya’, Othuman Njaidi ‘Patrick’ Wastara Juma ‘Stara’ Abdul Ahmed ‘Ben Blanco’, Patcho Mwamba na wasanii mahiri wengineo.
Uru atamba amezaliwa kwa ajili muvi za mapenzi
Uru Eke
Lagos, Nigeria
Mwigizaji wa sinema za Nigeria Uru Eke amesema anauwezo mkubwa wa kuigiza sinema za mapenzi, kwa sababu ana hisia kali za mapenzi. Hata hivyo amedai kwamba ameumbwa hivyo kuwa mkali wa kuigiza sinema za mapenzi.
"Nina uwezo mkubwa wa kuigiza aina hizo za filamu za mapenzi kwa sababu nimezaliwa nikiwa ni mtu mwenye hisia kali katika mapenzi," alisema mwigizaji huyo anayekuja juu kwa sasa na kutamba kwamba mwigizaji, Ramsey ni miongoni mwa waigizaji wa kiume wenye hisia kali katika mapenzi. Angependa kucheza naye kama angeambia kuchagua mwanaume wa kucheza naye sinema za mapenzi.
Licha ya kusema hivyo amesisitiza kwamba hisia zao za mapenzi zitakuwa katika kuigiza baada ya kuigiza hakuna kitakachoendelea.
" Najua kama Ramsey Noah ni mume wa mtu, kwa hivyo hakuna kitakachoendelea zaidi ya kuigiza na kila mtu kuendelea na shughuli zake," alisema Uru Eke aliyezaliwa London na kupata elimu ya msingi London. Elimu yake ya sekondary alipata Nigeria, baada ya kumaliza elimu ya sekondari alikwenda Uingereza kupata elimu ya chuo katika chuo cha City University.
Lagos, Nigeria
Mwigizaji wa sinema za Nigeria Uru Eke amesema anauwezo mkubwa wa kuigiza sinema za mapenzi, kwa sababu ana hisia kali za mapenzi. Hata hivyo amedai kwamba ameumbwa hivyo kuwa mkali wa kuigiza sinema za mapenzi.
"Nina uwezo mkubwa wa kuigiza aina hizo za filamu za mapenzi kwa sababu nimezaliwa nikiwa ni mtu mwenye hisia kali katika mapenzi," alisema mwigizaji huyo anayekuja juu kwa sasa na kutamba kwamba mwigizaji, Ramsey ni miongoni mwa waigizaji wa kiume wenye hisia kali katika mapenzi. Angependa kucheza naye kama angeambia kuchagua mwanaume wa kucheza naye sinema za mapenzi.
Licha ya kusema hivyo amesisitiza kwamba hisia zao za mapenzi zitakuwa katika kuigiza baada ya kuigiza hakuna kitakachoendelea.
" Najua kama Ramsey Noah ni mume wa mtu, kwa hivyo hakuna kitakachoendelea zaidi ya kuigiza na kila mtu kuendelea na shughuli zake," alisema Uru Eke aliyezaliwa London na kupata elimu ya msingi London. Elimu yake ya sekondary alipata Nigeria, baada ya kumaliza elimu ya sekondari alikwenda Uingereza kupata elimu ya chuo katika chuo cha City University.
Sura ya Van Vicker yapagawisha mademu
Van Vicker akiwa na mkewe pamoja na watoto zao
Lagos, Nigeria
Licha ya kupewa heshima kubwa ya kushiriki katika mambo mbali mbali ya kijamii ya ndani na nje ya nchini ya Ghana, mwigizaji maarufu katika anga la sinema za kiafrika. Mghana Van Vicker ametokea kuwa kivutio kikubwa kwa mademu kutokana na sura yake nzuri aliyojaaliwa na mwenyezi mungu.
Mghana ametokea kuwachengua waigizaji wenzake wa kike mpaka mashabiki wanaoangalia sinema zake.
Hata hivyo mwenyewe anadai kilichompeleka Nigeria ni kazi sio mademu. Van Vicker amefanya kweli katika sinema ya Beyonce - The President daughter.
Chioma Toplis amemaliza bifu lake na Oge Okoye
Lagos, Nigeria
Mwigizaji nyota wa Nigeria Chioma Tolips ametangaza hadharani kuwa hana tena ugomvi kama sio bifu na mwigizaji mwenzake anayejulikana kwa jina Oge Okoye. Bifu hilo lilikuwa la muda mrefu, hivi sasa ameamua kuachana na bifu na kujikita zaidi kwenye biashara zake.
Chioma alizungumza hivyo baada ya kuulizwa na mtandao mmoja wa taariza za sinema za kinaigeria, kuhusiana na bifu hilo kwani lilikuwa gumzo katika vyombo mbali mbali vya habari nchini Nigeria kwa kipindi kirefu.
Kwa mujibu wa maelezo yake Chioma amesema amewasamehe watu wote waliomfanyia mabaya, akiwemo Oge Okoye ambaye alisumbuana naye kwa muda mrefu.
" Ukweli ni kwamba siwezi kuongea chochote kuhusu Oge kwani, nimemsamehe kutoka moyoni. Tena si yeye tu hata waengine waliowahji kuniendea kinyume,"alisema Chioma mwanadada mwenye umbo kubwa la kuvutia.
Hata hivyo amedai kwamba kilichotokea ni kama darasa, yaani amejifunza kutokana na tatizo hilo, hivi anaendelea na shughuli zake.
