Tuesday, March 26, 2013

Wema anawaongoza waigizaji wa kike

Baadhi ya wadau wa sinema wamesikika wakisema Wema Sepetu ni miongoni mwa waigizaji wanaopenda kuvaa viatu virefu kwa muda mrefu kuliko waigizaji wote wa kike. Mabishano hayo yalitokea kwenye baa moja maarufu wakati wakiangalia sinema ya DJ BEN iliyochezwa na Jacob Stephen, Irene Uwoya na Wema Sepetu. Jamaa mmoja iliyoonekana kulewa ilisikika ikiongea kwa sauti, Wema anaongoza kwa kuvaa viatu virefu. Kila utakapomuona iwe kwenye televisheni, magazeti au mtaani utamuona amevaa kiatu kirefu tofauti na waigizaji wenzake wa kike. “ Ni kweli Wema anapenda kuvaa viatu virefu, ila atakuja kulia uzeeni. Miguu itamsumbua sana." alidai mwanamke mmoja aliyekuwa akipata ulabu katika baa hiyo. “ Wema anaongoza wenzake, wapili nani na mwisho ni nani?" Aliuliza Mzee mmoja wa makamu huku akicheka kilevi. “ Wa pili Lulu," Mlevi mwingine alijibu.“ Sio Lulu, yule mke wa Ndikumana." mwingine alijibu. “ Anaitwa Irene Uwoya." Alijibu huyo Mwanamke. Shangazi Ezekiel akimanisha Auntie Ezekiel na Mrs Dallas akimanisha Jaquline Wolper mbona mmewasahau?" Yule Mzee wa makamu aliuliza. Jamaa aliyeanzisha mada hiyo alidai wiki ijayo wakikutana hapo atawatajia wa pili na mwisho. Swahilicinemanews tunakubalina na wadau kama mwanamke akivaa kiatu kirefu anapendeza. Kazi kwenu waigizaji wa kike kutinga viatu virefu kwa ajili ya kuvutia machoni mwa mashabiki wenu.

No comments:

Post a Comment