Friday, March 29, 2013

Teknolojia yapunguza kasi ya soko la sinama

Kukua kwa teknolojia kumechangia kwa kiasi kikubwa kupunguza kasi ya usambazaji wa kazi za sinema. Ikilinganishwa na zamani kabla ya Tanzania kukua katika teknolojia. Kwa mujibu wa maelezo ya Abdalah Shaban anayemiliki duka la jumla la kuuza VCD, DVD, VCD na CD, amesema kasi ya kununua TAPE, DVD, VCD au CD za muziki na sinema kama ilivyokuwa zamani imepungua sana. Shaban amesema hivi sasa watu wengi wanaweka sinema na nyimbo kwenye flash Disc. Kwa mfumo huo umuhimu wa TAPE, DVD, VCD na CD hakuna tena, hivi sasa TAPE zimeshaanza kupotea katika soko la muziki kama zilivyopotea VHS. “Nakaa dukani toka asubuhi mpaka jioni, nauza CD hamsini. Zamani nilikuwa nauza VCD elfu tatu mpaka tano. DVD elfu sita mpaka kumi. Wateja wengi wanaoingia dukani kwangu hivi sasa wanaulizia memory card na flash disc." Alisema Shaban. Majumbani kumejaa deki zenye kutumia memory card na flash disc Kwa mfumo huo hakuna mtu atakayenunua DVD, VCD na CD. Shaban amesema hatuwezi kukataa maendeleo ya kupanuka kwa teknolojia, ila tunatakiwa kuandaa mazingira ya kutumia teknolojia hiyo bila ya watu wengine kuumia. Hivi sasa wanaoumia na kuteseka na njaa ni wanamuziki na waigizaji, wanaofaidika ni wale wafanyabishara, wanaokaa vibarazani na Computer wakiweka nyimbo na sinema kwenye flash disc na memory card bila ya ridhaa ya waigizaji na wanamuziki wenyewe. Shaban anasema memory card na flash disc ziendelea kuingia nchini kwa sababu zina matumizi mengi zaidi ya kuweka nyimbo na sinema. Ila wangepiga maarufu uingiaji wa deki na redio zinazotumia memory card na flash disc. Wakifanya hivyo soko la DVD, VCD, CD linaweza kurudi kama mwanzo. Vinginevyo wasambazaji wa muziki na wauzaji wa jumla na rejareja wataacha na kuanzisha biashara nyingine zenye wateja.

No comments:

Post a Comment