Danny Schechter ameitangaza Tanzania kwenye Movie ya Mandela
Danny Schechter
Danny Schechter a.k.a The News Dissector kwa wale wasio mfahamu ni mtayarishaji kama sio mtengenezaji wa sinema ya Nelson Mandela – “Countdown to Freedom” na “Mandela in America” ametaka dunia kuiheshimu Tanzania kwa nafasi yake kubwa kwenye kutengeneza demokrasia Afrika Kusini.
Schechter anayefanya dokumentari ya utengenezaji wa filamu ya Long Walk to Freedom kama alivyotakiwa na Nelson Mandela mwenyewe, alisema Tanzania ilitoa ushirikiano mkubwa kukomboa mataifa mengi ya Afrika ikiwemo Afrika Kusini.
Jumapili katika Tamasha la ZIFF ilikuwa ni siku ya kuangalia Afrika Kusini kabla na baada ya Uhuru. ZIFF iliweka siku maalumu ya Afrika Kusini kutokana na maendeleo ya hali ya afya ya Nelson Mandela ambayo sasa inazungumzwa duniani kote.
Mandela ambaye katika dokumentari hiyo anaonekana akifafanua vitu mbalimbali, alielezwa na Schechter kama mtu maarufu ambaye hakutaka kuitwa mtakatifu pamoja na kwamba aliombwa kutengenezewa sanamu na kuwataka wasifanye hivyo na badala yake kusaidia ujenzi wa zahanati.
Alisema dunia inapaswa kutambua kwamba katika ukombozi wa Afrika Kusini, Tanzania ni nchi muhimu ingawa dunia inaonekana kutotambua hilo lakini wenyewe wa Afrika Kusini wanafahamu.
Alisema baada ya kuwapo na nia ya kutengeneza filamu yake, Madiba alimwandikia barua ya kumtaka kutengeneza dokumentari inayohusu utengenezaji huo kwa kuhakikisha ukweli uliopo kama unazingatiwa.
Alisema hali hiyo ilimfanya kufika Tanzania japo alishawahi kufika wakati wa harakati za ukombozi. Schechte ambaye ni mwandishi wa habari za uchunguzi, mtengeneza sinema huru, bloga na mhakiki vyombo vya habari, alisema ni vyema dunia ikatambua mchango wa Tanzania kwa ukombozi si wa Afrika Kusini, bali na mataifa mengine ya Afrika.
Alisema pamoja na utawala wa Makaburu kuzishambulia nchi zilizokuwa zinasaidia ANC kama Zimbabwe, Msumbiji, Angola na Zambia, ilishindwa kufanya hivyo kwa Tanzania ambayo licha ya kuwa na makambi ya mazoezi ya kivita, pia ilikuwa na shule za kufunza viongozi wa baadaye wa Afrika Kusini, Morogoro.
Dukumentari hiyo yenye tofauti kubwa na zile zinaozotengenezwa kwa ajili ya kuoneshwa katika televisheni, inamweleza Mandela kama mtu wa watu huku waliohojiwa wakielezea matumaini na nini kinafanyika.
Sunday, July 14, 2013
Beckham kuigiza nafasi ya James Bond
David Beckham
London, England
Mke wa aliyekuwa mwanasoka wa Klabu ya Manchester United, Victoria Beckham amependekeza jina la mumewe, David Beckham kuwa miongoni mwa majina yatakayochaguliwa kupata nafasi ya kuigiza kama James Bond katika mfululizo wa sinema za 007, zinazomtumia muhusika mkuu anayeitwa James Bond.
Mapendezo hayo yanafanyika baada ya mwigizaji, Daniel Craig anayecheza sasa kama James Bond kubwaga manyanga. Majina yaliyopendekezwa ni kucheza kama James Bond ni pamoja na Christian Bale, Henry Cavill, Tom Hardy na Idris Elba.
Victoria ana amini Beckham anaweza kuitendea haki nafasi hiyo kuliko wote waliotaja kuziba pengo la Daniel Craig anayeacha kucheza nafasi hiyo.
" Nina uhakika Beckham ni bidhaa inayouzika, kama watamtumia kucheza kama James Bond. Sinema hayo itapendwa na watu wengi sana hata wale ambao sio mashabiki wa kuangalia sinema, kwa sababu Beckham ni mtu wa watu," alisisitiza Victoria alipokuwa anaongea.
Kama watampa nafasi ya kucheza kama James Bond, Beckham atafanya vizuri, kwanza ni mwanaume mwenye mvuto. Sura yake nzuri na shepu ya umbo lake ni nzuri tofauti na wanaume. Kwa hiyo watu watapenda kumtazama.
Hata hivyo Beckham mwenyewe alipoulizwa, alisema hana uhakika kama ataweza kufanya vizuri, kwa sababu hajawahi kuigiza au kusimama mbele ya camera kuigiza.
"Sina uhakika kama nitakuwa mzuri katika kuigiza, kwa sababu sijawahi kufanya kitu kama hicho katika maisha yangu. Ila kama nitapewa nafasi naweza kufanya. Nina rafiki yangu Tom Cruise ambaye ni mwigizaji mkubwa, labda ninaweza kuwa kama yeye. Ila sijafikiria kitu kama hicho kwa sasa," alisema Beckham, wengi wanamkumbuka kwa uhodari wake uwanjani.
Subscribe to:
Posts (Atom)







