Tuesday, September 27, 2016

MWAJUMA AU MAIMUNA amefariki dunia


Huwezi kuamini lakini ndio hivyo imetokea, jumapili ya tarehe 28 mwezi wa nane, ni siku tuliyompoteza msanii mkongwe Mwajuma Abdul maarufu kwa jina la MAIMUNA. Akazikwa jumatatu tarehe 29 saa kumi katika makaburi ya kisarawe. kwa wale wanaofuatilia matangazo ya redio watamkumbuka kwa tangazo la HII SASA SIFAAA, NA LEO TENA NYAMAAA, ni miongoni mwa matangazo kati ya mengi aliyocheza. Katika televisheni anakumbukwa kwa matangazo mengi aliyofanya ila kwa haraka tangazo la kifua kikuu akiwa na Kaboba, Onyango na wengine. Baadhi watamkumbuka kwa michezo ya redio, hasa mchezo wa TWENDE NA WAKATI uliokuwa ukirushwa na redio Tanzania kwa sasa TBC. Kwa upande wa sinema ameshiriki sinema nyingi baadhi Ni UWANJA WA DHAMBI. Jina la MAIMUNA alilipata baada ya kushirikia katika sinema ya UWANJA WA DHAMBI, sinema iliyompatia umaarufu mkubwa. Baadhi ya sinema alizoshiriki ni pamoja na I LOVE YOU, LAZIMA UFE JORAM, PICNIC, BUNGE LA WACHAWI, POPOBAWA, ZINDIKO, BOSS nk. Pia aliwahi kushiriki tamthilia ya HUKUMU YA TUNU akitumia jina la TUNDA. Amefariki akiwa tayari amecheza sinema inayoendelea kueditiwa pamoja na Tamthilia inayoendelea kueditiwa. Amefariki ghafla hakuwa na maradhi yoyote, alikuwa mzima wa afya njema. Mpaka saa mbili usiku alikuwa mzima wa afya katika sherehe ya kitchen part ya ndugu yake, Ghafla alijisikia kuishiwa na nguvu na kuanza kutapika, hali hiyo iliendelea mpaka alivyokimbizwa Amani Hospital, hatimaye akafariki dunia muda mfupi.Inna Lillahi wa inna ilaihi raji'un

Sunday, March 1, 2015

Viatu vya kishetani, ukivaa unamsambaza kwa nguvu moja.


          

               
Ukivaa unaendelea kumtukuza na kumsambaza shetani kwa wengi,    sio kila kinachotengenezwa na wabunifu ni  lazima ukivae.  Vitu vingine vinatengenezwa kwa sababu maalumu, watengenezaji wanajua wanachofanya, hakuna anayebahatisha katika hilo. Miongoni mwa wabunifu na watengenezaji wa mitindo mbali mbali ni wafuasi wa dini ya shetani. Kuweni makini katika kuchagua aina gani ya kiatu unachotaka kuvaa. Hasa kina dada wanaongoza kwa kuwa na mitindo mingi ya viatu na nguo.  Kwa vile wabunifu wanajua kama waigizaji, wanamuziki na wanamitindo wa mavazi ni watu wanaotazamwa sana na jamii, wanawavisha viatu hivyo kwa lengo la kuvitafutia soko na umaarufu miongoni mwa jamii ili shetani aweze kuwa na nguvu. Hivi sasa viatu hivyo vimeanza kutumika sana katika sinema mbali mbali au katika baadhi ya video za wanamuziki maarufu. Wakati mwingine vimekuwa vikitumika katika majukwaa ya wanamitindo. lengo ni kusambaza nguvu za shetani. kuwa makini kama unapenda kuigi kila kitu.

Mwanamume ametumia pauni 150,000 kutaka kufanana na Kim Kardashian


                                                                           
                                                                     Jordan James

                                                                   Kim Kardashian                                                                     
                                                                   Jordan  na Kim                                                                    
                                                                         Jordan                                     


