Mwaila na wenzake katika sinema ya Zungu la Unga
Kampuni ya kutayarisha
sinema na usambazaji ya What Ever Film imepania kunyanyua waigizaji chipukizi
kwa kuwashirikisha katika sinema watakazotayarisha hivi karibuni.
Akizungumza na gazeti hili,
Mkurugenzi wa kampuni hiyo Hussein Mwaila amesema mbali wa kuwashirikisha
katika sinema zao, pia watasambaza sinema za waigizaji chipukizi
walizotayarisha wenyewe.
" Tunapokea sinema za
watayarishaji chipukizi na kuzisambaza, vigezo vyetu ni sinema kuwa nzuri.
Yaani stori ieleweke, waigizaji wacheze kwa uhalisi wa hali ya juu sambamba na
ubora wa rangi na sauti. Ikifanikiwa vigezo hivyo tunaichukua na kuisambaza."
Alisema Mwaila.
Hata hivyo amesikitishwa na
baadhi ya makampuni yanayokataa sinema za waigizaji chipukizi kwa madai kwamba
haziuzi, kitu ambacho si kweli.
" Unajua kuna baadhi ya
makampuni hayataki kuona vijana wapya wanachipukia kwa kuhofia mastaa wao waliongia
nao mikataba wanaweza kufunikwa na waigizaji wanaochipukia. Hiyo ndiyo sababu
ya kudai sinema walizocheza chipukizi haziuzi." Alisema Mwaila.
Alitoa mfano wa sinema ya
kisiwa cha wachawi iliyochezwa na waigizaji chipukizi, inafanya vizuri sokoni mpaka
sasa. Wakati zile sinema zilizochezwa na mastaa zinafanya vibaya.
Ukitaka kupata uthibitisho
wa hiki ninachokueleza pita kwenye mabanda ya video, utagundua ukweli wa hiki
ninachokueleza. Sinema nyingi za mastaa zinapowekwa watazamaji wanazomea na kutaka
zitolewe, ila zinapowekwa sinema za waigizaji wanaochipukia wanashangilia
kuzifurahia.
Kwa utafiti mdogo kama huo
unaweza kupata taswira ya ukweli wa madai ya baadhi ya makampuni kwamba sinema
za waigizaji wanaochipukia haziuzi.
Mwaila amesema What Ever
Film watahakikisha dhana hiyo wanaitokomeza kwa wasambazaji wa jumla na
rejareja kwa ajili ya kuwasaidia waigizaji chipukizi.
No comments:
Post a Comment