Friday, March 29, 2013

Wema na Jaquliane mfano wa kuigwa

Aliyewahi kuwa Miss Tanzania na mwigizaji maarufu nchini, Wema Sepetu amefanya tukio la kistarabu baada ya kumsaidia mwigizaji mwenzake Kajala Masanja kwenda jela kutumikia kifungo cha miaka mitano baada ya kumlipia milioni kumi na tatu. Kwa mujibu wa hukumu ya hakimu Sundi Fimbo wa mahakama ya hakimu mkazi Kisutu, jijini Dar es Salaam. Alimuhukumu Kajala kwenda jela miaka mitano au kulipa faini ya milioni kumi na tatu za kitanzania. Wema alijitokeza kulipa faini hiyo, Kajala akajikuta akiwa uraiani akiwa huru. Mumewe alikosa mtu wa kumlipia faini alikuja akienda jela kutumikia kifungo. Kitendo alichofanya Wema Sepetu kinafanana na kile alichofanya mwigizaji mwingine maarufu anayeitwa Jaquline Wolper kwa kutoa kiasi kikubwa fedha kusaidia matibabu ya marehemu Sajuki. Waigizaji hawa ni mfano mzuri wa kuigwa, licha ya mapungufu yao. Kila binadamu ana mapungufu yake, cha muhimu kujiuliza yale mapungufu yao yanawaumiza wengine. Kama jibu hapana hatuna haki ya kuwasakama. Tunatakiwa kuwapa moyo ili waweze kuendelea kusaidia wenzao, kutoa msaada sio suala la kuwa na fedha nyingi. Wapo watu wana fedha nyingi sana lakini hawatowi msaada kwa mtu yoyote. Tukubali tusikubali Wema na Jaquliane ni mfano wa kuigwa. mnyonge mnyongeni haki yake mpeni. Wema na Jaquliane wanastahili pongezi. Kama kweli walichofanya Wema na Jaquliane ni kitu cha kawaida, hawastahili kupongezwa. Mbona hatujaona kampuni yoyote ya usambazaji wa sinema kutoa kiasi kikubwa cha fedha kama hicho kuwasaidia wahusika. Wakati wao wana fedha nyingi kuliko Wema na Jaquliane, swali kwenu.

No comments:

Post a Comment