                                                               Jordan akiwa na mkoba

                                                                  Kim akiwa mkoba
Kutana na kijana Jordan James kutoka Uingereza mwenye umri wa miaka 23 ambaye ari yake maishani ni kufanana tu kama Kim Kardashian.Mvulana huyu amefanya mambo ya ajabu akijitahidi kufanana na Kim kwa kujiongeza urembo bandia, hasa kufanya midomo yake kuwa mikubwa akitaka ifanane na ya Kim.
Je unajua ametumia kiwango gani cha pesa katika harakati zake za kutaka kufanana kama Kim? Pauni 150,000 au dola laki mbili na arobaini.
Pesa hizo zote amezitumia kwa kufanyiwa upasuaji na kuongezwa urembo bandia. Cha kushangaza ni kwamba huyu ni mwanamume anayetaka kufanana kama mwanamke
Jordan James hutumia mamia ya dola kujiweka urembo bandia na kufanana na  kichekesho kwa wengi. Amekua akitazama mamia ya picha za Kim akipiga pozi kumuiga
Aliambia jarida la The Sun kwamba alianza kumuenzi Kim Kardashian mwenye umri wa miaka 33 baada ya kutazama makala ya kipindi kijulikanacho kama ''Keeping Up With The Kardashians.'' Kipindi kinachohusu Kim na Familia yake.
'ninapenda kila kitu kumhusu Kim,' aliambia The Sun. 'yeye ndiye mwanamke mrembo zaidi duniani. Ngozi yake ni nyororo, nywele zake zinapendeza yaani kila kitu kumhusu kinanipendeza. ''
Jordan amefanyiwa upasuaji kuongeza urembo bandia zaidi ya mara 50 katika juhudi zake za kutaka kufanana kama Kim, amerembeshwa midomo, ametolewa nywele kwa kutumia miale ya Laser , amewekwa Tatoo na hata kubadilisha kope zake na mengine mengi.
Lakini mabadiliko haya yote yamemgeuza sura sana Jordan na kumanya kuwa kichekesho kwa watu wengi.
''Mimi mwenyewe hucheka watu wanapojaribu kunitusi au kunikejeli, na kuniambia kwamba mimi ni kama tu plastiki, yaani kila kitu mwilini mwangu ni baandia. Lakini hio hainijalishi.'' alisema Jordan kwa mapozi yote ya kike aliyoiga toka Kim.

Friday, February 6, 2015

Mazishi ya Muna Obiekwe, na kile usichojua kuhusu maisha yake

                                                         
                                                             Marehemu Muna Obiekwe
KIFO cha mwigizaji maarufu  wa Nollwood, Muna Obiekwe kimezua gumzo kwa wapenzi na mashabiki wake, sambamba na wale  wasiokuwa mashabiki wake ila wanafuatilia tasnia ya filamu nchini Nigeria,  kuna mambo kadhaa ambayo yawezekana ulikuwa huyajui kuhusu staa huyo aliyefariki kutokana na matatizo ya figo.
Wapo watu waliosema Muna alikuwa muoga wa waandishi wa habari hakuwa tayari kujitokeza hadharani, kuomba kuchangishiwa fedha kwa  ajili ya matibabu yake.  Kwa sababu hakupenda watu kujua maisha yake binafsi.
Wengi wanasema kwamba hakutaka kuchangisha  kwa kuhofia kujishusha kutokana na umaarufu aliokuwa nao, ingekuwa aibu kwa kwake.  kwa watu watajiuliza  atashindwa vipi kujitibia mpaka atafute fedha za michango, wakati wanapatiwa malipo mazuri.
Inaelezwa kwamba Muna alikuwa akinywa pombe sana, licha ya kukatazwa na daktari kunywa pombe. Alikuwa akijihudumia mwenyewe bila msaada wa watu wengine, lakini baadaye siku za mwisho za uhai wake alipata msaada mkubwa kutoka kwa mwanamama Patience Ozokwor na Kanayo O. Kanayo.                                                              
                                                Gari iliyobeba jeneza la Muna Obiekwe
Licha ya kuwa  mtu wa kuona aibu sana kueleza matatizo ya maisha binafsi,  siku za mwisho za uhai wake aliwasiliana na muigizaji wa kike wa Nollywood, Ibinabo Fiberesima lakini hakuwa na msaada kwa sababu  alifariki siku chache baadaye.
Alijua tatizo hilo siku nyingi lakini inaelezwa kuwa alijua atalitatua kimya kimya, aliyapuuzia maumivu aliyokuwa akiyasikia. Muna alikuwa na mke na watoto wawili lakini wengi hawakujua alikuwa akifanya maisha yake siri kubwa.                                                                    
                                          Baadhi ya waigizaji wa Nigeria wakiwa katika mazishi
Habari ziko nyingi sana Nigeria baada ya msanii huyu kupoteza maisha. Wamoja wanasema kwamba alikufa kwajili ya kuendeleza pombe kwa kiasi kama inavyoojulikana alivyokuwa anaitumia. Wengine wakasema kwamba alikufa na ugonjwa wenyewe wa kifafa baada ya yeye kusema kwamba alikuwa ameishapona.
Kama inavyojulikana  Muna ameacha pengo kubwa sana Nigeria kutokana na ujuzi wa uigizaji wake. Aliwahi kuigiza katika sinema  inayoitwa  Men in Love,  sinema iliyopigiwa kelele sana Nigeria wakidai itachangia kuhamasisha ushoga.
 Inasemekana kwamba aliweza kunywa pombe kwa kiasi kikubwa , ila director akisema action anaingia kwenye scene utazani ajalewa. Hiyo ni moja ya sifa yake tofauti na wengine wakilewa hawawezi kucheza vizuri. R.I.P Muna Obiekwe.

