Friday, November 28, 2014

Jeniffer Lopez kama msichana miaka 25 kumbe ana 45

                                                                      



Nadhani wengi watakuwa wanajiuliza huyu dada Jennifer Lopez kila siku anakuwa mdogo, jibu ni hapana anaendelea kuzeeka ila anajua kutunza mwili wake ndiyo maana leo anaonekana kama msichana wa miaka 25 kumbe ni  mwanamama mwenye miaka 45 na ana watoto wawili.  Hebu angalia  mastaa wetu wa kike wanavyojiachia na mabia sambamba na machips na nyama choma hatimaye wanafutuka  na kuwa kama watu wenye mimba. Huwezi kubishana na mastaa wetu  wa tano bila ya kukutana na nne wenye vitambi.  Hakina kitu kinachoharibu mrembo wa mwanamke kama kitambi.

Waigizaji wa kiafrika, Kizungu na vimbwa


                                                                




Waigizaji wengi wa Afrika wanapenda kuiga mambo ya  Ulaya na Marekani.  Kwa  vile mastaa  wengi wa Ulaya na Marekani wanapenda kutembea na vimbwa,  hivi sasa kila  anayejiona staa anatembea na kiumbe. Vipo vitu vya kuiga sio kutembea na viumbwa.  Tuwe makini  na mambo tunayoiga. Mastaa wengi wa Ulaya na Marekani  wanatafuta vimbwa kwa ajili ya kujifurahisha kimapenzi,  hayo yaliwekwa na  mwandishi mmoja wa habari za kijamii nchini Marekani, Josephine Cris aliandika mtandaoni kuwa, mchezo huo uko sehemu nyingi ulimwenguni licha ya kwamba una madhara. “Mara nyingi wanawake wengi wanatumia mbwa kujifurahisha katika mapenzi,  kwa sababu wanauwezo mkubwa kutumia ulimi kulamba kitu bila ya kuchoka. Wengi hufanya hivyo kwa siri kwani wanajua jamii itawashangaa kama watasikia taarifa zao.  Ni vitendo vinavyochukiza  sana hasa ukichukulia kwamba madhara ya kufanya mapenzi na mbwa yapo wazi. Hebu jiulize, kipi kinachoweza kukuvutia kwa mbwa hadi akupe mshawasha wa kufanya naye mapenzi, kwanza mnyama siku zote ni mchafu na anaweza kukuambukiza maradhi, sasa sijui kwa nini watu wanawatumia kimahaba,” anaeleza Josephine. Kwa upande wa waigizaji wa Afrika, hatujui kama wanahusika au ni kuiga bila ya kujua wanachoiga. Tuwe makini na vyakuiga sio kila kitu tunaiga.

Maajabu makubwa, binti amefunga ndoa na mbwa

.
                                                         Kufundoa na mbwa

Binti amefunga ndoa  na mbwa kwa ajili ya kuondoa mikosi na majanga  ya kimaisha, harusi hiyo imefanyika hadharani bila ya kuficho chochote. Wazazi wa mwanamke wafurahia kama vile binti yao ameolewa na mtoto wa tajiri namba moja duniani. Hebu niambie duniani inaelekea wapi?  Tutafakari na kumrudia mungu  wangu kwa kufanya ibada ya kweli na sio ibada za kinafiki. Hatuwezi kujua lini duniani itafika mwisho kama vitabu vya dini vinavyosema.

Chike Ike akitesa Dubai kwa raha zake, Mambo ya fedha








                                                             Chike Ike kwenye boti
                                                           Chike Ike akiburudika na kahawa
                                                          Chike Ike akipata mchana mwema
                                                               wakiwa ndani bori
                                                    Chike akiwa kwenye fukwe
                                                           Chike akiwa kwe boti


Marehemu Marijani Rajabu aliyekuwa  mwanamuzki wa Dar Intenatinal aliwahi kuimba pesa ni sabuni ya roho. Mwenye pesa akifika watu wote wanasimama kila analosema watu wanalipa uzito hata kama ni wazo la kijinga.  Ndiyo ilivyokuwa kwa muigizaji wa Nigeria, Chika Ike akitumia fedha anavyotaka katika  fukwe ya jiji  Dubai ambapo unaambiwa alikodi  boat kwa dola elfu 24,000 kwa muda wa siku mbili tu,  na kila alilosema alisikilizwa na lilitekelezwa kwa kasi ya ajabu.  PESA ni  mfalme wa dunia,  ukibisha wewe bisha lakini ndio ukweli wenyewe.

Thursday, October 30, 2014

Mwandishi yafichua machafu ya watu



Wapenzi wa kazi za Haji Dilunga, tarajieni kupata sinema  nyingine ya Mwandishi wa habari. Script nimeandika katika ubora wa hali ya juu, Kama uliburudika na Kwanini Mama  sambamba Jamila na Pete ya Ajabu. Mwandishi ni zaidi ya kile unachofikiria. Ni sinema aliyotumia  muda mwingi kufanya utafiti wa namna ya fani ya habari inavyotumika kwa faida ya wajanja wachache. Ni ujanja gani? Na nani anafanya ujanja huo ni kuitafuta DVD ya sinema  iliyoingia hivi karibuni. Imetayarisha na Kampuni ya Big One Entertainment. Daima ubora kwanza. Kama kawaida imeatungwa nakuandikwa na Haji Dilunga

Kwanini Mama yatoa wengi machozi



Kwanini mama ni sinema inayozungumzia maisha ya watoto wa kiume wanavyowanyanyasa mama zao na kuwasikiliza wake zao. ni sinema yenye mafunzo ya hali ya juu sio vizuri kuikosa. Stori na script ni kazi ya Haji Dilunga.



Jamila bado inatesa sokoni

Ile sinema ya Jamila na pete ya ajabu bado inaendelea kuvutia wengine,kila kukicha wapenzi na mashabiki wamekuwa wakiizungumzia. Ni sinema inayozungumzia unyanyasaji wa watoto. Imetungwa na Haji Dilunga.


                                                           Jamila akicheza na nyani
                                                              Jamila akicheza nyani
                                                    Jamila akipanda ngamia
                                                       Jamila akiwa juu ya ngamia