Tuesday, March 26, 2013

Waigizaji walia na serikali

Waigizaji wa sinema nchini, wametoa kilio chao kwa kuitaka serikali kuwasaidia kupata vitendea kazi ili kuleta uhalisi katika sinema zao na kutoa ushindani katika soko la kimataifa. Wamedai hivi sasa sinema zinapoteza uhalisi kwa sababu ya kukosa sehemu husika za kuigiza, mfano hai ni kukosekana kwa mavazi ya halisi ya Polisi, Jeshi, Trafik na Askari magereza, kuna changia sinema kupotea uhalisi. Mahitaji wanayotaka serikali kuwasaidia kuweza kupata kirahisi ni pamoja na mavazi ya askari wa aina zote, kutumia vituo vya polisi, majengo ya mahakama, bastola na bunduki, bendera, majengo ya hospital za serikali sambamba na majengo na maofisi ya serikali. Wameitaka serikali kuweka utaraibu wa kuwakodisha waigizaji ili kuweza kufanya maigizo yao katika ubora na uhalisi tofauti na hivi sasa.

No comments:

Post a Comment