Wednesday, February 4, 2015

Sinema ya Bekitatu yatoa watu machozi


Unaweza kuona kama hadithi ya kufikirika, lakini tukio hili limetokea katika banda la video la maeneo ya Mwanagati, wilaya ya ilala, jimbo la Ukonga. Baadhi ya watu waliokuwa wakiangalia sinema hiyo walijikuta wakitokwa na machozi.
Kwa mujibu wa maelezo ya Kijana anayeonyesha video katika banda hilo, anayejulikana kwa jina Festo amesema alichukua DVD ya BEKITATU kwa kushawishiwa na muuzaji, hakutarajia kama itatokea kuwa nzuri kiasi cha kuvutia watu.
"Wengi wameingia katika banda langu kuangalia video ya Swagga ya JB, baada ya kumaliza kuonyesha sinema ya Swagga niliweka Bekitatu yenye waigizaji wanaochipukia, baada ya kuweka katika deki, baadhi  watu walinyanyuka na kutoka nje,  ila wengine waliendelea kuangalia." alisema.Baada ya kuanza sinema na kuonekana kijana akinyata  kwenda kubaka, vijana waliokuwa wanaangalia wakaanza kupiga makelele ya kushangilia, waliotoka nje wakaanza kurudi kuangalia. Kadri sinema ilivyozidi kuendelea watu walianza kuingiwa na huruma na kuanza kusifia kama waigizaji wamejitahidi.
"Binafsi sina kawaida ya kutokwa na machozi ninapoangalia sinema za kibongo. Ila Bekitatu ni sinema ya aina yake, unapoangalia huwezi kujua nini kitakachotokea mbele, kila hatua inakuvutia kutazama.
Kama kuna wanawake makatili, Rukia ni miongoni mwao, kwa upande wa Bekitatu amecheza vizuri sana, ameweza kupokea manyanyaso kwa kiwango cha juu kiasi cha kuwafanya watazamaji kumuonea huruma na hatimaye kutokwa na machozi. Vipande vilivyonipa machungu makubwa ni pale walipompiga kwa kumchangia, chakula chake kilipotiwa katika maji machafu, chungwa lake kukanyagwa na kulazimishwa kula. Nguo yake ilivyochomwa moto, alivyonyimwa mshahara wake, kukanyagwa na kiatu. Sehemu nyingine ni watoto wa Rukia walivyokuwa wanatapatapa kwa ajili ya sumu, Bekitatu alivyokamatwa, Rukia analilia watoto wake baada ya kugundua wamekufa. Nikitaja vipande vyote nitamailiza sinema, kipande kilichowachekesha watu ni kile cha kijiweni. Hasa yule kijana mchungaji alivyokuwa akichangia maongezi na wenzake." alisema Festo.

Tuesday, February 3, 2015

Waigizaji kumi weusi wa kiume mwenye mvuto Hollywood

JE,UNAWAJUA WAIGIZAJI 10 WA KIUME WEUSI WA HOLLYWOOD WENYE MVUTO ?KAMA HUJUI ANGALIA HAPA
                                                                1. Morris Chesnut                                             
                                                             2. Taye Diggs
                                                                 3. Idrisa Elba                                                                      
                                                        4. Micharl Ealy                                                           
                                                                        
                                                          5. Shemar Moore
                                                                         
                                                                6. Will Smith

                                                                                                                                           
                                                        7 .Omar Epps                                                                    
                                                            8.Rick Fox                                                                    
                                                               9. Pooch Hall 
                                                                 10. Common

Maradhi ya kufanya manunuzi yawakumba wanawake


                                                                     
                                        Wanawake wakiwa dukani  na mifuko ya bidhaa zao
                                             Mwanamke akiwa dukani akijaribu viatu
                                             Mwanamke akiwa tayari amenunua bidhaa zake
                                       Mwanamke akiwa amechukua bidhaa zake anaondoka
                                          Mwanamke akiwa anajaribu viatu ili aweze kununua

Duniani kuna maradhi mengi sana yanayoibuka kila kikicha, hivi sasa dunia inasumbuliwa na maradhi ya kisaikolojia kuliko maradhi ya kimwili.  Hivi karibuni yamegundulika maradhi mapya  kwa wasichana na wanawake.  Maradhi hayo yanafahamika kama  shopping umegundulika aina mpya ya ugonjwa maarufu kwa wanawake wengi, Lakini hawajui yaani maradhi ya kupenda kufanya manunuzi ya nguo, viatu na mapambo. Chunguza kuanzia wasichana wa shule vyuo mpaka wamama wanao  maradhi hayo . Yaani mtu Ana nguo makabati chumba kizima viatu kibao Lakini bado anataka kuingia dukani anunue nguo mpya!  viatu vipya!  Watalaam wa maradhi ya akili wamesema shopping maradhi yanayoisumbua dunia kwa sasa, hasa kina dada na kinamama.. Tiba ya maradhi hayo ni ushauri zaidi kuliko vidonge au shindano.  Hata hivyo tafiti zinaonyesha hata baadhi ya wanaume wameanza kukumbwa na maradhi hayo, hasa wale wanaojifanya masharobaro.