Friday, November 28, 2014

Toni Braxton kuigiza kama msagaji

         




Mkali wa  muziki wa taratibu Toni Braxton ameonyesha nia aya kujitumbukiza katika fani ya uigizaji, baada  ya mwaka jana kutangaza kustaafu mambo ya muziki kama sio kupumzika.  Amesema nafsi yake inamtuma kufanya kitu ambacho alikuwa anakipenda sana toka zamani.Kwa mujibu wa maelezo yake anataka kuigiza sinema, tena anataka kuigiza kama msagaji. "Toka zamani nilikuwa na nndoto ya kuigiza kama mwanamke msagaji, nadhani sasa ndoto yangu inaweza kutimia kwa kufanya kitu roho inapenda." aliema Toni Braxton mwenye miaka 46, amabye amewahi kunyakuwa tuzo nne za grammy.











Mkali wa Home alone Macaulay Culkin hajafa







                                                                  
                                                       Macaulay Culkin alivyokuwa mdogo
                                 Macaulay Culkin alivyokuwa sasa baada ya kutumia madawa ya kulevya
                               Macaulay Culkin alivyoanza kujitumbukiza katika madawa ya kulevya
                                                     Macaulay Culkin katika pozi la kilevi
                                                      Macaulay Culkin alivyokuwa mdogo
                                                           
Yule makali wa sinema iliyojipatia umaarufu mkubwa ya home alone , Macaulay Culkin na pia ni mwanamuziki ameibuka na kufuta tetesi zilisambaa kwamba amefariki dunia. Hivi karibuni kuliibuka tetesi za kufariki mkwake licha ya kutokuwa na ufafanuzi wa kina kuhusiana na chanzo cha kifo chake. Taarifa za kifo chake zilienea katika mitandao ya kijamii,  baada taarifa hiyo. Dodo huyo aliibuka ana kusema "Tuko kwenye ziara ya kimuziki nyinyi wajinga, hakuna aliyekufa."  Ujumbe ulikuwa na picha inayomuonyesha akiwa rafiki zake ameshika kinywaji akiburudika.

Mkenya Lupita Nyong'o kuigiza katika Americanah

 







Muigizaji nyota kutoka Kenya Lupita Nyong'o amejumuishwa katika wasanii watakaoigiza katika filamu ya AMERICANAH  inayotokana na kitabu cha mwandishi Chimamanda Ngozi Adichie. Filamu hiyo haitofautini sana na  ile sinema  ya ''12 Years a Slave'' iliyompelekea mrembo  huyo kushinda tuzo la Oscars mwezi Februari itatayarishwa  na kampuni ya PLAN B P inayomilikiwa na Mtayarishaji na muigizaji  maarufu wa filamu, Brad Pitt . Filamu hiyo mpya ya AMERICANAH inaelezea mada ya mapenzi kati ya  wapenzi  wawili wa Nigeria ambao licha ya penzi kuchanuka kati yao wanatenganishwa na maswala ya uhamiaji. Muigizaji huyo aliwaambia mashabiki wake kuwa ni heshma kubwa kwake kupewa nafasi ya kuigiza katika filamu hiyo inayotokana na kitabu cha Adichie. Kitabu hicho cha Americanah, kiachoelezea maisha ya wapenzi wawili Ifemelu na Obinze. Kitabu hicho kilishinda tuzo la ''US National Book Critics Circle Award mwaka uliyopita. Aidha kimeteuliwa kuwa moja kati ya vitabu kumi bora na jopo la 'The New York Times Book Review. Nyongo aliiambia BBC kuwa baada ya kukisoma kitabu hicho , alitamanishwa na jinsi Ifemelu na mpenzi wake Obinze,walivyostahimili majaribu mengi katika uhusiano wao . Hali ambayo inawakumba waafrika wengi ambao kutokana na tamaa ya mafanikio wanakwenda ughaibuni kutafuta ajira na wengine kwa masomo ya juu. Mbali na Americanah , Adichie anajivunia tunu ya uandishi wa vitabu vingine kama vile Purple Hibiscus na Half of a Yellow Sun, ambayo pia imefasiriwa na kuigwa katika filamu na muigizaji nyota katika 12 Years a Slave , Chiwetel Ejiofor. Nyong'o aliwavutia wapenzi wa filamu kote duniani aliposhirikiana na Ejiofor na kutwaa taji la Oscar katika 12 years a slave.
















