Tuesday, March 26, 2013

Wema amnusuru Kajara kwenda Jela

HUKUMU ya kesi iliyokuwa inamkabili staa wa filamu za Kibongo, Kajala Masanja na mumewe imetolewa na Hakimu Sundi Fimbo katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, jijini Dar. Katika hukumu hiyo Kajala amehukumiwa kwenda jela miaka mitano au kulipa faini ya shilingi milioni 13 na mumewe kwenda jela miaka mitano au kulipa faini ya shilingi milioni 213. Kajala alikuwa anakabiliwa na kesi ya kuuza nyumba iliyowekwa kizuizini na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) baada ya mumewe, Faraji Agustino kukumbwa na msala wa kutaka kujipatia fedha haramu. Hata hivyo msanii Wema Sepetu amemwokoa Kajala kwa kumlipia faini ya shilingi milioni 13 ili kumnusuru na kifungo cha kwenda jela

No comments:

Post a Comment