Jeniffer Lopez kama msichana miaka 25 kumbe ana 45

                                                                      



Nadhani wengi watakuwa wanajiuliza huyu dada Jennifer Lopez kila siku anakuwa mdogo, jibu ni hapana anaendelea kuzeeka ila anajua kutunza mwili wake ndiyo maana leo anaonekana kama msichana wa miaka 25 kumbe ni  mwanamama mwenye miaka 45 na ana watoto wawili.  Hebu angalia  mastaa wetu wa kike wanavyojiachia na mabia sambamba na machips na nyama choma hatimaye wanafutuka  na kuwa kama watu wenye mimba. Huwezi kubishana na mastaa wetu  wa tano bila ya kukutana na nne wenye vitambi.  Hakina kitu kinachoharibu mrembo wa mwanamke kama kitambi.

Waigizaji wa kiafrika, Kizungu na vimbwa


                                                                




Waigizaji wengi wa Afrika wanapenda kuiga mambo ya  Ulaya na Marekani.  Kwa  vile mastaa  wengi wa Ulaya na Marekani wanapenda kutembea na vimbwa,  hivi sasa kila  anayejiona staa anatembea na kiumbe. Vipo vitu vya kuiga sio kutembea na viumbwa.  Tuwe makini  na mambo tunayoiga. Mastaa wengi wa Ulaya na Marekani  wanatafuta vimbwa kwa ajili ya kujifurahisha kimapenzi,  hayo yaliwekwa na  mwandishi mmoja wa habari za kijamii nchini Marekani, Josephine Cris aliandika mtandaoni kuwa, mchezo huo uko sehemu nyingi ulimwenguni licha ya kwamba una madhara. “Mara nyingi wanawake wengi wanatumia mbwa kujifurahisha katika mapenzi,  kwa sababu wanauwezo mkubwa kutumia ulimi kulamba kitu bila ya kuchoka. Wengi hufanya hivyo kwa siri kwani wanajua jamii itawashangaa kama watasikia taarifa zao.  Ni vitendo vinavyochukiza  sana hasa ukichukulia kwamba madhara ya kufanya mapenzi na mbwa yapo wazi. Hebu jiulize, kipi kinachoweza kukuvutia kwa mbwa hadi akupe mshawasha wa kufanya naye mapenzi, kwanza mnyama siku zote ni mchafu na anaweza kukuambukiza maradhi, sasa sijui kwa nini watu wanawatumia kimahaba,” anaeleza Josephine. Kwa upande wa waigizaji wa Afrika, hatujui kama wanahusika au ni kuiga bila ya kujua wanachoiga. Tuwe makini na vyakuiga sio kila kitu tunaiga.

Maajabu makubwa, binti amefunga ndoa na mbwa

.
                                                         Kufundoa na mbwa

Binti amefunga ndoa  na mbwa kwa ajili ya kuondoa mikosi na majanga  ya kimaisha, harusi hiyo imefanyika hadharani bila ya kuficho chochote. Wazazi wa mwanamke wafurahia kama vile binti yao ameolewa na mtoto wa tajiri namba moja duniani. Hebu niambie duniani inaelekea wapi?  Tutafakari na kumrudia mungu  wangu kwa kufanya ibada ya kweli na sio ibada za kinafiki. Hatuwezi kujua lini duniani itafika mwisho kama vitabu vya dini vinavyosema.

Chike Ike akitesa Dubai kwa raha zake, Mambo ya fedha








                                                             Chike Ike kwenye boti
                                                           Chike Ike akiburudika na kahawa
                                                          Chike Ike akipata mchana mwema
                                                               wakiwa ndani bori
                                                    Chike akiwa kwenye fukwe
                                                           Chike akiwa kwe boti


Marehemu Marijani Rajabu aliyekuwa  mwanamuzki wa Dar Intenatinal aliwahi kuimba pesa ni sabuni ya roho. Mwenye pesa akifika watu wote wanasimama kila analosema watu wanalipa uzito hata kama ni wazo la kijinga.  Ndiyo ilivyokuwa kwa muigizaji wa Nigeria, Chika Ike akitumia fedha anavyotaka katika  fukwe ya jiji  Dubai ambapo unaambiwa alikodi  boat kwa dola elfu 24,000 kwa muda wa siku mbili tu,  na kila alilosema alisikilizwa na lilitekelezwa kwa kasi ya ajabu.  PESA ni  mfalme wa dunia,  ukibisha wewe bisha lakini ndio ukweli wenyewe.